Rais Samia ashiriki uzinduzi wa Album ya Harmonize Ukumbi wa Mlimani City, leo Mei 25, 2024

Rais Samia ashiriki uzinduzi wa Album ya Harmonize Ukumbi wa Mlimani City, leo Mei 25, 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akishiriki uzinduzi wa album ya Harmonize leo tarehe 25 Mei, 2024 katika ukumbi wa Mlimani City.


View: https://www.youtube.com/live/PafgRqkHmNo?si=oHJtx2WgTWFmEp9k

1000049808.jpg

ALICHOZUNGUMZA RAIS SAMIA
Amemshukuru Msanii Harmonize kwa kumualika kwenye hafla hii aliyoiita 'Usiku wa kuutukuza muziki wa Mama'

Rais Samia ameoneshwa kufurahishwa na ukuaji wa Harmonize kwani alivyo sasa ni tofauti na alivyokuwa miaka 8 nyuma.

Amesema mapito ya kimahusiano aliyopitia Harmonize huwapata vijana wengi, na ametaja baadhi kama Ray Vanny, Ommy Dimpoz na Diamond Platnumz.

Amewapongeza wanawake wote waliolea na kukuza watoto hadi kuwafikisha kwenye mafanikio, wanawake na jeshi makini na jeshi imara.

Amesema amekuwa na kawaida ya kubeba wafanyabiashara kwenye ziara zake, sasa ataanza kwenda na wasanii ili kufungua zaidi nchi na kukuza tasnia hiyo.

Amewasaa wasanii wa muziki na filamu kuwekeza kwenye maisha yao kwani hawatafanya kazi hizo milele. Uwekezaji huo utawasaidia pindi watakapokuwa hawawezi tena kufanya kazi wanazofanya sasa.
 
Msimshangae ndio vitu anavyoviweza.

Hata huo urais ni mzigo kwake maana anasema ndoto yake ilikuwa awe mhudumu kwenye ndege.
😆😆
.... wacha ndugu yangu. Tanzania yetu hiyo.

Elewa kuwa kampeini za uchaguzi zitaanza baada ya muda si mrefu.
Kutakuwa na kitu kikubwa sana watanganyika tulimkosea mwenyezi Mungu.
 
Rais anapenda sherehe huyu.Ila maendeleo ni zero.Hana jipya.
Hivi kweli mlitegemea kitu chochote cha maana kutoka kwa Samia? Mtu mwenye vision anajulika anapoongea. Haya mambo ya kujirusha na wasanii ndiyo mambo anayoweza. Huyo mtu aliyeng'ang'ania Samia aapishwe baada ya kifo cha Magufuli aliikosea sana Tanzania.
 
Back
Top Bottom