Rais Samia atangaza siku 5 za maombolezo kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth aliyekuwa Mkuu wa Nchi ya Tanganyika

Rais Samia atangaza siku 5 za maombolezo kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth aliyekuwa Mkuu wa Nchi ya Tanganyika

Sasa hii ni shobo!

Sisi Rais wetu Magufuli alipofariki Waingereza walitangaza siku ngapi za maombolezo?.

Sisi tumeshafiwa na viongozi wetu wakubwa tu akiwemo Mzee Kawawa , hatujawahi kutangaza siku tano za maombolezo , Huyu Malkia kwetu ni nani haswa hadi tumpe siku zote hizo?

Huu ni utumwa wa Fikra!

Halafu hii serikali mbona inatoa taarifa kwa Umma usiku wa manane, imekuwa serikali ya kichawi?
Tatizo huelewi kiitifaki, Malkia alikuwa nani kwa Tanganyika. Malkia, kabla ya uhuru alikuwa mkuu wa koloni la Tanzania kufuatia Azimio la Umoja wa Mataifa, ambapo Tanganyika iliwekwa chini ya usimamizi wa Uingereza mpaka itakapokuwa tayari kujitawala.

Tanganyika, baada ya mkoloni Mjerumani kuondolewa, mwingireza aliwekwa kama mlezi wa Tanganyika.

Hata baada ya uhuru, Tanganyika/Tanzania imekuwa nchi mwanachama wa Jumuia ya madola. Na mkuu wa jumuia ya madola ni Malkia/Mfalme wa Uingereza.

Kudai kuwa mbona uingereza haikutoa siku za maombolezo kufuatia kifo cha Magufuli, ni sawa leo hii Rais au Waziri mkuu afariki, zitolewe siku za maombolezo, halafu wewe useme kuwa mbona hawakutoa siku za maombolezo kufuatia msiba wa baba yako au mama yako.

Binadamu wote ni sawa lakini tunatofautiana. Samia ni mkuu wa nchi, Biden ni mkuu wa nchi, malkia ni mkuu wa nchi lakini kuna tofauti kubwa. Ukubwa wa mamlaka hupimwa katika idadi ya unaowaongoza/unawahudumia. Malkia alikuwa mkuu wa mataifa mangapi, linganisha na Magufuli alikuwa mkuu wa mataifa mangapi. Kufuatia kifo cha Magufuli, Uingereza ilitoa salamu za rambirambi, kwa nafasi ya Magufuli kama mkuu wa nchi ya Tanzania pekee, ilitosha.
 
Tatizo huelewi kiitifaki, Malkia alikuwa nani kwa Tanganyika. Malkia, kabla ya uhuru alikuwa mkuu wa koloni la Tanzania kufuatia Azimio la Umoja wa Mataifa, ambapo Tanganyika iliwekwa chini ya usimamizi wa Uingereza mpaka itakapokuwa tayari kujitawala.

Tanganyika, baada ya mkoloni Mjerumani kuondolewa, mwingireza aliwekwa kama mlezi wa Tanganyika.

Hata baada ya uhuru, Tanganyika/Tanzania imekuwa nchi mwanachama wa Jumuia ya madola. Na mkuu wa jumuia ya madola ni Malkia/Mfalme wa Uingereza.

Kudai kuwa mbona uingereza haikutoa siku za maombolezo kufuatia kifo cha Magufuli, ni sawa leo hii Rais au Waziri mkuu afariki, zitolewe siku za maombolezo, halafu wewe useme kuwa mbona hawakutoa siku za maombolezo kufuatia msiba wa baba yako au mama yako.

Binadamu wote ni sawa lakini tunatofautiana. Samia ni mkuu wa nchi, Biden ni mkuu wa nchi, malkia ni mkuu wa nchi lakini kuna tofauti kubwa. Ukubwa wa mamlaka hupimwa katika idadi ya unaowaongoza/unawahudumia. Malkia alikuwa mkuu wa mataifa mangapi, linganisha na Magufuli alikuwa mkuu wa mataifa mangapi. Kufuatia kifo cha Magufuli, Uingereza ilitoa salamu za rambirambi, kwa nafasi ya Magufuli kama mkuu wa nchi ya Tanzania pekee, ilitosha.
Tanzania ilikuja mwaka 1964, Wakati huo Malkia hakuwa mtawala tena wa Tanganyika au Zanzibar.

Kama unaleta hoja kuwa Malkia alikuwa mkuu wa nchi ya Tanganyika, alipigiwa kura na mtanganyika gani mpaka akawa mkuu wa nchi yao?. Naona unatetea legacy ya ukoloni!
 
MNATAKIWA MJUE KUANZIA SASA NA KUENDELEA ,KIONGOZ YOYOTE MKUBWA HUANZIA ROHONI YANI UPANDE WA PILI, JUMUHIYA YA MADOLA SIO MNAVYO IJUA NINYI condoo wa mungu
 
Tanzania ilikuja mwaka 1964, Wakati huo Malkia hakuwa mtawala tena wa Tanganyika au Zanzibar.

Kama unaleta hoja kuwa Malkia alikuwa mkuu wa nchi ya Tanganyika, alipigiwa kura na mtanganyika gani mpaka akawa mkuu wa nchi yao?. Naona unatetea legacy ya ukoloni!
Kabla ya uhuru Afrika iligawanyika katika tawala za kikabila, ndiyo maana ilikuwa rahisi kwa wakoloni kuzichukua tawala hizi, kuzigawanya walivyoona inafaa, na kuzifanya kuwa makoloni.

Tanganyika, Uganda, Kenya ilikuwa ni koloni koloni moja la Wajerumani, likijulikana German: Deutsch-Ostafrika) (GEA), na mjerumani alikuwa mtawala wake kwa utaratibu ambao hao wakoloni walikubaliana. Ni mifumo na migawanyo hiyo ya wakoloni, mpaka leo tunaendelea nayo. Wao ndio walituwekea mipaka ambayo mpaka leo tunaendelea kuheshimu kuwa ni mipaka ya nchi zetu, kama vile ilikuwepo kabla ya ukoloni, kumbe haikuwepo.

Ni baada ya Mjerumani kupoteza ushindi kwenye vita ya Dunia ndipo Tanganyika ikawekwa kwenye uangalizi wa Uingereza mpaka itakapokuwa tayari kujitawala. Wakati huo wote, kiongozi mkuu wa Uongereza ndiye alikuwa kiongozi pia mkuu wa Tanganyika na makoloni mengine yote yaliyokuwa chini ya Uingereza. Kwa wakati huo, hao wakoloni walikuwa ndiyo mamlaka halali za kiutawala mpaka pale mataifa mengi yaliyokuwa makoloni yalipogomea mfumo huo. Machifu ambao kabla ya ukoloni, walikuwa ndio viongozi wakuu wa tawala zao, wakafanywa kuwa viongozi wa chini katika mfumo wa nchi ulioacnzishwa na wakoloni.

Siyo kila utawala huwekwa kwa njia ya kura. Hivi hata kabla ya kuja kwa wakoloni, ni nchi gani ya Afrika ilikuwa inawapata viongozi wak kwa njia ya kura? Kwa sababu hakukuwa na upigaji kura, tuseme Afrika nzima haikuwahi kuwa na watawala?
 
Zilipotea Mkuu mambo ya UTAWALA BORA

Two years back...niliiipata ila kwa mbinde sana Mkuu kupitia hukohuko kwao SKOTISHI tena kwa heshima ya Julius upande wa Conservation
Duuu. Kweli hapa kazi tuu
 
Mapaka ya mbali yaliyokuwa yanafadhili utumwa Afrika Mashariki ikiwa ni pamoja na huku Tanzania na kututesa sana kupitia ukoloni yafe halafu tuomboleze?!Haya ni mambo ya aibu na ya ajabu kabisa kutoka Serikali dhaifu na mfu ya CCM🐒🐒🐒
 
Kuna mahala Mwafrica anapaswa kuonyesha hasira zake dhidi ya ukoloni ule na huu uliopo sasa ambao umeendelea zaidi kwa kutumia ndugu zetu kama vibaraka na mkoloni kupandikiza mifumo inayoendelea kutokoloni.
 
Nakuuliza tuliwatuma wafanye hivyo vitu?? Nani kawaleta huku kama sio ujangili wao?

Hakuna njia yoyote ya kumtetea mkoloni atabaki kuwa shetani tu daima.
Ni shetani kwako ambaye hupendi lakini kwa wengine ni binadamu tu kama binadamu wengine na ni chanzo cha maendeleo Afrika na duniani kote.
 
Rais Samia atangaza siku tano za maombolezo kufuatia kifo cha Malkia Elizabeth II kilichotokea tarehe 8 Septemba, 2022.

Maombolezo hayo yataanza tarehe 10 Septemba hadi tarehe 14 Septemba.

Katika kipindi hicho bendera za Tanzania zitapepea nusu mlingoti, ikiwa ni pamoja na kwenye balozi zetu.

Ni jambo la hekima kidiplomasia kuonyesha kama nchi mwanachama wa Jumuiya ya Madola kuwa umeguswa na msiba huo wa kiongozi huyo mkuu wa Uingereza. Baadhi ya nchi zilizoshusha bendera yao nusu mlingoti ni pamoja na Nigeria, Kenya na Ghana.

Tanzania ni kati ya nchi 19 za Afrika zilizopo ndani ya Jumuiya ya Madola ambazo ziliwahi kuwa sehemu ya Ufalme wa Uingereza na zilipata uhuru ndani ya Jumuiya hiyo.

Kwa hiyo, Malkia Elizabeth II alikuwa moja kwa moja mkuu wa nchi, aliyewakilishwa ndani ya nchi na Gavana Mkuu.

Nchi hizo ni


Tanganyika (Tanzania) , 9 Desemba 1961 kama Ufalme - ikawa Jamhuri ya Tanganyika tarehe 9 Desemba 1962, Jamhuri ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar tarehe 26 Aprili 1964, na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania tarehe 29 Oktoba 1964.


Botswana , 30 Septemba 1966 kama Jamhuri

Cameroon , 11 Novemba 1995 kama Jamhuri

Gambia , 18 Februari 1965 kama Ufalme - ikawa Jamhuri tarehe 24 Aprili 1970

Ghana , 6 Machi 1957 kama Ufalme - ikawa Jamhuri ya 1 Julai 1960

Kenya , 12 Desemba 1963 kama Nchi - ikawa Jamhuri tarehe 12 Desemba 1964

Lesotho , 4 Oktoba 1966 kama Ufalme

Malawi , 6 Julai 1964 kama Ufalme - ikawa Jamhuri ya 6 Julai 1966

Mauritius , 12 Machi 1968 kama eneo - ikawa Jamhuri ya 12 Machi 1992

Msumbiji , 12 Desemba 1995 kama Jamhuri

Namibia , 21 Machi 1990 kama jamhuri

Nigeria , 1 Oktoba 1960 kama Ufalme - ikawa Jamhuri mnamo 1 Oktoba 1963 - kusimamishwa kati ya 11 Novemba 1995 na Mei 29, 1999

Rwanda , Novemba 28, 2009 kama Jamhuri

Seychelles , 29 Juni 1976 kama Jamhuri

Sierra Leone , 27 Aprili 1961 kama Ufalme - ikawa Jamhuri 19 Aprili 1971

Afrika Kusini , 3 Desemba 1931 kama Ufalme - aliondoka kuwa Jamhuri tarehe 31 Mei 1961, alijiunga na 1 Juni 1994

Swaziland , 6 Septemba 1968 kama Ufalme

Uganda , 9 Oktoba 1962 kama Ufalme - ikawa Jamhuri tarehe 9 Oktoba 1963

Zambia , 24 Oktoba 1964 kama Jamhuri

Zimbabwe , 18 Aprili 1980 kama Jamhuri - kusimamishwa tarehe 19 Machi 2002, iliondoka tarehe 8 Desemba 2003

Taarifa kamili,

View attachment 2351886
Malawi na Rwanda ni siku 10 😆😆

Cheki hii 👇
 

Attachments

  • Screenshot_20220911-205531.png
    Screenshot_20220911-205531.png
    39.8 KB · Views: 3
Malawi na Rwanda ni siku 10 [emoji38][emoji38]

Cheki hii [emoji116]
Ukiwa mjinga unaweza kuamini kuwa una uwezo wa kujitenga na mzungu, na ukaishi.

Leo hii hao wazungu ndio wanaofanya tuwe na mawasiliano ya haraka kuanzia kusafiri mpaka simu, television, mitambo mbalimbali, n.k.

Mchina pamoja na kupifa hatua katika kuiga teknolojia mbalimbali za wazungu, bado ameshikamana na wazungu kiasi cha kuwa mvutiaji no.1 wa wawekezaji toka Ulaya na America. Mjinga asiteweza kutengeneza hata baiskeli, anaamini anaweza kuishi kwa kujitenga na mataifa ya wazungu.

Wametutangulia, tufanye kazi kwa bidii, tushirikiane nao, huenda siku moja tutawakaribia, au pengine vizazi vyetu vya huko mbeleni vitawafikia. Lakini kwa fikra duni za baadhi ya watu kuwachukia wazungu, ndiyo tutazidi kuwa duni zaidi.

Ni nini ulicho nacho mtu mweusi ambacho kina thamani bila ya hao wazungu?

Tuna mbuga za wanyama, lakini watalii tunaowategemea kwa idadi kubwa ni hao wazungu.

Tuna dhahabu, almasi, tanzanite, wanunuzi wakubwa tunaowategemea ni hao wazungu.

Hata huko Uarabuni, kwenye mafuta mengi, makampuni ya uchimbaji, na soko kubwa la hayo mafuta, ni wazungu.

Hata chanjo za watoto wetu na akina mama wajawazito, bado tunamtegemea mzungu atulipie.

Wazungu wana mabaya yao, lakini matatizo mengi yanayompata mtu mweusi, mhusika mkubwa ni mtu mweusi mwenyewe.
 
mimi kabisa nimsifie huyo alibino alietesa babu zangu ngoja likapugwe mirungu huko
😂😂
 
Back
Top Bottom