Rais Samia atoa bilioni 5.9 kuboresha afya ya mifugo

Rais Samia atoa bilioni 5.9 kuboresha afya ya mifugo

Jamal Akbar

JF-Expert Member
Joined
Oct 9, 2014
Posts
413
Reaction score
471
Katika kuboresha huduma za mifugo na kuiepusha dhidi ya magonjwa, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia matumizi ya jumla ya Shilingi Bilioni 5.9 kwa ajili ya ujenzi wa majosho 257 katika Halmashauri 80, ambapo kati ya hayo tayari majosho 88 yamekamilika.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (Mb) amebainisha hayo katika Kijiji cha Narakauo kilichopo Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, wakati akihitimisha ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo kukagua miradi ya ujenzi wa mabwawa kwa ajili ya mifugo, huku akibainisha majosho ambayo yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi ni 169.

Akizungumza na jamii ya wafugaji Mhe. Ulega amesema katika kuhakikisha lengo na dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuokoa afya ya mifugo ya wafugaji katika mwaka wa fedha 2022/23, vifo vya mifugo vinavyotokana na maradhi ya kupe na ndorobo vimepungua kutoka asilimia 72 hadi 56.

Ameongeza kuwa tayari majosho matano yamejengwa katika Wilaya ya Simanjiro mwaka huu wa fedha, majosho mawili mwaka uliopita na majosho saba yatajengwa mwaka ujao wa fedha.

Aidha, amesema licha ya ujenzi wa majosho serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa dawa ya ruzuku kwa ajili ya kuweka kwenye majosho lita 52,560 kote nchini zenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.3, huku takriban lita 400 zikipelekwa katika Wilaya ya Simanjiro kwa ajili kuzitawanya katika majosho yaliyopo kwenye wilaya hiyo.

Picha na. 1.JPG
 
Tengeni na maeneo ya malisho ya Mifugo, kuondoa kero ya migongano kati ya mkulima na mfugaji...msiishie hapo tu, ndani ya eneo la marisho kuwepo na huduma ya visima vya maji kwaajil ya Mifugo..
Yatengwe mashamba KWAAJILI ya kupanda mbegu Bora za malisho..

Wizara ya Mifugo ni kama Wizara yatima, Huwa inasahaulika sana.
Ukiangalia chat ya nchi zenye idadi nyingi ya Mifugo kwa Afrika, sisi tupo kwenye 3 Bora..
Lakini angalia wizara isivyopewa thamani.
 
Tengeni na maeneo ya malisho ya Mifugo, kuondoa kero ya migongano kati ya mkulima na mfugaji...msiishie hapo tu, ndani ya eneo la marisho kuwepo na huduma ya visima vya maji kwaajil ya Mifugo..
Yatengwe mashamba KWAAJILI ya kupanda mbegu Bora za malisho..

Wizara ya Mifugo ni kama Wizara yatima, Huwa inasahaulika sana.
Ukiangalia chat ya nchi zenye idadi nyingi ya Mifugo kwa Afrika, sisi tupo kwenye 3 Bora..
Lakini angalia wizara isivyopewa thamani.
Una hoja valid kabisa, naunga mkono
 
Nchi ishakwisha hii

Nchi haina fedha kugharamia miradi bali inategemea tajiri bilionea mmoja atoe fedha zake kwa hisani akiridhia.


Huku kwingine tunaelezwa kila siku kuwa Tanzania Sio Masikini kumbe nchi inategemea mfadhili tajiri namba moja kwa kila kitu

1676979306589.png
 
Hili swala la kusema Rais ametoa kila kitu linakera sana, machawa haya hayachoki,mtu ukisema serikali imetoa utakuwa unapungukiwa nini
Vyovyote vile, watumishi wa umma wanafanya kazi kwa niaba ya Rais, na Rais ndio Kiongozi Mkuu wa Serikali, kama ambavyo nyie Chadema Mdude na Maranja Masese ni viongozi wa matusi
 
Tulichelewa kumpata Rais huyu

Ongezea ambaye ni tajiri namba moja Philanthropist mzawa .

Wenzetu huwa wanatambua na kuwaenzi matajiri wanaojitolea kubadilisha maisha ya watu wengi.

BILLIONAIRES

America’s Top Givers 2022: The 25 Most Philanthropic Billionaires​

MÁXIMO TUJA
Forbes Wealth Team
Forbes Staff
Follow
Jan 19, 2022,06:30am EST

From Warren Buffett to newcomer Jeff Bezos, the nation's most generous billionaires have given away a collective $169 billion in their lifetimes–and are still richer than ever.


The billions keep piling up for many of America’s great philanthropists. So, too, do their charitable contributions. The nation’s 25 biggest givers have donated a total of $169 billion over the course of their lifetimes, according to Forbes’ estimates. That’s up from $149 billion last year, partly due to new information uncovered by Forbes—but mostly due to another year of huge giving by these 25 mega-donors.

Leading the pack: Warren Buffett, whose annual summer gift of Berkshire Hathaway stock topped $4.1 billion this year. The funds, as usual, went to The Bill and Melinda Gates Foundation
 
Katika kuboresha huduma za mifugo na kuiepusha dhidi ya magonjwa, Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameridhia matumizi ya jumla ya Shilingi Bilioni 5.9 kwa ajili ya ujenzi wa majosho 257 katika Halmashauri 80, ambapo kati ya hayo tayari majosho 88 yamekamilika.

Naibu Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega (Mb) amebainisha hayo katika Kijiji cha Narakauo kilichopo Wilaya ya Simanjiro Mkoani Manyara, wakati akihitimisha ziara ya kikazi ya siku mbili mkoani humo kukagua miradi ya ujenzi wa mabwawa kwa ajili ya mifugo, huku akibainisha majosho ambayo yapo katika hatua mbalimbali za ujenzi ni 169.

Akizungumza na jamii ya wafugaji Mhe. Ulega amesema katika kuhakikisha lengo na dhamira ya Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuokoa afya ya mifugo ya wafugaji katika mwaka wa fedha 2022/23, vifo vya mifugo vinavyotokana na maradhi ya kupe na ndorobo vimepungua kutoka asilimia 72 hadi 56.

Ameongeza kuwa tayari majosho matano yamejengwa katika Wilaya ya Simanjiro mwaka huu wa fedha, majosho mawili mwaka uliopita na majosho saba yatajengwa mwaka ujao wa fedha.

Aidha, amesema licha ya ujenzi wa majosho serikali ya awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan imetoa dawa ya ruzuku kwa ajili ya kuweka kwenye majosho lita 52,560 kote nchini zenye thamani ya Shilingi Bilioni 2.3, huku takriban lita 400 zikipelekwa katika Wilaya ya Simanjiro kwa ajili kuzitawanya katika majosho yaliyopo kwenye wilaya hiyo.View attachment 2524982
Zipigwe tu
 
Back
Top Bottom