kwani hujui kuwa Samia ni taasisi?Samia naona kawa tajiri sana.
Hebu tuache hizi porojo za kusema raisi katoa kiasi fulani.
Hivi kuna ugumu gani wa kusema raisi kaidhinisha kiasi kadhaa kwaajili ya ujenzi wa kitu A
Kwani Musoma iko wapi?Ingejengwa Butiama kama ilivyojengwa ya Chato ningeelewa. Hii airport ilihitajika siku nyingi ni uzembe tu wasituleee kumuenzi Mwalimu hapa. Kila kitu siasa WaTZ tumekosea wapi?
Kwani Chato ipo wapi? Geita? auKwani Musoma iko wapi?
Hivi Rais anatoa wapi pesa mpaka tuseme kwamba Rais katoa kiasi hiki na hiki kufanya mradi fulani? Are we serious?RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATOA TZS 35BL KUJENGA UWANJA WA "MUSOMA AIRPORT " ILI KUMUENZI HAYATI BABA WA TAIFA KWA VITENDO.
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma karibu na Sehemu alikozaliwa muasisi wa Taifa hili Mwl Julius Kambarage Nyerere,
Serikali sikivu ya Rais Samia Suluhu Hassan imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma uliotelekezwa na awanu zote tangu Uhuru,
Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua mkoa wa Mara,,Uwanja huu pia utahudumia na maeneo ya jirani kama Simiyu na Mwanza,
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma|Mara na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo kwani kabla Watalii wengi walishuka uwanja wa KIA,
Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.
Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.
Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakika hakuna kama Rais Samia Suluhu Hassan,
Nashangaa siasa zimebadilika na kusifia mtu badala ya wananchi. Kodi ni zetu leo imekuwa ya Rais tulimuweka sisi leo kageuka tajiri anatoa fedha mifukoni Mwake hovyo hii kabisa.Hivi Rais anatoa wapi pesa mpaka tuseme kwamba Rais katoa kiasi hiki na hiki kufanya mradi fulani? Are we serious?
Seriously waTanzania tunahitaji kubadilika tujitambue. Tunaona kila kinachofanywa na watawala kama tunafanyiwa hisani wakati ni kodi zetu.
Hii yote ni legacy ya mwendazake kuamini kwamba bila yeye maendeleo tutayasikia na kuyaona kwingine. Hii tabia imeanza kipindi cha Mwnedazake.
Leo katangulia kwa muumba wake..Tanzania si ipo na inaendelea kudunda?
Tubadilike. Tujiamini! Watawala watakuja na kuondoka. Tanzania itakuwepo mpaka mwisho wa dahari!
Masanja,
Kwani hujui Rais anafanya badala ya Wanachi?Nashangaa siasa zimebadilika na kusifia mtu badala ya wananchi. Kodi ni zetu leo imekuwa ya Rais tulimuweka sisi leo kageuka tajiri anatoa fedha mifukoni Mwake hovyo hii kabisa.
He/She should not take all the credits by naming him/her, better say the GOV has given the money to finance this and that and not the president. The actual allocation of funds is approved by Parliament not even the president why naming him/her, it looks as if it's a favor while it is the right of the people.Kwani hujui Rais anafanya badala ya Wanachi?
Hapa umebadili tu lughaHe/She should not take all the credits by naming him/her, better say the GOV has given the money to finance this and that and not the president. The actual allocation of funds is approved by Parliament not even the president why naming him/her, it looks as if it's a favor while it is the right of the people.
mwenye ubongo ndivyo ilivyo, asiye na ubongo atakubishiasikia, sote tunampenda mama, lakini ninachotajiru kukwambia ni kwamba, hizo hela hajatoa mfukoni mwake, hana hela kama hizo. ni hela za serikali, sema serikali imetoa. over.
Nimefurahi sana comment yako, sorry lugha gomgana.Hapa umebadili tu lugha
Kwani hiyo miaka 20 unayosema kuhusu Rwanda kuna uongozi wa juu umebadilika halafu mwelekeo wa taifa ukabaki vilevile? Rwanda is has a one man show leadership for over 20 years now.Tanzania kamwe hatutaendelea hivi karibuni ikiwa hatuna mwelekeo wala dira katika uongozi wa nchi. Kila rais ajaye anabuni mambo yake. Baya zaidi ni mambo haya ya kujitakia sifa. Uwanja wa ndege ni huduma/kitega uchumi, haujengwi kwa sababu ya kmuenzi mtu, yeyote. Sidhani kama kuna mtaala wowote uliofanywa juu uwanja huo utarudisha vipi pesa za watoa kodi. Inaelekea pesa za Watanzania zaamuliwa na mhumuko mmoja tu na mapenzi ya mtu! Nchi itaendelea vipi hivyo?
Natoa mfano wa Rwanda: kwa miaka 20 tu iliyopita Rwanda imepiga hatua kubwa sana ya kuigwa. Bila shaka sababu kuu ni kuwa kuna mwelekeo, dira na uongozi usobadilika badilika kama kinyonga.
Pili: Kwa nini kajiwanja kama haka kajengwe na Wachina? Jamani. Inadhi sana. Si muagize vyombo tu msivyonavyo? Mainjinia chungu nzima wapo. Walieni tu nusu ya mnavyowalipa Wachina watafanya kazi zaidi ya Wachina. Mbona Waafrika hatujiamini hivi?
RAIS SAMIA SULUHU HASSAN ATOA TZS 35BL KUJENGA UWANJA WA "MUSOMA AIRPORT " ILI KUMUENZI HAYATI BABA WA TAIFA KWA VITENDO.
Huu ni muonekano wa baadhi ya vifaa vya ujenzi vya mkandarasi Beijing kutoka nchini China ambavyo vinatarajiwa kutumika katika kazi za maboresho ya uwanja wa ndege wa Musoma karibu na Sehemu alikozaliwa muasisi wa Taifa hili Mwl Julius Kambarage Nyerere,
Serikali sikivu ya Rais Samia Suluhu Hassan imesema inatarajia kutumia kiasi cha TZS 35BL ili kuboresha uwanja wa ndege wa Musoma uliotelekezwa na awanu zote tangu Uhuru,
Maboresho hayo ni pamoja na kuweka lami na kuongeza urefu wa uwanja huo ili kuruhusu ndege kubwa na ndogo kuweza kutua mkoa wa Mara,,Uwanja huu pia utahudumia na maeneo ya jirani kama Simiyu na Mwanza,
Mkuu wa Wilaya ya Musoma, Dkt. Khalfani Haule, amesema kuwa mradi huo ukikamilika utarahisisha huduma za usafiri na usafirishaji kwa wananchi wa Musoma|Mara na pia kuchochea biashara ya utalii kupitia Hifadhi ya Taifa ya Serengeti ambayo ipo mkoani humo kwani kabla Watalii wengi walishuka uwanja wa KIA,
Ameongeza kuwa Uongozi wa Wilaya tayari umejipanga kwa kuupokea mradi huo na wameahidi kutoa ushirikiano wa kutosha kwa Mkandarasi huyo kwa kumpatia eneo la kuchimba mchanga na kokoto za ujenzi.
Naye, Meneja wa Uwanja wa ndege wa Musoma, Mohammed Bakari, amesema kuwa uwanja huo utajengwa na Kampuni ya kikandarasi ya Beijing kutoka China na unatarajiwa kukamilika mwezi Desemba, 2022.
Amefafanua kuwa Mkandarasi huyo tayari ameshawasilisha vifaa vyake katika eneo la mradi kwa ajili ya kuanza rasmi ujenzi huo, na kusisitiza kuwa ujenzi wa uwanja huo unasimamiwa na Wakala wa Barabara Tanzania (TANROADS), mkoa wa Mara.Hakika hakuna kama Rais Samia Suluhu Hassan,
Daahkatoa kwani zake za mfukoni ndugu?
Safi Sana mzalendoMtupe basi na connection za kufanya hapo airport kama kujenga uwanja na mambo mengine
Rais ni taasisi, Mzigo ni wakoUjinga ni Mzigo. Mh. Rais anatoa wapi hizo Fedha?.??