Mkanganyiko kukanganya
JF-Expert Member
- Jun 26, 2022
- 1,204
- 5,053
Zipo sheria Tanzania ba mama kasema zifatwe.Haendi kwa papara kwakuwa CAG sio wa kuaminika?πππππ
Katibu mkuu ndiye msimamizi mkuu, wa taasisi zote zilizo chini ya wizara yake na ana wajibu wa kupitia hoja za CAG na kuzipatia majibu....Sasa kwanini Rais akaagiza hao makatibu wakuu wawachunguze wa chini yao na ikibidi hatua dhidi yao zichukuliwe?
Inawezekana vipi hao wasaidizi kufanya jambo bila kushirikishwa makatibu wakuu? na kama makatibu wakuu walishirikishwa, kwanini wawachunguze hao wasaidizi ikiwa nao ni sehemu ya tatizo?
Ulitaka Rais afanye nn kwani?Inashangaza sana, kwanini Rais anawaagiza makatibu wakuu na watendaji wakuu wahakikishe wanapitia ripoti na kuwawajibisha wale waliohusika na uzembe?
Yeye kama Rais anachukua hatua gani kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe wakiwemo mawaziri?
Alichokifanya Rais hapo ni sawa na kufunika kombe mwanaharamu apite, sioni jipya, kapanua magoli hao jamaa wapate visingizio.
Wajinga hao wanaumia mioyoni ndugu zao wanaochemsha wanaposhughulikiwa.Mtaendelea kuumbuka kwa kudra za Mungu na udini wenu huo mpaka basi!
Huyo ni mjinga kweli kweli.Ni mjinga tu anaewaza mambo kwa mgongo wa UDINI...
Tumlaumu NyerereBado haitakuwa suluhisho.
Moja ya suluhisho kubwa ni kumpunguzia rais madaraka makubwa aliyonayo ikiwemo madaraka ya kuteua ma CEOs karibu wote. Madaraka haya yapunguzwe yapelekwe bungeni na kwenye mhimili wa mahakama....maana yake hapo ni katiba mpya.
Usiwe na haraka basi!Da!Katibu Mkuu na Makatibu yeye na Mawaziri tusubiri tuone.Haraka ya Nini Kamanda.Vipi kwa hao wakuu waliosimamia huo uzembe na ubadhirifu, mamlaka yao ya uteuzi na nidhamu ni nani?
Hivi unategemea hao wakuu watakuwa tayari kuwatoa sadaka wasaidizi wao watakaobainika kufanya uzembe?
Sababu kwa akili ya kawaida tu, kama wasaidizi wakibainika kusababisha uzembe, swali litakuja, je, wakuu wao walikuwa wapi hadi huo uzembe kutokea?
Alichofanya Rais hapa ni muendelezo wa kulindana, sioni jipya; wakuu watawalinda wasaidizi wao waliofanya uzembe, kama ambavyo Rais nae anawalinda wakuu wao waliosimamia uzembe, mwishowe mbwa mwitu wataendelea kututafuna kila siku.
Huyo ndio mhusika mkuu, TGFA ndiye mnunuzi kwa niaba ya serikali, ndege zinaponunuliwa anasaini yeye upande mmoja na mtendaji wa ATCL upande mwingine.Huyu bwana anahusika na ununuzu wa ndege za ATCL? Bodi na management za ATCL hazihusiki?
Hii maana yake Rais haoni tatizo, anaelekeza kitu gani ambacho yeye hakioni?
Naona mnatumia kigezo cha "utaratibu na sheria" ili kuzubaisha watu, na kulindana tu, na bahati nzuri kwasababu nae hapendi kuhangaisha kichwa chake ...
TAKUKURU sio independent wanashakizwa kukamata vidagaa.
Ila rais anakusanya maoni ipo siku hii itakuwa independent maana wamemchezea na kashawaelewa.
Kuna mtu hataki kufanya kazi yakeKulingana na taarifa ya Ikulu ikiwaelekeza watu hao kusoma report ya CAG na kuchukua hatua kwa wahalifu imekaaje?
Naona kama mbwa kala mbwa !
Maruweruwe hapa sielewi!
Badala ya kuagiza TAKUKURU wanagizwa wakurungenzi!View attachment 2582586
Sio wote wanaojua kuhusu "principles of natural justice"Ungekuwa wewe ungefanyaje? Unazijua kazi na majukumu ya katibu mkuu kwenye wizard?
Duh watz wajuaji sana. Sasa hizi si ndio hatua zenyewe jamani ??? Mlitaka Whitwell wanyongwe bila hata kusikilizwa
Mkuu hizi ni dana dana tu. Chama ni kile kile Serikali ni ile ile Majizi ni wale wale Bunge ni lile lile kibogoyo. Hakuna jipya.Kwani hizi anazochukua sio hatua? Kumbuka Rais Huwa hana mihemko na hataki kumuonea mtu.
Ukweli ukibainika wote wataondoka.