Mtakumbuka awamu ya tano ya Hayati Dk John John Joseph Pombe Magufuli tulifanikiwa kununua jumla ya ambulance 117,awamu hii ya Sita ya Rais Samia Suluhu Hassan tumeagiza ambulance brand new 395 || Kaziindelee
" Hakuna kama Samia "
Rais mpole na mnyenyekevu Samia Suluhu Hassan,Rais anayethamini na kulinda Utu na Uhai wa Watanzania wote bila kujali dini,kabila,rangi wala kanda kwa kutumia Economic Stimulus relief fund toka IMF ameagiza zinunuliwe Jumla ya Toyota Land cruiser ambulance mpya 395 pamoja na magari mapya 214 kwaajili ya Chanjo aina zote 15 ikiwemo chanjo ya Corona,Hakika kumbeza Rais Samia nikujitafutia laana za bure kwa Mungu.
Mtakumbuka awamu yetu ya tano katika kutekeleza Ilani ya CCM tulifanikiwa kununua Toyota Land cruiser ambulance mpya 117 na hapa tuendelee kumuenzi na kumwombea pumziko jema Mwanamwema wa Africa Hayati Dk John John Joseph Pombe Magufuli kwa kazi kubwa na nzuri alizozifanya kwenye sekta hii ya afya nchini,
Kwakuwa Tanzania tuna jumla ya Wilaya 139 na zote zina hospitali za Wilaya baada ya hizi ambulance kufika kila Hospitali ya wilaya itapata ambulance mpya ( brand new) kwaajili ya kunusu roho za Watanzania hawa masikini kwa kuwakimbiza kwenye hospitali za juu yao ( referral hospitals )
Kwakuwa Tanzania pia tuna jumla ya Halmashauri 184 ikiwemo Ushetu tulikoshinda kiti cha Ubunge kwa kishindo majuzi kwa hesabu hii ya ambulance 395 kila halmashauri itapata ambulance mpya kwaajili ya kuhudumia ama za Kituoa cha afya ama Zahanati zao kwaajili ya rufaa za wagonjwa wao kwenye hospitali za Wilaya, Watu wa Idara ya afya tunzeni sana mali hizi,
Ambulance hizi 395 ni mara tatu zaidi ya ambulance zote 117 zilizonunuliwa kwa miaka mitano yote ya awamu ya tano ,kwa wenye kumbukumbu nzuri mtakubaliana na mimi kuwa jambo hili halijawahi kutokea katika historia ya nchi hii,
" kama kuna mtu wa kumwombea kwa nguvu zote kwa sasa basi ni Rais Samia Suluhu Hassan "
VIVA SAMIA VIVA || VIVA TANZANIA VIVA