Rais Samia: Awamu ya 5 heshima iliyokuzwa ni ya uoga kwa sababu kulikuwa na Simba wa Yuda, ukimgusa sharubu anakurarua, hatukukua kivile

Haishangazi maana wewe ni kati ya wale wanyonge
 
Simba wa Yuda au Simba wa Chato-Rubondo

Simba wa Yuda ni Yesu Kristo
 
Dunia ina amani kutokana na uvumilivu wa imani tulionao wakristo na hilo halina ubishi. Sijapendezwa kabisa na kauli hiyo ya Simba wa Yuda hata kama ni alikuwa mkali kama simba ni bora angeitwa hata simba wa Chato
Kwani SIMBA WA YUDA ni nani??
Huyo YUDA ni nani??
Maana Simba anajulikana ni mnyama hatari.
 
Kwani SIMBA WA YUDA ni nani??
Huyo YUDA ni nani??
Maana Simba anajulikana ni mnyama hatari.
Yuda ni moja ya watoto wa Yacob au Israel ambayo ni moja wa Kabila 12 za Israel na Yesu ni mzawa katika kabila la Yuda na ni mfalme na ufalme wake unafananishwa na mnyama Simba. Kwa nini Simba? Simba ni mnyama mwenye nguvu na jasiri sana na pia ni mfalme wa Pori.
 
Pia Simba huwakilisha ufalme uliokengeuka. Usiomtambua Mungu wa Israel Yehova.

Daniel sura ya 7. Imetaja mnyama mwenye kinwa kama cha simba mwenye miguu mwili. Ufalme wa Babel
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…