Rais Samia awastukia Chawa, aanza kufuata ushauri wa Askofu Bagonza

saidoo25

JF-Expert Member
Joined
Jul 4, 2022
Posts
624
Reaction score
1,456
RAIS Samia Suluhu Hassan ametangaza rasmi kuruhusu kukosolewa baada ya kilio cha muda mrefu cha wananchi na viongozi wa dini kuwa amezungukwa na watu wanaomsifu kama njia ya kumdanganya asione changamoto za nchi.

Hatimaye sasa Rais Samia amewastukia watu hao na kuruhusu rasmi kukosolewa kama njia ya kuona changamoto na kuzirekebisha.

"MH RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AWE MACHO SANA NA WATU WENYE HULKA YA KUMSIFIA KAMA NJIA YA KUMDANGANYA ASIWEZE KUONA UDHAIFU AU CHANGAMOTO ZA NCHI" Askofu Bagonza

Your browser is not able to display this video.
 
Ukiwa umezungukwa na Chawa kama 5 tu aina ya Lucas mwashambwa, aisee unaweza ukafikiri wewe ni bonge la Kiongozi/Mtawala!!

Maana hao Chawa wa desturi ya kumpamba mtu, mpaka wanapitiliza.
Mimi huwa naongea ukweli kwa ushahidi na siyo kuandika tu Kama stori,Mambo aliyoyafanya mh Rais wetu mpendwa mama Samia kiutendaji ni makubwa Sana na yanayoonekana mbele za mtu yeyote mwenye kuona na asiye taka kujipa upofu wa makusudi
 
Kusifiwa na mtu aina ya Kigwa, unayejua kabisa yupo tayari kusema lolote ili arudi kwenye system lazima ushtuke kama kweli unajipenda, kuna watu wako tayari kuonekana makatuni ilimradi warudi kwenye v8 walizozimisi baada ya kuondolewa uwaziri.
 
Najaribu sana kujiweka mbali na kuhoji elimu za watu humu lakini pia nawaza Uhuru wa kutoa maoni
 
Baba Askofu hongera kwa kusamsaidia Rais wetu kuwajua wabaya waliomzunguka
 
Rais Samia Suluhu anamaono ya mbali na ndio maana ana sikiliza maoni ya wananchi alafu unakuta mtu anasema eti mama hajaachia uhuru wa kutoa maoni mama anasikiliza maoni na ya kuyafanyia kazi
 
Watumishi wa Mungu ndio hawa sasa.

Hawa ni akina Yeremia wa enzi zetu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…