Rais Samia awatembelea Mzee Makamba, Mama Maria Nyerere pamoja na Familia ya Marehemu Membe leo 14 Julai 2023

benzemah

JF-Expert Member
Joined
Nov 19, 2014
Posts
1,533
Reaction score
3,187
Kwa nyakati tofauti leo Julai 14 2023 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametembelea na kumfariji Mama Dorcas Membe Mjane wa Waziri Mstaafu wa Mambo ya Nje Hayati Bernard Membe nyumbani kwake Mikocheni Jijini Dar es Salaam.

Rais Samia pia amemtembelea Katibu Mkuu Mstaafu wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Mzee Yusuf Makamba nyumbani kwake Wazo Jijini Dar es Salaam.

Vilevile Rais Samia amemtembelea kumsalimia na kumjulia hali Mjane wa Baba wa Taifa Mama Maria Nyerere nyumbani kwake Msasani Jijini Dar es Salaam.





 
naona mama Nyerere kavaa masks, ha-take chances, we are living in dangerous times …
 
Mama bado anaamini corona ipo
 
Vipi Kwa Janetth Magufuli anaenda lini?
 
F
Full pendo. Yaani watu wenye tamaa wangetukosesha Rais mzuri sana wallah.
 
Bibi mkubwa ni hakika isio na shaka anapenda kutembea!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…