Rais Samia awatumbua Wakurugenzi wa Halmashauri wanne kwa ubadhirifu wa Fedha zikiwemo za UVIKO-19

Rais Samia awatumbua Wakurugenzi wa Halmashauri wanne kwa ubadhirifu wa Fedha zikiwemo za UVIKO-19

John Haramba

JF-Expert Member
Joined
Feb 4, 2022
Posts
365
Reaction score
1,374
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan akiwa njiani kutoka Mwanza kwenda mkoani Mara, leo Ijumaa ametangaza kutengua uteuzi wa wakurugenzi wanne wa Halmashauri ya Buchosha, Iringa, Mbeya na Singida Mjini baada ya kubainika kutumia vibaya fedha za UVIKO-19.

---


Rais Samia Suluhu Hassan amewatengua Wakurugenzi wa Halmashauri nne kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na amesema Mkurugenzi wa Geita kama akikutwa na ubadhirifu pia tataenguliwa

Wakurugenzi waliotenguliwa ni Mkurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya Mjini na Singida Mjini. Utenguzi umefanyika baada ya Waziri wa OR-TAMISEMI Innocent Bashungwa kusema wanafanya uchunguzi wa haraka kwa wakurugenzi walioripotiwa kufanya ubadhirifu

Halmashauri ya Buchosa ilikuwa chini ya Mkurugenzi Paulo Malala, Mkurugenzi wa Iringa ni Limbe B. Limbe, Mkurugenzi wa Singida Mjini ni Zefrin Kimolo Lubuva, na Mbeya Mjini ni Amede E.A Ngwanidako
 
Rais Samia Suluhu Hassan amewatengua Wakurugenzi wa Halmashauri nne kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na amesema Mkurugenzi wa Geita kama akikutwa na ubadhirifu pia tataenguliwa

Wakurugenzi waliotenguliwa ni Mkurugenzi wa Buchosa, Iringa, Mbeya na Singida Mjini. Utenguzi umefanyika baada ya Waziri wa OR-TAMISEMI Innocent Bashungwa kusema wanafanya uchunguzi wa haraka kwa wakurugenzi walioripotiwa kufanya ubadhirifu.

Halmashauri ya Buchosa ilikuwa chini ya Mkurugenzi Paulo Malala, Mkurugenzi wa Iringa ni Limbe B. Limbe, Mkurugenzi wa Singida Mjini ni Zefrin Kimolo Lubuva, na Mbeya
 
Mama Samia amewatengua wakurugenzi wanne wa halmashauri za Buchosa, singida mjini, Itinga na Mbeya kwa matumizi mabaya ya pesa za Uviko.

Mama Samia nakuunga mkono kwa 100%, kwa kuwa hizi pesa watakaokuja kuzilipa ni wananchi hivyo zinapaswa kutumiwa vizuri ili kuleta maendeleo.

Mfuko wa cement unauzwa 21000 lakini mkurugenzi anaenda kununua kwa 24000. Haya ni matumizi mabaya ya pesa za wananchi na n Bora umeliona hili, japo hapo mwanzo walikuwepo washabiki wakawa wanatetea humu sijui Leo watasemaje.

Mama Samia endelea kuhakikisha kila pesa ya serikali kwenye miradi haipotei.

Lakini pia usiishie kuwatengua tu unaweza kwenda mbali kwa kuwawajibisha zaidi ili kuzuia wengine kujipimia kwa urefu wa kamba zao.




Screenshot_20220204-123225_1.jpg
 
Hao kosa lao itakuwa wamekula wakavimbiwa, Rais hapendi hilo anataka ule kwa kiasi.

Huyo mkurugenzi wa Iringa sio yule alieshutumiwa kwa ubakaji siku chache zilizopita? kama ndie akapumzike tu, yeye alikuwa hachagui vyakula anabugia chochote.
 
Usiombe kujikuta uraiani ghafla bin vuuuh!!

Pole sana kwao waliokuwa wakurugenzi , Hongera sana kwa Rais Samia kusimamia maslahi ya Taifa!

Liwe fundisho kwa wengine wenye tabia hizo
 
Rais Samia Suluhu Hassan amewatengua Wakurugenzi wa Halmashauri nne kutokana na tuhuma za matumizi mabaya ya fedha na amesema Mkurugenzi wa Geita kama akikutwa na ubadhirifu pia tataenguliwa....
Huyu Limbe B. Limbe ni juzi tu hapa kulikuwa na uzi wake humu mfanyakazi wa kike akilalamika kuliwa na jamaa baada ya kuleweshwa madawa!
 
Back
Top Bottom