Rais Samia awekeze kwenye utawala wa sheria, katiba mpya na tume huru ya uchaguzi

Rais Samia awekeze kwenye utawala wa sheria, katiba mpya na tume huru ya uchaguzi

Katiba mpya iko tayari, na inasemekana Kikwete wakati anaachia kiti alimwachia magu aipitishe hiyo katiba mpya, magu nae kimyaaaaaaa kama maka umauti umemkuta.

Haya sasa Mama samia tunaomba aipitishe, asiwasikilize wapumbavu ambao roho zao zimejaa kutu.
 
Suala la katiba mpya lisitazamwe kwa fikra za upenzi wa vyama bali kwa fikra za upenzi wa Taifa letu.

Katiba inatakiwa imfae mwananchi yeyote awaye bila ya kujali itikadi. Watu wanaofikiria kuwa katiba ni suala la vyama vya upinzani, wanafanya makosa makubwa. Wasichojua, hata kama leo wewe ni mwanaCCM kindakinda, au kiongozi wa Serikali, bila katiba bora, huna uhakika na lolote katika maisha yako.

Tunataka watu wawe na uhakika na maisha yao. Wajione wapo salama kama hawajavunja sheria. Wajione wana fursa alimradi wana uwezo na nia ya kuzitumia fursa zilizopo. Watu wasiishi kwa hisani, wasizitumia fursa mbambali za maisha kama hisani. Thamani ya utu na ubinadamu wao isiwe ni kwa hisani ya kiongozi/mtawala.

Wazambia walikuwa na katiba iliyokuwa inampa madaraka makubwa Rais. Vyama vya upinzani na wanaharakati mbalimbali walilalamika, lakini walipuuzwa. Kaunda na Serikali yake wakaanguka kwenye uchaguzi. Chiluba, japo wakati wa kampeni aliahidi akishinda, atabadilisha katiba, alipoingia madarakani, hakubadilisha. Aliitumia katiba ile ile ya Kaunda, kumweka ndani Kaunda na mwanasheria wake mkuu wa Serikali. Kilio kikabadilika.
 
Hivi vyeo fake hivi !! kodi za watanzania kutumika hovyo hovyo

Naombeni tuanzishe movement ya kudai katiba mpya kabla ya 2025

Haiwezekani rais awe na mamlaka makubwa ya kuteuwa watu zaidi ya elfu 1

Yaani ni mambo ya ajabu kweli

Lazima twende street tudai katiba aisee
Upo sahihi kabisa mkuu
 
Ni baada ya utafiti wa ndani tena ndani ya CCM ,ni hivi kuna makundi na haya makundi ndio yale yale ,na hatari iliyopo ni Samia kupigwa na chini na kama akipita basi CCM itapoteza viti vya wabunge vingi sana na watapoteza uwingi wao ndani ya bunge.

Kinachofanyika ni kuwa CCM ipoteze ,hivyo kuepuka hilo ni lazima iwepo tume huru itakayokubalika na vyama vyote,ili kudhibiti wizi wa kundi linalompinga Samia,kundi ambalo bado limo kwa wingi ndani ya tume ya Uchaguzi Tanzania nzima.

2025 si mbali tena kimikakati. CCM wakitaka washinde basi hili kundi la Tume ya Uchaguzi

walisambaratishe na mapema.
 
Hakuna kada wa ccm aliye tayari kukubali uwepo wa Tume Huru ya uchaguzi au uwepo wa Katiba Mpya. Wanajua siku zote Tume Huru ya uchaguzi ndiyo kaburi lao.
 
Katiba mpya iko tayari, na inasemekana Kikwete wakati anaachia kiti alimwachia magu aipitishe hiyo katiba mpya, magu nae kimyaaaaaaa kama maka umauti umemkuta.

Haya sasa Mama samia tunaomba aipitishe, asiwasikilize wapumbavu ambao roho zao zimejaa kutu.
Katiba Mpya tunayoitaka sisi ni ile Rasimu ya Jaji Warioba. Hiyo iliyopitishwa na ccm baada ya ukawa kususa, haina tofauti kubwa na katiba ya sasa ya mwaka 1977!

Naunga mkono hoja. Katiba Mpya ni muhimu kwa hapa tulipofikia. Tungekuwa na Katiba Mpya, watu kama akina Joshua Nassari, wangefanya kazi kwa bidii! badala ya kuishi kwa kutegemea UTEUZI.
 
CCM watawaachia wapinzani viti vya ubunge kama kawaida, ila ikulu itabaki kwao vyovyote iwavyo, Tume Huru ndio tumaini pekee la upinzani kuingia ikulu nikiwa naamini hilo ndio lengo namba moja la upinzani makini Tz, sio wapinzani opportunist.
 
CCM watawaachia wapinzani viti vya ubunge kama kawaida, ila ikulu itabaki kwao vyovyote iwavyo, Tume Huru ndio tumaini pekee la upinzani kuingia ikulu nikiwa naamini hilo ndio lengo namba moja la upinzani makini Tz, sio wapinzani opportunist.
Tume huru sio kwa ajili ya vyama. Ni haki ya watanzania wote.
 
Mkuu makundi ccm hayakuanza leo.yapo muda mrefu labda ww ni mgen kwenye siasa za nchi hii.Nakuhusu tume huru sahau hskuna tume huru wala katiba mpya.
 
Back
Top Bottom