miji yote mizuri imejengwa na wafanyabiashara wakihindi na waarabu .Sisi miji yetu ni kama Mtoni kwa azizi ally, vingunguti, keko akida ,buguruni na msasani ya mmakonde. tumeshindwa hata kuweka shule za secondari na maktaba maeneo hayo! mtu anakaa vingunguti shule asome tambaza au shaaban robert, hatuoni hapo bado tunabudi stepu?
Amin Amin nawaambieni kuja jenga Dodoma lije kuwa jiji la kuvutia kama mfuko wa yohana{johanesburg} au Cairo pana hitaji adhabu ya kifo kwa wwahujumu uchumi. kwa kadili utakapo peleka pesa nyingi katika miradi ndipo na maofisa wa serikali nao wanalipana posho za kiajabu ajabu,safari imprest,vikao vya tender, na mishahala lukuki. ndio maana utakuta JPM alikuwa anafuatilia mpaka machinjio mapya ya vingunguti yanavyoendelea ili awatishe wahujumu uchumi.