Midimay
JF-Expert Member
- Apr 12, 2015
- 3,036
- 5,039
Yeye pengine na wasaidizi wake pale jumba jeupe, kina Katanga wanadhani wapenda pesa wanaogopa kelele. Hata kidogo. Wapenda pesa wakipata nafasi, hawajali uliwaamini au hukuwaamini! Hawajali Rais ana huruma au hana! Dawa ya wapenda pesa za dili ni kuwanyima nafasi ya kupiga pesa za dili tu.Rais wangu mama Samia Suluhu Hassan kuendesha serikali yenye kupata mafanikio si jambo la lelemama hata kidogo,kama unatafuta kupendwa,fahamu utapendwa na wachache ila utachukiwa na wengi sana na mwisho wa siku historia itakuhukumu.
Nikupe mfano,kwa kinachoendelea bandarini ,kama ukweli uko seriously,mkurugenzi wa bandari na mkrugenzi wa TRA unapaswa kutengua nafasi zao haraka sana,ili tujue uko mguu sawa ,wanasubiri nini ofisini?
Pili Kitendo cha kumrudisha January Makamba pamoja na bodi nzima ya tanesco iliojaa watu wasio na weledi na ambao huko nyuma wamehusika kwa namna flani kulihujumu taifa, tegemea kashifa nyingine kwenye uongozi wako huko mbeleni .hapa umeingizwa chaka.
Mambo bado kabisa,kuendesha serikali hii inahitaji kuwa na roho ngumu sana .Hayati Magufuli hili alilifahamu sana na ndio maana aliteua na kutengua kila uchao.
Nimalize kwa kusema, kwa kuwa wewe ni mwenye huruma na macho yako ni ya huruma kabisa tegemea na wewe kuhurumiwa ndani ya uongozi wako,
Wamejipanga ,walipukutishwa wanazirudisha kwa kasi na pia hawakumalizwa
Lakini pia umeibua jambo muhimu. Mwenyekiti wa Bodi sio mtendaji wa day to day wa Taasisi yoyote. Mwa hiyo mamlaka haiwezi kumwajibisha bodo halafu ikamwacha Mtendaji Mkuu wa Taasisi(DG wa TPA hapa na DG wa MSCL) kwa sababu mamlaka ya kinidhamu ya Mwenyekiti wa Bodi ndio hiyo hiyo Mamlaka ya Kinidhamu ya DG.