Rais Samia: Demokrasia ni kuheshimu Sheria, heshima ya Mtu inakuja kwa kuheshimu Sheria za Nchi, ombi la Zitto kuhusu kesi ya Mbowe lajibiwa

Misimamo ktk mambo ya haki sio kiburi.Kiburi ni kuharibu heshima ya haki ktk jamii kwa kutumia madaraka vibaya.Rais anastahili heshima.Lakini ukweli,haki na uadilifu una heshima kuliko nafasi ya Urais.Rais anapaswa kuwa mlevi wa HAKI ili apate heshima anayostahili.Huwezi kuminya HAKI halafu unataka watu wafuate sheria ambayo imeewekwa kidemokrasia.Demokrasia huanza badae sheria inafuata.
Demokrasia na sheria
Sheria hutungwa ili kufuata demokrasia.
 
Heshima haina gharama. lakini nyie mnaona matusi ni mtaji.
Mnashindwa vipi kuheshimu wengine ili muheshime.. hivi akili zenu zina akili kweli.
MaCCM toka lini mkawa na heshima.. pumbavu..
 
Hii ni kauli ya Zitto Kabwe Jana akiwa clubhouse.

Wanasiasa bwana Sasa Jana alimwombea Nini kwa Raisi wa nchi?

Kimsingi kisiasa Mbowe ni Baba wa Zitto.
 
Zitto aliongea aliyoongea ili kupaka mkate wake siagi.
 
Sawa mkuu......

Tujikite kwenye mzizi wa mada hii.....

Kuratibu au kuendesha vitendo vya kigaidi ni kosa kisheria na anayefanya anakuwa amevunja sheria.......kauli ya raisi kuwa kama hangevunja sheria angekuwa hapa nadhani ameakisi na kesi inayoendelea mahakamani dhidi ya tuhuma za Mbowe.......

Kuheshimu sheria ni pamoja na kujipusha na vitendo au matukio yanayopelekea uvunjifu wa sheria......

Kwa mujibu wa utaratibu wa nchi yetu mahakama pekee ndio chombo Cha kutoa haki.....

Kuhusu kusameheana bila shaka amelenga mamlaka aliyokuwa nayo kama mkuu wa nchi kuhusu misamaha dhidi ya wafungwa na sio kesi zinazoendelea mahakamani.......
 
Kuna maswali muhimu ya kujiuliza
Afuate sheria gani? Kavunja sheria gani?
Amheshimu nani? Ni nani kamkosea heshima?
Kwahiyo kesi yake sio ugaidi tena? Bali ni maswala ya sheria na heshima?
Kwa kweli Rais leo kanifungua macho. Nilikuwa najiuliza sana juu ya ugaidi wa Mbowe. Inakuwaje Mbowe awe gaidi? Leo nimepata jibu toka kwa mama. Akina Mama wana majibu. Kasema kosa la Mbowe ni kutofuata sheria na kumkosea heshima mtu fulani. Kazi tuliyonayo na mawakili wa mbowe watusaidie kumtafuta huyo ambaye alimshitaki Mbowe kwa kumkosea heshima.
 
Kwani imeshathibitika kwamba Mbowe aliratibu vitendo vya ugaidi? Mbona kesi inaendelea sasa.
 
Kwani imeshathibitika kwamba Mbowe aliratibu vitendo vya ugaidi? Mbona kesi inaendelea sasa.
Hapana mkuu sijasema kuwa Mbowe amethibitika kuwa ni gaidi bali nimeichukulia kama mfano kutokana kauli ya mama....
 
Sasa kwanini watu wanamwombea msamaha mbowe kwa Mama? Mbowe kamfanyia kosa gani mama?
Nadhani ni hulka tu na mitazamo ya watu juu ya jambo hilo.....lakini kimantiki kesi ya Mbowe ipo mahakamani na itaamuliwa kwa mujibu wa sheria.,....
 
Nadhani ni hulka tu na mitazamo ya watu juu ya jambo hilo.....lakini kimantiki kesi ya Mbowe ipo mahakamani na itaamuliwa kwa mujibu wa sheria.,....
Lakini mbona Mama anaonyesha kama vile hatima ya Mbowe ipo mikononi mwake vile? kwa mba amevunja sheria na hayamheshimu, katika lipi?
 
Lakini mbona Mama anaonyesha kama vile hatima ya Mbowe ipo mikononi mwake vile? kwa mba amevunja sheria na hayamheshimu, katika lipi?
Hapana nina hakika hana maana hiyo kwa kuzingatia kuwa yeye ni muumini wa utawala wa sheria......nadhani watu ndio wamechagua kumuelewa hivyo......
 
Misingi ya uzalendo ndo ipi hiyo?
 
Hapana nina hakika hana maana hiyo kwa kuzingatia kuwa yeye ni muumini wa utawala wa sheria......nadhani watu ndio wamechagua kumuelewa hivyo......
Sina uhakika kama umemsikiliza vizuri. Majibu yake yana ujumbe ambao unaonyesha wazi kabisa kwamba Mbowe ana hatia kwa sababu kavunja sheria na amekosa heshima. Mimi naona angejibu tu kwamba hilo la Mbowe tuiachie mahakama, basi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…