Rais Samia: Demokrasia ni kuheshimu Sheria, heshima ya Mtu inakuja kwa kuheshimu Sheria za Nchi, ombi la Zitto kuhusu kesi ya Mbowe lajibiwa

Rais Samia: Demokrasia ni kuheshimu Sheria, heshima ya Mtu inakuja kwa kuheshimu Sheria za Nchi, ombi la Zitto kuhusu kesi ya Mbowe lajibiwa

Hivi wanavyofanya sasa chadema inaweza sababisha Mh.Mbowe asiachiwe.
Ingewatosha kunyamaza watu ambao mwisho wao ni maneno tu hata kujaribu kuandamana kutetea mwenyekiti hawakuweza. They are very weak opposition. Lkn maneno yao utasema Duh kimewaka.
Ikiwa Mbowe hana hiyo jinai na wahusika wanajua hilo lakini hawakiri ukweli ni bora aachwe muda utaongea kwani njia ya mwongo ni fupi. Unaombaje msamaha kwa kosa usilotenda?

Sent from my Nokia 6.1 using JamiiForums mobile app
 
Nadhani wachangiaji wengi hawakuelewa kauli ya mama.........

Kufuata sheria ni pamoja na kuacha mhimili wa mahakama ifanye kazi yake.....

Mbowe ametuhumiwa kwa ugaidi na makosa mengine na kesi yake ipo mahakamani hivyo ni vyema Sheria ikaachwa ichukue mkondo......

Kumtaka rais aingilie uhuru wa mahakama kwa kumtoa Mbowe ni kudharau mhimili wa mahakama......

Macho na masikio yote ya wazalendo n wapenda demokrasia ni huko mahakamani.....huko ndiko tutashuhudia namna gani Mbowe ataidhalilisha serikali kama kweli tuhuma zake ni za kubambikia....
Wewe unaamini tuna mahakama? Hiyo unayoiita mahakama, ina tofauti gani na ofisi ya mkuu wa wilaya au mkoa?
 
Ni kuicha mahakama iwe huru basi...kwani nini shida ,Nyie ngojeni siku akisamehe wa upande wake mje mtupigie makelele humu...
 
Mbowe hayupo juu ya sheria, ameshtakiwa kisheria atahukumiwa kwa sheria na kama akishinda ni kwa sheria. Sio kwamba akishinda alikuwa kaonewa ni kwa sababu ametumia udhaifu wa sheria
Well said, Kina nanii wanvyo lalama apa utazani ni kwamba yeye hayupo kabisa chini ya Katiba ya Jamuhuri au yeye ni exceptional kiasi cha kuombewa msamaha kwa raisi wakati tayari swla liko mahakamani na mahakama haijatoa uamuzi.
 
Suala la Mbowe halina mashiko yoyote,na kadri mnavyozidi kumshikilia ndivyo atakavyozidi kuwaumiza.Ni kama kukumbatia kaa la moto.
Kama hamjaelewa basi endeleeni mtaelewa mbele.
Mnautafutia uongozi wenu aibu isiyo lazima.
Truth be told.Haina kumung'unya maneno.
 
Kuna maswali muhimu ya kujiuliza
Afuate sheria gani? Kavunja sheria gani?
Amheshimu nani? Ni nani kamkosea heshima?
Kwahiyo kesi yake sio ugaidi tena? Bali ni maswala ya sheria na heshima?
Ningependa kuongezea:

na Heshima maana yake nini?
 
Mimi ningependa Mbowe afungwe jela na kifungo chake ndicho kitapelekea Watanzania kwa wingi kukiondoa chama changu cha CCM madarakani kwenye uchaguzi ujao wa mwaka 2025.

Huu ni mtizamo wangun

Ninavyousoma huu mchezo, mimi naona viashiria vinaonesha kuwa Mbowe na wenziwe ni lazima watafungwa halafu baada ya muda si mrefu Samia atawapa msamaha!!! Ndio siasa ilivyo, lakini kifungo hicho kitamuimalisha Mbowe kisiasa zaidi nchini which will be detrimental to ccm.
 
My take; kumbe Mbowe yupo ndani kwa kuwa kuna mamlaka imetaka iwe hivyo!
Daah! Imekuwaje tumefanikiwa kumfanya mtu mmoja awe juu ya kila kitu hadi ile mifumo huru ya kimahakama ya kutoa haki??
 
Africa bado haijawa na sifa ya kuwa na Rais Mwanamke! Wanawake siku zote wana mtizamo hasi kwa kila jambo wanalokosolewa, wakikosolewa hufikiria kwamba, wametendewa hivi kwa vile ni Wanawake. Na wataiacha hoja ya msingi, na kuanza kupayuka huku wakitafuta kutoa adhabu. Tangu lini huyu Rais, akaweza kukabiriana na changamoto za siasa na uongozi bila kuzua balaa!?

Pamoja na ubabe wa Magufuli, hakudhubutu kumfunga Mbowe gerezani, Mama huyu ameonesha udhaifu mkubwa, hatufai. Hatahivyo, ni vema aende kwao Zanzibar, atuachie viongozi wetu wa Tanganyika!
Umejisahaulisha kesi ya kifo Cha Akwilina eeeh!!!
 
Ukiwa na akili ndogo Ni vigumu Sana kumuelewa lissu. Anajua madhara ya kuomba eti huruma ya rais kumtoa mbowe wakati mbowe Hana Hilo kosa. Lkn usipomuelewa lissu utabaki kumuona Ni mkorofi, Kumbe mwenzio anaona mbele zaidi.

Implicit kwenye maombi ya Zitto kwa Samia kuwa amuachie Mbowe ni kwamba Mbowe kweli ana makosa ya UGAIDI!! Je Mbowe Kweli ni GAIDI?
Mnaomfahamu Zitto mnadhani alifanya hivyo kwa nia njema? Zitto maisha yake yote ya kisiasa ni mnafiki!!!
 
Akakimbia bwana. Aliyemkimbiza leo yuko mavumbini nani mjanja?? Lissu asingekimbia siku ile wote wangekuwa udongoni Yeye na Jiwe
Hakuna kitu hapo! Najua unataka kusema Lisu mjanja? Vip kwa waliokufa wote ni wajinga sie ni wajanja kisa tuko hai? Nyie CHADEMA ndo maana mnaitwa nyumbu na mataahira!
 
Viongozi serikalini wao wanafata Sheria? moja tuu,
Je,uchaguzi Wetu huwa ni huru na haki ?
 
Back
Top Bottom