Rais Samia: Demokrasia ni kuheshimu Sheria, heshima ya Mtu inakuja kwa kuheshimu Sheria za Nchi, ombi la Zitto kuhusu kesi ya Mbowe lajibiwa

CCM acheni tabia ya kuona nchi hii n yenu Kwan kati ya wapinzani na nyinyi CCM nani anavunja sheria?alieharibu uchaguzi wa mwaka Jana ni nani?msione wenzenu hawana akili na ipo siku mtafikishwa mahakamani.Sasa hivi mtu kupata haki yake imekua kama hisani .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna maswali muhimu ya kujiuliza
Afuate sheria gani? Kavunja sheria gani?
Amheshimu nani? Ni nani kamkosea heshima?
Kwahiyo kesi yake sio ugaidi tena? Bali ni maswala ya sheria na heshima?
Kushangilia kifo cha Magufuli wazi wazi kwenye ile hotuba yake,nadhani ni worst mistake Mheshimiwa mbowe alifanya.
 

Rais Samia: "Mbowe afuate sheria halafu awe na Heshima"

haya maneno hajatamka Mh. rais umemnukuu vibaya, tuache kumlisha maneno Rais

Rais amesema "Heshima ya mtu inakuja kwa kuheshimu sheria za nchi, unapovunja sheria ya nchi heshima yako taitaheshimiwa, serikali haitakuheshimu, lkn ujue kwamba unapotumia uhuru wako mwisho wa uhuru wako unaanza heshima kwa mtu mwingine" haya ndio nimeyasikia mimi, haya habari ya Mbowe afuate sheria afu awe na heshima imetamkwa wapi hapo?

tuache kufanya mambo kwa nia mbovu!!
 
Kwa hiyo kosa la Mbowe ni kutokufuata sheria na kutokuwa na heshima!

1) Sheria gani aliyoivunja?

2) Heshima gani aliyokosa, na kwa nani?

Ndiyo maana tunasema hii nchi tunaongozwa kihuni. Rais akihisi au akafanyiwa chochote ambacho hakikumfurahisha, unakamatwa na kufanyiwa chochote. Ukiwekwa ndani na kupelekwa mahakamani kwa kesi ya kubumba kama alivyofanyiwa Mbowe, ni bahati. Maana unaweza kufanyiwa kama alivyofanyiwa Lisu, Kinguye, Azory au Ben Sanane.

Katiba mpya inahitajika sana sasa kuliko wakati mwingine wowote.
 
angalau hata hiyo nafasi imepatikana na leo tunaweza kupata habari....sasa ZZK naye asingeenda au wote tungesusia hiyo habari tungeitoa wapi...
Sumarai usudanganyike hiyo n paned nkijikosha tu hamana kitu,ameona mbinyo umekua mkubwa kimataifa .Huyu mama Sometimes anayumba .

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kuna maswali muhimu ya kujiuliza
Afuate sheria gani? Kavunja sheria gani?
Amheshimu nani? Ni nani kamkosea heshima?
Kwahiyo kesi yake sio ugaidi tena? Bali ni maswala ya sheria na heshima?
Mama uwezo n mdogo na hama kitu hapo Sasa afate sheria ipi Tena wakati mikitano ya kisiasa ni takwa la kisheria?pia katiba mpya ni takwa la Wananchi na sio la Mbowe,Kati yake na Mbowe nani anaeipenda Tanzania?Mbowe n mzalendo kwa Sababu kama mwaka2025 yakitokea ya mwaka Jana basi nchi itanwaga damu.Hicho ndo Mbowe hataki kitokee .Hii nchi sio ya Samia ni Nchi ya Watanzania wote.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwan sheria haiongelei suala la ugaidi??? Otherwise ungekuwa na point
Tatizo wewe hata Kiswahili hujui.

Aliposema kufuata sheria, maana yake ufuate sheria unapofanya mambo yako.

Kwa uelewa wako mdogo, unamaanisha Rais alikusudia kumwambia Mbowe afuate sheria anapotaka kufanya ugaidi?

Ni dhahiri, anamaanisha kuwa Mbowe kuna kitu akifanya, na kwa mawazo yake, hakufuata shwria wala hakumtii. Ndiyo maana tunataka kujua jambo gani alilolifanya Mbowe bila kufuata sheria, na kipi ambacho yeye Samia anaona Mbowe hakumtii.
 
Mama aliona Mbowe kama anataka kumpanda kichwani kwa kampeni yake ya katiba mpya.

Hapa inadhihirisha tuhuma za Mbowe ni za kubumba.... Na pia kumwonyesha tu kuwa huwezi kushindana na serikali
Huyo mama anayumba kama kweli ana unasili akaze asimtoe tuone ataendaje

Sent using Jamii Forums mobile app
 
kwa hiyo ugaidi wa Mbowe ni kukosa heshima kwa kudai katiba.
usikute Mbowe alipigiwa simu na mama kuombwa aache harakati za katiba,akamwambia mama acha ufala 🀣🀣🀣🀣
Mtanzania mpe picha tu maelezo atatoa yeye πŸ™„πŸ™„πŸ™„
 
Kuna kitu mbowe wamepishana na Samia.
Kila kiongozi akiingia madarakani Kuna watu lazma atawanyoosha.
Mimi nakumbuka magufuli na manji.
Kikwete na Babu seya.
Kiufupi hyo kesi wametengeneza na wanaweza kumfunga.maana wamedhamiria
Amfunge aone. Atakuwa amempiga chura teke.
 
Kwahiyo kutokua na heshima ndiyo sababu ya kubambikiwa kesi ya ugaidi??

Ndiyo mlikua mnataka Chadema wahudhurie huu mkutano wa kipuuzi namna hii??
 
Mh. Zitto nadhani leo ndiyo kaelewa urais ni taasisi na siyo mtu. Ajifunze na yeye kuwa na adabu. Maana alidhani atasema kiurahisi tu Mbowe atolewe. Mbowe yeye asubiri kama ilivyokuwa kwa Sabaya. Maana mlifurahi sana kwa Sabaya. Inabidi tufike pahala hii nchi iendeshwe kwa misingi ya uzalendo
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…