Iselamagazi
JF-Expert Member
- Sep 26, 2011
- 6,020
- 6,161
Yego mwamba!Tunataka kujiaminisha zaidi kuwa makosa ni ya wapeleka majina peke yao, lakini anaeteuwa pia anatakiwa kuyapitia kwa kina kama kweli tunamlipa mshahara wa kodi zetu kwa kazi hizo...haya ni majina, vipi kuhusu vitu vingine ambavyo vyaweza hatarisha maisha ya watanzania,aweza pelekewa na hao tunaosema wanamhujumu,kwa kuwa havipitii kwa kina,atasaini tu ikaja kuleta shida alafu tuseme anahujumiwa
Siyo kumtumbua tu pia kumchukulia hatua kali.Mkuu umeliona hilo!! laiti kama mama hangekuwa na mauzoefu ya kazi za kiofisi jamaa angekuwa RS. Kwa mapungufu haya 3 ningekuwa ndio mimi, huyo msaidizi wangu wa masuala ya documention ningemtumbua.
Ujanjaujanja Umerudi Tena
Hiyo tabia ya kulala na mafaili sidhani kama ilitusaidia, labda ilimsaidia aliyekuwa nayo!alikuwepo mtanzania mmoja (sasa ni hayati) yeye aliwahi sema alikuwa analala na mafaili kitandani,akiamka anayapitia kwa kina...labda tumshauri huyu Rais wetu nae ajenge utaratibu wa kusoma kwa kina( umesema watanzania hatupendi kusoma) labda na yeye yumo kwenye kundi letu la kutosoma vitu
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Bungeni mkuu kwa mzee wa Kongwa, maana haingii akilini uongoze mkoa/ofisi yenye watu wenye elimu zao wakati ni form four B.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Nenda kwenye mawizara, serikalini wasomi wenye Degree, Masters na PhD wamejaa tele wala huhitaji kuwasha tochi, fomu four anatoboa vipi kwenye nafasi ya RAS, yaani mtu mwenye qualifications za kufanya usafi maliwatoni anakuwa RAS, are we serious? mnataka kuua kabisa hii nchi..
Kwa watu kama hawa ambao makosa ya kibinadamu yanafanyika kwenye teuzi zao na hatimaye kutenguliwa, nashauri kama raia wa JMT, baada ya kutenguliwa teuzi zao, wawe wanapozwa kwa kutafutiwa nafasi nyingine mbadala inayoendana na kiwango cha elimu yao, iwapo tu kutenguliwa huko kunakuwa hakujatokana na sababu zingine zaidi nje ya eimu yao; ili kukwepa kuya-frustrate maisha yao yaliyoko mbele yao, na familia zaoMoja kwa moja nimpe mama Samia hongera kwa kurekebisha makosa yaliyofanyika kwenye teuzi za makatibu tawala na zile za wakurugenzi wa mashirika mfano ile teuzi ya DG wa TPDC.
Ni wazi Kuna majina mama anayopewa ya teuzi yakiwa na makosa. Ieleweke mama Samia hawezi kuwajua watu wote hivyo ni wazi lazima wengine awe hajui historia zao. Juzi aliteua makatibu tawala na kwa bahati mbaya kulikuwa na jina la Azza Hilal Hamad ambae aliteuliwa kuwa katibu tawala mkoa wa simiyu.
Hapa kulikuwa na tatizo kwa kuwa elimu ya huyu Azza ni ndogo na isingekuwa vyema kwenda kuwa katibu tawala. Katibu Tawala mkoa ndio mtendaji, anahitaji mwenye elimu ni Bora ingekuwa nafasi ya mkuu wa mkoa au wilaya maana hizo hazihitaji Sana wasomi.
Mama Samia pia angalia kwa jicho la pili aina ya majina unayoletewa maana hii ikiendelea utawapa nafasi wapinzani wako wapate upenyo wa kukutukana Sana.
Nakupongeza sana kwa kurekebisha haya makosa mapema sana, maana wengeenda huko kazini ingekuwa ni kituko. Pia Kama Kuna wengine uliletewa majina na hawapo vizuri watengue tu, ni Bora lawama kuliko fedheha.
Nafikiri mama hatataka kuingizwa chaka kwenye hizi nafasi za kiutendaji ndo maana anabadirisha haraka sana akigundua jambo haliko sawa, na hata kwenye nafasi za kisiasa bado atataka kuwa na watu competent....kwa hiyo wachomekaji wasifikiri watafanikiwa na inaweza kuwagharimu wao wenyewe.Kwa watu kama hawa ambao makosa ya kibinadamu yanafanyika kwenye teuzi zao na hatimaye kutenguliwa, nashauri kama raia wa JMT, baada ya kutenguliwa teuzi zao, wawe wanapozwa kwa kutafutiwa nafasi nyingine mbadala inayoendana na kiwango cha elimu yao, iwapo tu kutenguliwa huko kunakuwa hakujatokana na sababu zingine zaidi nje ya eimu yao; ili kukwepa kuya-frustrate maisha yao yaliyoko mbele yao, na familia zao
Moja kwa moja nimpe mama Samia hongera kwa kurekebisha makosa yaliyofanyika kwenye teuzi za makatibu tawala na zile za wakurugenzi wa mashirika mfano ile teuzi ya DG wa TPDC.
Ni wazi Kuna majina mama anayopewa ya teuzi yakiwa na makosa. Ieleweke mama Samia hawezi kuwajua watu wote hivyo ni wazi lazima wengine awe hajui historia zao. Juzi aliteua makatibu tawala na kwa bahati mbaya kulikuwa na jina la Azza Hilal Hamad ambae aliteuliwa kuwa katibu tawala mkoa wa simiyu.
Hapa kulikuwa na tatizo kwa kuwa elimu ya huyu Azza ni ndogo na isingekuwa vyema kwenda kuwa katibu tawala. Katibu Tawala mkoa ndio mtendaji, anahitaji mwenye elimu ni Bora ingekuwa nafasi ya mkuu wa mkoa au wilaya maana hizo hazihitaji Sana wasomi.
Mama Samia pia angalia kwa jicho la pili aina ya majina unayoletewa maana hii ikiendelea utawapa nafasi wapinzani wako wapate upenyo wa kukutukana Sana.
Nakupongeza sana kwa kurekebisha haya makosa mapema sana, maana wengeenda huko kazini ingekuwa ni kituko. Pia Kama Kuna wengine uliletewa majina na hawapo vizuri watengue tu, ni Bora lawama kuliko fedheha.
Unalala Na mafaili we we ni kichaa? Ubongo wenye afya ni ule unaopata muda wa kutosha wa kupunzika.Hiyo tabia ya kulala na mafaili sidhani kama ilitusaidia, labda ilimsaidia aliyekuwa nayo!