Rais Samia, Katiba Mpya ndio suluhu ya matatizo ya Watanzania

Rais Samia, Katiba Mpya ndio suluhu ya matatizo ya Watanzania

Lord OSAGYEFO

JF-Expert Member
Joined
Feb 19, 2021
Posts
3,085
Reaction score
4,890
Rais Samia Suluhu Hassan kwanza nakupongeza sana kwa hatua mbalimbali unazochukua baada ya kuondokewa na Magufuli Mhe. Rais kama lilivyo jina lako wewe ndio Suluhu ya suala la Katiba mpya.

Haya yote unayohangaika nayo kuyaweka sawa ni kutokana na Mwendazake kuona mapungufu yaliyopo kwenye katiba iliyopo ndio ikawa rahisi kwake kuyafanya aliyoyafanya. Nadhani hata wewe utakumbuka hayati Baba wa Taifa aliwahi kusema Katiba hii ilimpata rais dikteta atawaonea wananchi na hilo limetimia kwa Mwendazake.

Rais samia "legacy" yako pekee sio kujenga zahanati au kupandisha mishahara bali ni kuwapatia wananchi katiba mpya nakuhakikishia rais samia utakumbukwa kwa miaka hata 50 ijayo rais mstaafu Jakaya Kikwete pamoja na kuwa hakufanikiwa kutupatia katiba mpya lakini vizazi vinamkumbuka kwa uthubutu wake wa kuanzisha mchakato kwani alisema katiba iliyopo ina miaka 50 na mambo mengi yamebadilika.

Mungu ambariki sana.
 
Hivi vyeo vinanivuruga sana katika utendaji wao. Haya mamilundikano ya vyeo Wilaya moja ya nini haya. Hapa ije katiba mpya tu hakuna jinsi.
Kila awamu wanakuwa na majukumu yao, unaweza kupata details kutoka
  1. Hai
  2. Iringa
  3. Mbeya
  4. Dar nk
 
Hivi vyeo vinanivuruga sana katika utendaji wao. Haya mamilundikano ya vyeo Wilaya moja ya nini haya. Hapa ije katiba mpya tu hakuna jinsi.
Kazi yao ni kutafuna hela!
 
Vyeo vingi Sana for nothing kwa uelewa wangu wa hizo nafasi RC, RAS, DC, DAS hawana kazi za msingi zaidi tu ya kula fedha za Serikali
Ifike wakati vyeo hivyo vifutwe abaki DED, Municipal Directors, na City Directors tu na Ofisi za TAKUKURU wilayani ziongezewe uwezo ziwasimamie hao watu
 
Iwe ni kuwa na bunge lenye meno na ambalo litakuwa wajibu wa kuiwajibisha serikali lazima watanzania tukomae tupate katiba mpya.

Iwe ni kudhibiti wanasiasa waovu ambao walishageuza nchi yetu kama shamba la bibi kuvuna na kuiba mali za umma. Tunahitaji katiba mpya.

Kulinda na kutetea haki za kila mtanzania dhidi ya maovu ya udhalimu wa wakora wa kisiasa na wanaoua, kutesa na kuletea maumivu watanzania. Tunahitaji katiba mpya.

Katiba mpya itafutwe kwa kila namna, iwe kwa maandamano, makongamano, elimu na kuhamasisha watanzania wote bila kujali itikadi zao.

Katiba mpya ndio suluhu la matatizo ya taifa letu. Tupate katiba ambayo itaruhusu raisi, spika, waziri , Igp na kiongozi yoyote kushitakiwa kama akifanya kosa.
 
Iwe ni kuwa na bunge lenye meno na amabalo litakuwa wajibu wa kuiwajibisha serikali lazima watanzania tukomae tupate katiba mpya.

Iwe ni kudhibiti wanasiasa waovu ambao walishageuza nchi yetu kama shamba la bibi kuvuna na kuiba mali za umma. Tunahitaji katiba mpya.

Kulinda na kutetea haki za kila mtanzania dhidi ya maovu ya udhalimu wa wakora wa kisiasa na wanaoua, kutesa na kuletea maumivu watanzania. Tunahitaji katiba mpya.

Katiba mpya itafutwe kwa kila namna, iwe kwa maandamano, makongamano, elimu na kuhamasisha watanzania wote bila kujali itikadi zao.

Katiba mpya ndio suluhu la matatizo ya taifa letu. Tupate katiba ambayo itaruhusu raisi, spika, waziri , Igp na kiongozi yoyote kushitakiwa kama akifanya kosa.
Inspekta Ndowo ameshadukuwa Mtu huku siyo bure.
 
Back
Top Bottom