Rais Samia kuanza Ziara ya Siku 3 Nchini Ghana. Hii ni ziara ya 12 tangu aingie madarakani

Rais Samia kuanza Ziara ya Siku 3 Nchini Ghana. Hii ni ziara ya 12 tangu aingie madarakani

Wakuu Mwanzo Nilileta Uzi Wa kwanba Hangaya anasafiri Kwenda India, Ni Ghana na Sio India.

Rais Samia ameondoka Nchini Kuelekea Accra, Ghana kwa ajili ya Ziara ya kikazi ya siku tatu Nchini Humo.

======

Rais Samia anatarajiwa kuondoka leo kuelekea Accra Ghana kwa ziara ya kikazi ya siku 3 nchini humo.

Rais anatarajiwa kushiriki mdahalo wa Wakuu wa Nchi utakaojadili fursa zilizomo na changamoto zinazozikabili nchi za Afrika ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabia ya nchi, kupanda kwa bei ya vyakula na matumizi ya nishati endelevu.

Aidha anatarajia kupokea tuzo ya mwaka 2022 ya Babacar Ndiaye kwa mafanikio ya ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji ambayo hutolewa kila mwaka kwa Mkuu wa Nchi iliyofanya vizuri zaidi.

Watanzania tuchangamkie cocoa za Ghana ni nzuri sana pia watatusaidia kubuni vazi la taifa.
 
Kuna shughuli gani ya kiuchumi, kibiashara au kiteknolojia kati ya Tanzania na Ghana?

tunaweza kushare experience kwenye mining business, walianza siku nyingi kufanya mining na wana sera nzuri kiasi fulani kuwanufaisha na kuna makampuni makubwa mengi sana ya uchimbaji wa dhahabu..

Pia walianza kuwa na oil refinery plant siku nyingi sana, wakifanyia refinery mafuta ya Nigeria huku wazarishaji wenyewe wa mafuta Nigeria wakiwa hawana refinery baadala yake wanachimba crude inakwenda refinery Ghana wanapata diesel, petrol na kerosene...Japo Nigeria nao sasa wanajenga Refinery kupitia Tajiri Aliko Dangote..

Ni nchi pia ambayo Siasa za chama tawala na upinzani sio za kijinga kama huku, siasa ni za watu serious kidogo na yeyote kutoka chama chochote anaweza kupewa nchi na mambo yakaenda smooth tu...

Vipo vingi vya kujifunza na kushare uzoefu kwa Ghana...
 
Wakuu Mwanzo Nilileta Uzi Wa kwanba Hangaya anasafiri Kwenda India, Ni Ghana na Sio India.

Rais Samia ameondoka Nchini Kuelekea Accra, Ghana kwa ajili ya Ziara ya kikazi ya siku tatu Nchini Humo.

======

Rais Samia anatarajiwa kuondoka leo kuelekea Accra Ghana kwa ziara ya kikazi ya siku 3 nchini humo.

Rais anatarajiwa kushiriki mdahalo wa Wakuu wa Nchi utakaojadili fursa zilizomo na changamoto zinazozikabili nchi za Afrika ikiwa ni pamoja na kuongezeka kwa athari za mabadiliko ya tabia ya nchi, kupanda kwa bei ya vyakula na matumizi ya nishati endelevu.

Aidha anatarajia kupokea tuzo ya mwaka 2022 ya Babacar Ndiaye kwa mafanikio ya ujenzi wa miundombinu ya usafirishaji ambayo hutolewa kila mwaka kwa Mkuu wa Nchi iliyofanya vizuri zaidi.

Ataenda India akotoka Ghana 👇

Screenshot_20220523-121527.png
 
Huyu mama kwa Safari atapewa Tuzo ya Oscar na Nobel

Machinga wanafukuzwa, watumishi wanakwiba Mali za umma,

Yeye Ni Safari tu Kila wiki ,

Hii nchi tulilaaniwa, Rais alikuwa JPM tu
Rais Samia hajawahi fanya ziara za hasara

Machinga wanafukizwa kwenda wapi?

Na wewe ka kwibe uone moto 👇

Screenshot_20220523-121217.png
 
Mama anapenda safari kama nini!
Mabalozi awamu hii wanakula bata, wanafuatwa kutafuniwa kila kitu huko wamebaki na mapokezi airport na cocktails, ndiyo maana wanajirekodi kucheza muziki hadi jikoni Lilongwe. Huu ni uelewa wa laymen mitaani.

Uelewa wa elites ni kwamba nchi inafunguliwa kimataifa.

Hizi schools of thought mbili ipi ina nguvu?
 
Back
Top Bottom