Rais Samia, kujua ukubwa wa tatizo kutasaidia kuliponya; kundi la wanasiasa liliumizwa sana

Rais Samia, kujua ukubwa wa tatizo kutasaidia kuliponya; kundi la wanasiasa liliumizwa sana

KISHADA

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2012
Posts
2,226
Reaction score
3,291
Nianze hapo. Kumeibuka taswira halisi na Kali baada ya kugusia Katiba Mpya na mikutano ya siasa. Ni kama imeficha mema yote uliyofanya Kwa Siku 100 ulizokaa madarakani.

Sifa zote ulizopata zimefichwa. Mama yetu mpendwa hio ndio taswira ya ukubwa wa tatizo lililopo.

Watakuja makada na washauri wako kupitia taasisi zao wajipendekeze na kukudanganya usione huo ukweli.

Wanasiasa ni wahanga wakubwa Wa awamu ya 5. Na hadi sasa hawajapata tiba sahihi na matumaini.

Hawajasikia kuhusu watu walioteswa, kuuwawa na kupotezwa. Hawa wengi ni wanasiasa. Hawajasikia mwelekeo Wa chaguzi zilizovurugwa Kwa makusudi. Hawajasikia kuhusu Tume ya uchaguzi na usimamizi Wa Wakurugenzi. Hawajasikia Namna Polisi na vyombo vyengine vikitajwa na kuwajibishwa Kwa kutumika kisiasa. Mambo yako wazi mama. Mifumo na sheria za kusimamia haki hazijaguswa kimya.

Katika hali hio, tumaini ni Katiba Mpya na kufuatwa sheria ya vyama vya siasa. Leo unapokuja na kauli zile unatonesha vidonda na kuyakwaruza makovu Kwa viwembe.

Nadhani ujumbe baada ya kauli ile umefika. Nia yako njema kwa Taifa hili inatazwa na hayo mawili.

Jitahidi kuwa makini na washauri wako. Taifa ni kubwa kuliko CCM. Wanasiasa Kwa umoja wenu ndio hutoa taswira ya nchi. Malalamiko yao hufika haraka kote duniani na nchi kuwekwa rehani.

Hili kundi lina wafuasi wengi na ukweli ni kwamba liliteseka mno.

Jitahidi kuvumilia kama ulivyo, na jitahidi ku-balance mambo.

Nchi hii ni ya wote. Kumbuka ule msamiati kwamba cheo ni dhamana na daima tenda mema uwende zako.

Nawasilisha.

Kishada
 
Hata mimi naungana na hao wanaotaka katiba mpya japo hawaungwi mkono na watu walio wengi. Sababu kubwa ni uelewa finyu wa katiba iliyopo na mapungufu yake.

Ndio maana mchakato mzima wa kudai katiba mpya, unaonekana ni wa kisiasa. Nini cha kufanyika? Uundwe utaratibu maalumu wa kuhakikisha kila mtu anaijua katiba iliyopo na mapungufu yake kisha tuanze kudai katiba mpya tukiwa na nguvu ya wananchi.

Mbali na hapo, hakuna mafanikio maana kila mtu yupo busy kuhakikisha anapata japo tonge moja la ugali.
 
"Jitahidi kuwa makini na washauri wako. Taifa ni kubwa kuliko CCM." Hapo ndo nimepaona mimi
Mifano ya akina Mzee Kabudi na Prof. Shivji inafikirisha.

Viongozi Wa Dini na ile kamati ya a man I ya viongozi Wa dini imethibiti wanatumika kumsaidia mtawala bad ala ya nchi.

Mama endelea kuliponya taifa Kwa njia sahihi.

Tunakushauri utulie zaidi. Wanasiasa waliumizwa. Kuvumiliana ni muhimu
 
Hata mimi naungana na hao wanaotaka katiba mpya japo hawaungwi mkono na watu walio wengi. Sababu kubwa ni uelewa finyu wa katiba iliyopo na mapungufu yake.

Ndio maana mchakato mzima wa kudai katiba mpya, unaonekana ni wa kisiasa. Nini cha kufanyika? Uundwe utaratibu maalumu wa kuhakikisha kila mtu anaijua katiba iliyopo na mapungufu yake kisha tuanze kudai katiba mpya tukiwa na nguvu ya wananchi.

Mbali na hapo, hakuna mafanikio maana kila mtu yupo busy kuhakikisha anapata japo tonge moja la ugali.
Jitihada za mama na kueka alama zitakuwa na maana akirejesha heshima ya nchi ya umoja Wetu na kushirikiana.
 
Walioumizwa nchi hii ni wanasiasa tu? au wao ndio wananchi sana sisi wengine wasindikizaji?
Vipi kama walioporwa pesa zao watatishia kuingia barabarani? watumishi walionyimwa nyongeza nao wakitishia kuandamana, itakuwa nchi hii? Wote tuna majeraha wanasiasa msijikute so special...tunajua mmemiss posho za bungeni na ruzuku ila tujikaze wote tujenge uchumi kwanza.
By the way tukikupa wewe urais unaweza kuponya majeraha yote ndani ya miezi mitatu?
 
Mifano ya akina Mzee Kabudi na Prof. Shivji inafikirisha.

Viongozi Wa Dini na ile kamati ya a man I ya viongozi Wa dini imethibiti wanatumika kumsaidia mtawala bad ala ya nchi.

Mama endelea kuliponya taifa Kwa njia sahihi.

Tunakushauri utulie zaidi. Wanasiasa waliumizwa. Kuvumiliana ni muhimu
Mkuu hongera kwa mada mzuri na kwa wakati sahihi. Hawa viongozi wa dini naona siku hizi wamechukua nafasi ya Wazee wa DAR ambao wapo kwa niaba ya wazee wa Tanzania. Tofauti yao KUU ni moja, viongozi wa DINI wapalilia sana masuala yao binafsi na misamaha ya kodi wakati Wazee wa DAR (si wazee wa CCM) wao wazungumzia masuala uchumi, kisiasa na usalama kwa niaba ya Watanzania wote. Kwa mantiki hiyo asisahau kuzungumza na kupata ushauri kutoka kwa Wazee wa DAR.
 
We mama umeambiwa utanyolewa kama mtangulizi wako [emoji23][emoji23] sasa sijui ni nywele za wapi [emoji119]
 
Walioumizwa nchi hii ni wanasiasa tu? au wao ndio wananchi sana sisi wengine wasindikizaji?
Vipi kama walioporwa pesa zao watatishia kuingia barabarani? watumishi walionyimwa nyongeza nao wakitishia kuandamana, itakuwa nchi hii? Wote tuna majeraha wanasiasa msijikute so special...tunajua mmemiss posho za bungeni na ruzuku ila tujikaze wote tujenge uchumi kwanza.
By the way tukikupa wewe urais unaweza kuponya majeraha yote ndani ya miezi mitatu?
Kimsingi ukiumiza wanasiasa umeumiza watanzania. Hakuna mtanzanua haguswi na siasa ndio maana kila mahali tulifurahi Samia alivyoanza siasa nzuri.
 
Jitihada za mama na kueka alama zitakuwa na maana akirejesha heshima ya nchi ya umoja Wetu na kushirikiana.
Na mwisho wa Siku ya Mungu mengi. Autumie muda huu kufanya jambo jema. Katiba mpya na tume huru itamaliza migigoro mingi rushwa na utapanyaji wa mali za umma.
 
Naam, hivi ndivyo watu wazima hufikiri [emoji1433][emoji1433]

Mama anafanya vizuri, so far.

Lakini haimaanishi hawezi ku improve.
 
Hata mimi naungana na hao wanaotaka katiba mpya japo hawaungwi mkono na watu walio wengi. Sababu kubwa ni uelewa finyu wa katiba iliyopo na mapungufu yake.

Ndio maana mchakato mzima wa kudai katiba mpya, unaonekana ni wa kisiasa. Nini cha kufanyika? Uundwe utaratibu maalumu wa kuhakikisha kila mtu anaijua katiba iliyopo na mapungufu yake kisha tuanze kudai katiba mpya tukiwa na nguvu ya wananchi.

Mbali na hapo, hakuna mafanikio maana kila mtu yupo busy kuhakikisha anapata japo tonge moja la ugali.
Naunga mkono. Watu hawajui hata nini maana ya katiba. Na Kitendo cha Wanasiasa kuchokoza kinaonekana ni hatari kwa watawala. Watawala hawataki wananchi kujua haya mambo.
 
Naam, hivi ndivyo watu wazima hufikiri [emoji1433][emoji1433]

Mama anafanya vizuri, so far.

Lakini haimaanishi hawezi ku improve.
Mleta mada amemaliza kila kitu. Mi sina cha kuongeza.
 
  • Thanks
Reactions: Pep
Siasa ni ngumu sana...
Mno. Hebu fikiria tulivyo. Sheria za vyama IPO kikatiba anatokea MTU Anaisaga. Anauwa vyama Kwa kutengeneza migogoro na kulazimisha kupendwa Kwa nguvu za kidola.

Chaguzi kuporwa live na kulazimishwa kuunga mkono juhudi.

Kivuli hiki kinaishi. Consequence zake ni kunyamazishwa kila aliyepaza sauti, kubambikizia mikesi mikubwa, kuuana, kutesana n.k.

Taifa linakosa umoja, Ku we po visas I na kulipizana.

Mifumo ya haki kulazimishwa visivyo na kusimika udikteta kamili.

Dawa ya haya si kufoka na kunyamazishana Kwa nguvu za madaraka. Wat u walimizwa sana.

Tunatokaje hapa? Mifumo yetu ni mibovu. Tusirembe.

Katiba iwekwe sawa na kujenga utamaduni Mpya Wa kufuata sheria.
 
Back
Top Bottom