Rais Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa

Rais Samia, kuna dalili zote za kuwa na mafuta ziwa Tanganyika na Nyasa

Sasa kuna tatizo. Kutokana na tatizo la mabadiliko ya mazingira (climate change), mataifa makubwa duniani yameweka mkakati wa kuacha kutumia mafuta kwa ajili ya magari na mitambo. Norway kwa mfano, wanasema kufikia 2050 wataacha kabisa shughuli za kuchimba mafuta. Uingereza wanasema watapiga marufuku magari ya kutumia diesel kufikia 2025 nadhani. Japan, Germany na hata China, wote wanasema ndani ya miaka 15 ijayo wanataka kutoka kwenye kutumia mafuta kwenye magari na kuingia kwenye magari ya umeme (from internal combustion engines to electric vehicles)

Sasa hii inamaanisha nini kwa nchi kama Tanzania ambazo hadi sasa zimekalia tu uchumi wa mafuta bila kuuendeleza? Ina maana ndani ya miaka 20 ijayo, mafuta yatakuwa si mali kitu. Hata ukigundua una mafuta mengi kama bahari ya Hindi, hayatakusaidia tena kwa kuwa dunia imeanza kuondoka toka tekinolojia ya mafuta kwenda teknolojia ya umeme!

Hivyo basi, kama kweli tunataka kufaidika na rasilimali ya mafuta tuliyonayo, ni lazima iendelezwe ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo. La sivyo haya mafuta yatakuwa na rasilimali isiyohitajika tena duniani, na ndani ya kipindi cha miaka kumi ijayo tutaanza kushuhudia kuporomoka kwa bei ya mafuta kadiri magari ya umeme yanavyoingia sokoni. Leo hii hata Lamborghini wamesema wataacha kutengeneza gari za mafuta!
Mseveni yuko Dsm mida hii, je anayajua haya? Je ana uhakika hiyo investment itarudisha hizo pesa ndani ya kipindi hicho?
 
Tutatengeneza.Mbona hata kenya tu wanatengeneza magari.
South, Ghana, Nigeria kote wanatengeneza gari.
Kuundda magari sio jambo linalowasumbua waafrika kwa sasa labda ndege.
Kumbuka mafuta yanaweza kubadilishwa kuwa umeme.
Tunabadilisha vp
 
Mawazo yako ni mgando! Wewe unadhani mafuta hutumika kwenye magari tu? Kuna activities kwa maelfu kama siyo malaki hutumia mafuta hapa duniani!
Na wewe akili yako ni mgando. Najua kuna maelfu ya vitu vingine vinavyotumia mafuta, lakini elewa sababu kwa nini kuna msukumo wa kuacha kuchimba mafuta - yanasababisha climate change. Hata process ya hivyo vitu vingine bado itasababisha ongezeko la carbon ambalo ndio wanachotaka kuzuia.

Na pia, unapaswa kuelewa hivyo vitu vingine unavyosema vipo, vinachangia return za kiasi gani katika mafuta yanayochimbwa ili kuchimba mafuta kuendelee kuwa economically feasible? Ni sawa na kusema hata kama nazi zitaonekana zisiliwe tena kwa sababu ya tatizo fulani lililogundulika, watu waendelee kulima nazi kwa kuwa wanaweza kunywa madafu na kutumia makuti kuezeka nyumba na kutengeneza matenga. Hapo ndipo akili yako imeishia.
 
Tutatengeneza.Mbona hata kenya tu wanatengeneza magari.
South, Ghana, Nigeria kote wanatengeneza gari.
Kuundda magari sio jambo linalowasumbua waafrika kwa sasa labda ndege.
Kumbuka mafuta yanaweza kubadilishwa kuwa umeme.
Kwana jiulize kwa nini kuna msukumo wa kuacha takinolojia ya mafuta.

Kisha jiulize, kwa hiyo utachimba mafuta ili uyatumie kwa ajili ya kuzalisha umeme. Una kuku watano, unaagiza ujengewe kisima kwa milioni tano, ambacho utakihudumia kwa laki tatu kila mwezi, ili kuku wako watano wapate maji ya kunywa, sivyo?

Halafu jiulize kama mataifa makubwa yameacha kutumia mafuta, technolojia ya mafuta utakayotaka kuchimba kwa ajili ya generator zako za umeme utaipata wapi.

Halafu unasikia mtu kama wewe umeteuliwa waziri wa uchumi na mipango.
 
Mitambo yote mikubwa na injini zenye ujazo mkubwa tutatumia sana dizeli sio leo sio kesho mafuta kuacha kutumika labda miaka 100 baadae

Bado sioni teknolojia ya kutumia umeme kwenye meli za mizigo,magari makubwa na mitambo hivi karibuni

Halafu watu bado wanatumia mpaka coal ambayo emmisions zake ni mbaya zaidi kuliko mafuta so zutu la muarabu bado lipo lipo sana tu
Kweli kabisa, umeongea point. Lakini sasa, ili kuendelea ku-supply mafuta kwa hizo line za consumption, huhitaji vi-nchi vyenye production ndogo kama Tanzania kuwepo. Hapo ni kitakachotokea ni kushuka kwa bei ya mafuta na kusababbisha kubaki kwa labda supplier wawili au watatu ambao watatosheleza market ya dunia nzima, kwa kuwa production cost zao ni ndogo ukilinganisha na nchi wazalishaji wadogo kama Tanzania. Ndio maana nikasema tutashuhudia bei ya mafuta ikiporomoka with time hadi kufikia kuwa kuchimba mafuta yetu yaliyoko Tannganyika, kuyaleta hadi Dar ili yawe exported, itakuwa haina maana tena.
 
Mkuu kama ni hivyo tumeshachelewa! Tuachane na miradi hiyo.









































































































































































































































alikuwa tayari kulitetea kwa nguvu zote.
Labda Ziwa Tanganyika.
 
Mseveni yuko Dsm mida hii, je anayajua haya? Je ana uhakika hiyo investment itarudisha hizo pesa ndani ya kipindi hicho?
Investment katika mafuta kwa sasa sio tatizo. Ndio maana nikasema baada ya miaka kama kumi hivi itakuwa too late
 
Investment katika mafuta kwa sasa sio tatizo. Ndio maana nikasema baada ya miaka kama kumi hivi itakuwa too late
anyway nilipata kumsikia mtu mmoja alisema bi-products za mafuta zinalipa zaidi kuliko mafuta yenyewe
 
Atakubali Tu , hiyo Saudi Aramco inapumulia mirija Tu sasa hivi , na Qatar na Saudia Arabia wanadiversify uchumi wao kutoka dependency ya mafuta kwenda kwenye utalii NK
Very true. Hata Dubai inabadilika wanatumia hela ya mafuta waliyonayo kuigeuza kuwa destination ya tourism na business. Na wameachana na kuijenga Dubai kama mji wa kiarabu wameona hailipi, imekuwa kama Western city, huwezi tena kuamini uko nchi ya kiarabu. Wana invest in such a way hata mafuta yakikoma wanapeta tu bila tatizo. Wameangalia mbali na kuona mafuta mwisho wake unakuja.
 
anyway nilipata kumsikia mtu mmoja alisema bi-products za mafuta zinalipa zaidi kuliko mafuta yenyewe
Kwenye natural gesi mkuu ni kweli kabisa, kitu kinaitwa petrochemical industry. In fact Tanzania tuliambiwa gesi ya Songo Songo ni so pure (sweet gas) kiasi kwamba ni hasara kuichoma ili kuzalisha umeme, tulipaswa tuiingize kwenye petrochemical industry na tungefaidika zaidi. Nasikia kuna Mtanzania msomi mmoja alisimamia sana hilo akaondoshwa! Labda pia ku-invest mafuta kwenye plastic, lakini sasa vita dhidi ya plastics ni kubwa zaidi hata ya vita dhidi ya mafuta
 
hawa TPDC bonde la mandawa huko lindi bonde la ruvuma huko mtwara na bonde la tanga hawajamaliza kufanya utafiti ingawa viashiria vya uwepo wa mafuta vinaonekana wazi pamoja na sababu za kijiolojia zinazo sadifu uwepo wa mafuta.
They are saving the best for last, bila kujua kwamba hizo sehemu zitawavundia!
 
Nishati ya mafuta haiwezi kuwa obsolete hata kwa miaka mia mbili ijayo, bado yatatumika sana kwenye kuendesha mitambo mikubwa hata huko kwa wazungu, na kwa nchi za ulimwengu wa tatu itachukua miaka mingi zaidi kuacha kutegemea nishati ya mafuta....
Sawa, lakini tunachoongelea hapa ni economic feasibility ya sisi kuchimba mafuta wakati matumizi yake yakiwa yamepungua sana, kitu kitakachosababisha yashuke sana bei. Leo kuna watu bado wanatumia ndoo au makarai ya bati - lakini je, utataka leo tujenge kiwanda cha ndoo za bati?
 
Mkuu kama ni hivyo tumeshachelewa! Tuachane na miradi hiyo.













































































































































































alikuwa tayari kulitetea kwa nguvu zote.
Labda Ziwa Tanganyika.
Bado kidogo hatujachelewa kabisa, lakini lazima tukaze mwendo, angalau ndani ya miaka kumi ijayo tuhakikishe sehemu zenye uwezekano mkubwa wa mafuta tumezifanyia exploration ili kama yapo tutumie advantage kwamba bado mafuta yana soko zuri. Baada ya hapo it will be too late!
 
Ulaya hawatumii lami kama huku kwenu kimanzichana.

Angalia mfano wa barabara za mwendokasi hakuna lami pale.

Barabara za zege ndio habari ya zama hizi
Najua kuuliza sio ujinga, lakini unapaswa kuelewa lami ni zao mojawapo la kuchimba mafuta na kuyasafisha. Unafikiri lami inatokana na nini?

Pia ukiwa na uchumi mzuri wa mafuta ni rahisi kutengeneza barabara zote kuwa lami. Huhitaji degree kuelewa hilo.
 
Tatizo wenye makampuni ya kuchimba mafuta ndo HAO HAO.
Yaani marekani na ulaya.
Na ukumbuke marekani Wana HAZINA kubwa Sana ya mafuta .
SIO RAHISI KUKWEPA MATUMIZI YA MAFUTA WATAPATA HASARA KATIKA MAKAMPUNI YAO
You can't fight changes
 
Na wewe akili yako ni mgando. Najua kuna maelfu ya vitu vingine vinavyotumia mafuta, lakini elewa sababu kwa nini kuna msukumo wa kuacha kuchimba mafuta - yanasababisha climate change. Hata process ya hivyo vitu vingine bado itasababisha ongezeko la carbon ambalo ndio wanachotaka kuzuia.

Na pia, unapaswa kuelewa hivyo vitu vingine unavyosema vipo, vinachangia return za kiasi gani katika mafuta yanayochimbwa ili kuchimba mafuta kuendelee kuwa economically feasible? Ni sawa na kusema hata kama nazi zitaonekana zisiliwe tena kwa sababu ya tatizo fulani lililogundulika, watu waendelee kulima nazi kwa kuwa wanaweza kunywa madafu na kutumia makuti kuezeka nyumba na kutengeneza matenga. Hapo ndipo akili yako imeishia.

Rudi darasani kijana! Huku umerusha upupu mtupu! Nashukuru waelewa wa mambo wamekujibu!
 
Back
Top Bottom