Rais Samia kuwa mwenyeji wa mkutano wa marais wa nchi za SADC na EAC kujadili Mgogoro wa DR Congo

Rais Samia kuwa mwenyeji wa mkutano wa marais wa nchi za SADC na EAC kujadili Mgogoro wa DR Congo

bagamoyo

JF-Expert Member
Joined
Jan 14, 2010
Posts
24,941
Reaction score
28,869
03 February 2025
Dar es Salaam, Tanzania

Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kwa ukarimu kuandaa mkutano huo kujadili hali ya Mashariki mwa DRC

Dar es salaam kupokea marais wa nchi za sadc na eac kujadili mgogoro wa nchi ya dr congo

Mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) utafanyika Ijumaa na Jumamosi kuhusu mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Hii inafuatia makubaliano kati ya Mwenyekiti wa SADC Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa EAC Rais William Ruto wa Kenya.
"Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kwa ukarimu kuandaa mkutano huo kujadili hali ya Mashariki mwa DRC," Rais Ruto alisema.

MORE INFO :
Baada ya M23 Kunyakua pande la jimbo la Kivu ya Kaskazini uliopo mji wa Goma na kuonekana kuelekea Kivu ya Kusini mjini wa Bukavu.

Marais wa kanda za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wale wa nchi za Kusini SADC wamependekeza pande mbili katika mgogoro wa ndani wa DR Congo wa kujongea katika meza ya mazungumzo kutafuta utatuzi wa kudumu

Pia soma
- Waasi wa M23 sasa waelekea mji wa Bukavu

A joint summit of the Southern African Development Community (SADC) and the East African Community (EAC) will take place in Dar es Salaam, Tanzania

View: https://m.youtube.com/watch?v=ImbnMrR2NXs

03 February 2025

Les présidents congolais Félix Tshisekedi et rwandais Paul Kagame doivent participer ce week-end en Tanzanie à un sommet régional extraordinaire sur la guerre dans l'est de la RD Congo.
 
Uthibitisho wa wawili hao kukutana umetolewa na Rais William Ruto wa Kenya, Februari 3, 2025.
Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Paul Kagame wa Rwanda, wanatarajia kukutana jijini Dar es Salaam, Februari 8, 2025 kujadili mustakabali wa hali ya usalama katika eneo la Mashariki mwa DRC.

Taarifa iliyotolewa na Rais wa Kenya William Ruto, wawili hao watakutana katika mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania kuridhia nchi yake kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

Hatua hiyo inafuatia makubaliana kati ya mwenyekiti wa SADC Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na Rais William Ruto wa Kenya, ambaye pia ni mwenyekiti wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya EAC.
“Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo ambao unalenga kutafuta suluhu ya mgogoro wa Mashariki mwa DRC," alisema Rais Ruto.

Kulingana na Rais Ruto, wawili hao wamethibitisha uwepo wao kwenye mkutano huo wa pamoja ambao utatanguliwa na mkutano wa mawaziri siku ya Ijumaa, kabla ya Wakuu wa EAC na SADC hawajakutana siku ya Februari 8, 2025.
Rais Ruto pia amesemsa kuwa amewashirikisha jambo hilo Marais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Yoweri Museveni wa Uganda na Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia.
 
Wanaweza pigana kwenye meza ya mazungumzo hawa...

Cha msingi Tshisekedi usikubali ku-bow-down kwa huyu mlingoti wa ka jimbo kanakopakana na Kigoma..
 
Labda wamfate congo ilaa jamaa hawezi fanyaa kosa la rais wa burundii.
 
03 February 2025
Dar es Salaam, Tanzania

Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kwa ukarimu kuandaa mkutano huo kujadili hali ya Mashariki mwa DRC

DAR ES SALAAM KUPOKEA MARAIS WA NCHI ZA SADC NA EAC KUJADILI MGOGORO WA NCHI YA DR CONGO

Mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Maendeleo ya Kusini mwa Afrika (SADC) na Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) utafanyika Ijumaa na Jumamosi kuhusu mzozo wa Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo jijini Dar es Salaam, Tanzania.

Hii inafuatia makubaliano kati ya Mwenyekiti wa SADC Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na Mwenyekiti wa EAC Rais William Ruto wa Kenya.
"Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kwa ukarimu kuandaa mkutano huo kujadili hali ya Mashariki mwa DRC," Rais Ruto alisema.


MORE INFO :
Baada ya M23 Kunyakua pande la jimbo la Kivu ya Kaskazini uliopo mji wa Goma na kuonekana kuelekea Kivu ya Kusini mjini wa Bukavu.

Marais wa kanda za Jumuiya ya Afrika ya Mashariki na wale wa nchi za Kusini SADC wamependekeza pande mbili katika mgogoro wa ndani wa DR Congo wa kujongea katika meza ya mazungumzo kutafuta utatuzi wa kudumu


Tunarembesha rembesha maneno wakati wanajeshi wanakufa huko eti "kwa ukarimu" huu ni wakati wa vita
 
Uthibitisho wa wawili hao kukutana umetolewa na Rais William Ruto wa Kenya, Februari 3, 2025.
Rais Felix Tshisekedi wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na Paul Kagame wa Rwanda, wanatarajia kukutana jijini Dar es Salaam, Februari 8, 2025 kujadili mustakabali wa hali ya usalama katika eneo la Mashariki mwa DRC.

Taarifa iliyotolewa na Rais wa Kenya William Ruto, wawili hao watakutana katika mkutano wa pamoja wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) na Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), baada ya Rais Samia Suluhu Hassan wa Tanzania kuridhia nchi yake kuwa mwenyeji wa mkutano huo.

Hatua hiyo inafuatia makubaliana kati ya mwenyekiti wa SADC Rais Emmerson Mnangagwa wa Zimbabwe na Rais William Ruto wa Kenya, ambaye pia ni mwenyekiti wa Wakuu wa Nchi za Jumuiya ya EAC.
“Rais Samia Suluhu Hassan amekubali kuwa mwenyeji wa mkutano huo ambao unalenga kutafuta suluhu ya mgogoro wa Mashariki mwa DRC," alisema Rais Ruto.

Kulingana na Rais Ruto, wawili hao wamethibitisha uwepo wao kwenye mkutano huo wa pamoja ambao utatanguliwa na mkutano wa mawaziri siku ya Ijumaa, kabla ya Wakuu wa EAC na SADC hawajakutana siku ya Februari 8, 2025.
Rais Ruto pia amesemsa kuwa amewashirikisha jambo hilo Marais Cyril Ramaphosa wa Afrika Kusini, Yoweri Museveni wa Uganda na Hassan Sheikh Mohamud wa Somalia.
Tanzania tusingekubali kuhost mkutano huo ili kulinda hadhi na heshima ya Nchi Kimataifa.
Ni vipi kama baada ya mkutano ndege ya Kedi na Rama zikapotea mawasiliano kwenye Rada?. Au ndege ya Kagame?.Nakumbuka ndege ya rais wa Rwanda na Burundi; hata ile ya Samora zilikuwa zinatokea Dar kwenye Mkutano
 
Back
Top Bottom