Rais samia, Magereza wanaovutana kwenye miradi kushirikiana na sekta binafsi ni kutaka kulea upigaji

Rais samia, Magereza wanaovutana kwenye miradi kushirikiana na sekta binafsi ni kutaka kulea upigaji

kmbwembwe

JF-Expert Member
Joined
Aug 16, 2012
Posts
10,892
Reaction score
7,780
Rais samia hua anatoa kauli na maelekezo yenye utata. Lakini wenye kuelewa wanajua ni mwelekeo wake wa kupendelea sekta binafsi iliyojaa 'wahuni'
Inafaa atambue sekta binafsi kuleta ufanisi inatakiwa kua shindani sio kubebwa kwa kusudi kuingia ubia na majeshi au mashirika au mamlaka za umma ambapo makomanda na vigogo wanagombea ulaji na wala weledi hawana.

Anapaswa kutambua majeshi wakati wa amani lazima kufanya shughuli za uzalishaji mali.

Mtangulizi wake alitaka jeshi la magereza kutumia wafungwa kuzalisha mali na kwanza kabisa kujitegemea kwa chakula.

Kama Rais anazo taarifa za mifarakano kwenye miradi ya magereza kwa nini asitake kujua wakorofi au wakwamishaji akawatumbua. Nidhamu ya kijeshi na weledi ndio jambo muhimu kupata ufanisi.

Kutaka makomanda wa magereza wanaovutana kugombea ulaji kwenye miradi waingie ubia na sekta binafsi hapo ni kuanzisha ushirikiano wa makamanda wasio waadilifu wa magereza na 'wahuni' ambapo fedha ya umma italiwa na kutajirisha fisadi tu.

Rais samia ajue hawezi kufanikiwa kwa kutafuta sifa kwa mabwanyenye wabinafsi wenye nia siku zote kupiga hela ya umma kwa ushirika na serikali. Ushirika usiyokua na tija kwa umma wa wananchi.
 
Rais samia hua anatoa kauli na maelekezo yenye utata. Lakini wenye kuelewa wanajua ni mwelekeo wake wa kupendelea sekta binafsi iliyojaa 'wahuni'
Inafaa atambue sekta binafsi kuleta ufanisi inatakiwa kua shindani sio kubebwa kwa kusudi kuingia ubia na majeshi au mashirika au mamlaka za umma ambapo makomanda na vigogo wanagombea ulaji na wala weledi hawana.

Anapaswa kutambua majeshi wakati wa amani lazima kufanya shughuli za uzalishaji mali.

Mtangulizi wake alitaka jeshi la magereza kutumia wafungwa kuzalisha mali na kwanza kabisa kujitegemea kwa chakula.

Kama Rais anazo taarifa za mifarakano kwenye miradi ya magereza kwa nini asitake kujua wakorofi au wakwamishaji akawatumbua. Nidhamu ya kijeshi na weledi ndio jambo muhimu kupata ufanisi.

Kutaka makomanda wa magereza wanaovutana kugombea ulaji kwenye miradi waingie ubia na sekta binafsi hapo ni kuanzisha ushirikiano wa makamanda wasio waadilifu wa magereza na 'wahuni' ambapo fedha ya umma italiwa na kutajirisha fisadi tu.

Rais samia ajue hawezi kufanikiwa kwa kutafuta sifa kwa mabwanyenye wabinafsi wenye nia siku zote kupiga hela ya umma kwa ushirika na serikali. Ushirika usiyokua na tija kwa umma wa wananchi.
Una mawazo mgando.

New Public Management Vs Old Public Management
 
Mkuu haiwezekani pesa ya Serikali kuzunguka huko huko serikalini.
Sekta binafsi ndio chain nzuri ya mzunguko wa fedha kukuza Uchumi.
Tukijipanga vizuri kupitia Sekta binafsi Uchumi wa watu mitaani utaimalika sana.
Hongera Mh. Rais Samia Suluhu,hotuba yako ya leo imepokelewa kwa furaha kubwa na wadau wa Ujenzi.
 
Ukute watu wenye mawazo kama haya ndo wamejazana kwenye nafasi muhimu serikalini.
 
Kwa kauli yake ya leo nimekumbuka ile ya Manji kupewa tenda ya kutengeneza sare za jeshi, hata kama wanasema wanataka kuinua sekta binafsi lakini ukweli utabaki pale pale, hizo tenda watapewa wapigaji walewale na marafiki zao, hazina maana yoyote kwa mtu wa pembeni asie na connection ndio nawashangaa vipofu wanashangilia tu.
 
serikali haipaswi kifanya biashara majeshi yakatafute tenda nje ya serikali ,na watu binafsi washike tenda za serikali ndo mzunguko wa fedha unaoleta tija.zalisheni mkauze sio mnataka mtelemko
 
Kwa kauli yake ya leo nimekumbuka ile ya Manji kupewa tenda ya kutengeneza sare za jeshi, hata kama wanasema wanataka kuinua sekta binafsi lakini ukweli utabaki pale pale, hizo tenda watapewa wapigaji walewale na marafiki zao, hazina maana yoyote kwa mtu wa pembeni asie na connection ndio nawashangaa vipofu wanashangilia tu.
Asante kwa kunielewa. Kinachotakiwa ni sekta binafsi yenye kuleta thamani ya kiuchumi sio upigaji wa umma. Ubabaishaji na ukosefu wa weledi unaishia kwa kuhamisha fedha ya umma kwa 'wahuni' bila kuongeza thamani kwenye uchumi au umma kupata thamani kutoka fedha ya umma.
 
Back
Top Bottom