Rais Samia: Mashtaka dhidi ya Mbowe sidhani kama yamechochewa kisiasa. Natamani kukutana na Wapinzani

Sijaelewa kusita kwa Mama kuagiza kufutwa kwa sintofahamu hii kwa taifa. Miaka 60 ya Uhuru taifa linaendesha Shauri la kizandiki linalopaka matope taifa na kuharibu umoja wa taifa kwa makusudi!?!? Ujinga huu walifanya Makaburu SA Zama zile.
 
Kwa mujibu wa jarida la Sauti Kubwa wanaomlisha matango pori rais na wahandisi wa kesi hii ni Zerro na bamkwe Waziri Mchengerwa.
 
Sheria [katiba] inamlinda kushitakiwa yeye binafsi kwa makosa ya jinai anapokuwa na hata atakapokuwa ametoka madarakani...
Mawakaili wa utetezi imewapasa kulikumbuka hili , Kama wataleta utani imewapasa kujua kesi hii imehukumiwa na Raisi kabla ya kusikilizwa, kwa hyo Hawa majaji hawataenda kinyume na maoni ya kiongozi wao!

Namna pekee ya kuwanasua ni kumwita huyu aliyeuthibitishia ulimwengu kuwa Mbowe Ni Gaidi na wanao ushahidi wa kutosha na kwamba umekamilika ( ingawa Kingai Leo kasema upelelezi haujakamika) ili aje atuambie yeye hizo habar alizitoa wapi? Na alizungumza Kama nani (kisheria), mbona kinachoendelea kinapingana na maneno yake? Alimaanisha Nini kuhukumu shauri ambalo muhukumu ni jaji? Kuna agenda gani iliyojificha?
 
Yule hana jipya zaidi ya kutafuta huruma ya maumbile yake,yani yupo kwende kundi la mazuzu
Aje hivyo hivyo, maana huyo anaijua kesi hii kuliko majaji ndo maana alijichukulia mammlaka ya kuhukumu, kwa huyo ni shahidi wa muhimu Sana katika kesi hii Wala wasilete mwakilishi!
 
Sijaelewa kusita kwa Mama kuagiza kufutwa kwa sintofahamu hii kwa taifa. Miaka 60 ya Uhuru taifa linaendesha Shauri la kizandiki linalopaka matope taifa na kuharibu umoja wa taifa kwa makusudi!?!? Ujinga huu walifanya Makaburu SA Zama zile.
Kwani unaona Kuna utofauti Kati ya matendo yaliyofanywa na Makaburu dhidi ya wapigania haki wa SA, na matendo yanayoendelea hivi Sasa ya CCM dhidi ya wapinzani?

CCM =Makaburu
 
Kwa mujibu wa jarida la Sauti Kubwa wanaomlisha matango pori rais na wahandisi wa kesi hii ni Zerro na bamkwe Waziri Mchengerwa.
Zero naye wanamkawiza, zamu yake ingefika mapema, aje athibitishe!
 
Labda katiba mpya ipatikane ndo anaweza kusimama mahakamani....ila saivi vyoooote anamiliki yeye Chief hangaya
Ikumbukwe Katiba mpya ndiyo hiyo iko Mahakamani, Sasa Sijui hiyo katiba mpya unayoipendekeza kwa Nia njema itapatikanaje??
 
Si ni CHIEF HANGAYA
Ndiyo maana huyu ni mtu muhimu Sana katika kesi hii, nitawashangaa upande wa utetezi Kama watamkalia kimya!

Wamwite ili anisaidie mahakama, ili pia iwe fundisho kwa viongozi wengineo kuwa si Jambo la busara kuingilia kazi inayosimamiwa na muhimili mwingine!!
 
Hii kesi ya Mh Mbowe ina mambo mengi ya kufikirisha sana
 
Haitatokea kwa katiba iliyopo, we jua hata akiamua aue maelfu akiwasomba na kuwamwaga baharini hatoshtakiwa!
 
Haitatokea kwa katiba iliyopo, we jua hata akiamua aue maelfu akiwasomba na kuwamwaga baharini hatoshtakiwa!
Unasema kweli Rais wa Tanzania anaweza kukiuka kiapo chake kiasi hicho asishtakiwe atakuwa kamzidi madaraka Mungu!!
 
Hii ni zaidi ya kuropoka. Uhuru gani anaoujua. Bora aende asome Azimio la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu linalompa raia hata haki ya kuandamana, lichaya kukusanyika na kutoa maoni yao bila kuzuiwa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…