Rais Samia, mfute kazi Waziri wa Maliasili na Utalii, mzungu naye akamatwe na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi

Hawana kibali? Mamba mzee anafaida gani? Uskute naye ashakula watu kibao!! Hii ndonchi mnyama akiua poa ila akiuwawa sipoa😳
 
Kuna watu ni mambumbu. Hawapendi kujielimisha na kujua taratibu za mambo mbalimbali.
Kwa nini tunahifadhi?
1. Kulinda wanyama na mimea visitoweke.
2. Kuingiza fedha za kigeni kwa njia ya utalii.
Kuna aina mbili kubwa za utalii wa wanyama.
1. Utalii wa kuangalia na kupiga picha.
2. Utalii wa uwindaji. Huu ufanyika katika maeneo maalumu yaliyotengwa.
 
... sema mama mjane maskini alambwa miaka 20 jela kwa kukutwa na ndoo yenye vipande vya mzoga wa swala huko Iringa.

Mzungu tajiri milionea apongezwa duniani kote kwa kuua mamba mkubwa zaidi duniani kutoka Tanzania. Umaskini kitu kibaya sana!
 
Mkuu; Kama amezingatia Taratibu zote za uvunaji wa Mali asili sioni shida hapo.
Naomba nikuulize kidogo: Hivi, kati ya huyo anayekuwa muwazi na pengine amefuata Taratibu zilizopo na amelipa inavyostahili na wale wanaojibebea mnyama mzima au Mali asili nyinginezo kiujanja-ujanja ni yupi bora?
Kwamba aliye muua anaenda kumfanyia nini, nadhani hilo lisikuumize kichwa anajua mwenyewe.
 
... sema mama mjane maskini alambwa miaka 20 jela kwa kukutwa na ndoo yenye vipande vya mzoga wa swala huko Iringa.

Mzungu tajiri milionea apongezwa duniani kote kwa kuua mamba mkubwa zaidi duniani kutoka Tanzania. Umaskini kitu kibaya sana!
Usikutwe na nyama ya Nyati bila vibari, nishakula sana Nyati hapa karibu kuna butcher ya nyama Pori
 
Kuna utalii wa uwindaji, hujaonesha kuwa kakiuka masharti yoyote.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…