Rais Samia, mfute kazi Waziri wa Maliasili na Utalii, mzungu naye akamatwe na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi

Rais Samia, mfute kazi Waziri wa Maliasili na Utalii, mzungu naye akamatwe na kushtakiwa kwa uhujumu uchumi

Kuna watu ni mambumbu. Hawapendi kujielimisha na kujua taratibu za mambo mbalimbali.
Kwa nini tunahifadhi?
1. Kulinda wanyama na mimea visitoweke.
2. Kuingiza fedha za kigeni kwa njia ya utalii.
Kuna aina mbili kubwa za utalii wa wanyama.
1. Utalii wa kuangalia na kupiga picha.
2. Utalii wa uwindaji. Huu ufanyika katika maeneo maalumu yaliyotengwa.
 
... sema mama mjane maskini alambwa miaka 20 jela kwa kukutwa na ndoo yenye vipande vya mzoga wa swala huko Iringa.

Mzungu tajiri milionea apongezwa duniani kote kwa kuua mamba mkubwa zaidi duniani kutoka Tanzania. Umaskini kitu kibaya sana!
 
Kwa akili yako ya kawaida,kumuua mamba kama huyo kwenye hifadhi ni sawa?!! Unaweza kukadiria imechukua miaka mingapi mpaka akawa na ukubwa huo?!!

Kama angebaki na akajengewa eneo maalumu kwa ajili ya watu kwenda kumuona ingekua ni hasara kwa Taifa ama faida zaidi?!! Baada ya huyo kuuliwa,kuna wengine wenye ukubwa huo?!! Kama wapo,nao hawatauliwa?!! Aliemuua anaenda mfanyia nini?!!!! Hicho anachoenda kukifanyia- Taifa linanufaikaje?!!

Tuache kutetea upuuzi na uharibifu wa Mali asili
Mkuu; Kama amezingatia Taratibu zote za uvunaji wa Mali asili sioni shida hapo.
Naomba nikuulize kidogo: Hivi, kati ya huyo anayekuwa muwazi na pengine amefuata Taratibu zilizopo na amelipa inavyostahili na wale wanaojibebea mnyama mzima au Mali asili nyinginezo kiujanja-ujanja ni yupi bora?
Kwamba aliye muua anaenda kumfanyia nini, nadhani hilo lisikuumize kichwa anajua mwenyewe.
 
... sema mama mjane maskini alambwa miaka 20 jela kwa kukutwa na ndoo yenye vipande vya mzoga wa swala huko Iringa.

Mzungu tajiri milionea apongezwa duniani kote kwa kuua mamba mkubwa zaidi duniani kutoka Tanzania. Umaskini kitu kibaya sana!
Usikutwe na nyama ya Nyati bila vibari, nishakula sana Nyati hapa karibu kuna butcher ya nyama Pori
 
Mzungu huyu ameonekana akiwa na maafisa wa wanyama pori akifurahia kumuua mamba mkubwa mwenye urefu zaidi ya mita 4 ndani ya hifadhi moja wapo ya Taifa.

Huu ni uhujumu wa makusudi ambae umefadhiliwa na vyombo vya dola (maafisa wa hifadhi kwani kazi ya kumuwinda mamba mkubwa kama huyo na hatimae kumuua na kuanza kumburuta na kumfunga abebwe sio jambo la siri na clips zimeenea mitandaoni na dunia nzima.

Mzungu husika akamatwe kama ndugu zetu na jamaa wanavuokamatwa hata kwa kukutwa na vipande vya nyama tu ya kitoweo cha familia.

Waziri husika nae aachie ngazi, ikiwa watu wanafikia hadi kufanya ujangiri wa kuhujumu uchumi huku wanalindwa na vyombo vya dola na wakijitajgaza wazi wazi, je vungapi hatuoni ambavyo ni zaidi ya hivi?



===

Raia mmoja wa Kizungu anayejiita Bowmarbow hunting ameonekana mitandaoni akitrend kwa kujisifu kuua Mamba mkubwa zaidi kutoka Tanzania.

Kupitia Instagram yake ameandika kuwa ameingia kwenye rekodi ya kuua Mamba mkubwa zaidi.

Ameandika haya;

“PENDING NEW WORLD RECORD CROC with a bow. This monstrous crocodile measured in at an astounding 16’ 3”! Making him the largest croc in history to ever be harvest with a bow and arrow. The best part is, he’s a 100% wild & 100% free ranging croc in the wilds of Tanzania, which is not how most of the WRs are shot in Africa.

This hunt was beyond incredible to say the least, I can’t wait to share it with you all! The footage we captured was some of our best and this is by far the biggest animal ever shot with a beast_broadheads at 25 yards with an 84lb bow and only a 530 gr arrow it buried through his armor and went all the way up to the fletching.

Just a crazy testament to the lethality of the head.

PSA: As for the Broadheads, next week we’ll be opening them back up for you everyone again A thank you all for your patience with being sold out”

Je, ni sahihi kwa Wanyama kama hawa kuuawa kiholela kwa ajili ya kuweka Rekodi?

Bongo 5
Kuna utalii wa uwindaji, hujaonesha kuwa kakiuka masharti yoyote.
 
Back
Top Bottom