Rais Samia: Mgao wa maji unatokana na ubishi na ukaidi wa binadamu pia na kudra za mwenyezi Mungu

Rais Samia: Mgao wa maji unatokana na ubishi na ukaidi wa binadamu pia na kudra za mwenyezi Mungu

Janga gani na wewe? Yaani huoni haya mabadiliko ya tabia ya nchi? Joto kali sana na maeneo mengine kama Morogoro mvua haijanyesha kabisa, na hii ni November inaenda mwishoni. Yeye afanyeje kama maji yamepungua kutokana na sababu hizo? Kazi tu kukariri corus bila ya kufanya tafakari.
😍
 
Ng'ombe mmoja anakunywa lita 40 kwa siku [emoji1787][emoji1787] ama kweli mama kafungua nchi wallah!!
Kwenye kipindi cha kiangazi ng'ombe anaweza kunywa mpaka lita 80 kwa siku...
 
Dar es Salaam kuna mgao mkubwa wa maji kwa sababu mto Ruvu umevamiwa na binadamu na kuchepusha maji.

Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku..
Jamani watu ni hatari, kwa maana kwa kipindi cha miezi nane ni kama walishauriana kumuangusha Mama na kuvamia mitoni na kupunguza maji. Si hao pia wavugaji sijui waliwahamisha ngombe toka Mwanza na Shinyanga ili kuvamia maji kwa kipindi hiki cha miezi 8.

Na hawa wakataji miti sijui nao walifuatana na wachunga ng`ombe toka Mwanza na Shinyanga na kufanya hujuma kwa miezi hii 8. Du, ni ajabuuuuuuu!!!!!!!!!! Kwa hilo mmefanikiwa kusumbua akili ya Mama, yaani inaitwa MGOMO NA HUJUMA BILA MATANGAZO.
 
Naagiza Wakuu wote wa mikoa kuweka ulinzi katika mito yote ili kulinda maji ya watu wetu……… waagize wakasimamie upandaji wa miti kwenye vyanzo vya maji badala ya kwenda kulinda mito tu.
Utekelezaji wa maagizo ndicho kinacho takiwa kuzingatiwa .
 
Dar es Salaam kuna mgao mkubwa wa maji kwa sababu mto Ruvu umevamiwa na binadamu na kuchepusha maji.

Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku...
Mama tumewahi kuwa na.ukame na.mifugo ilikuwepo, Hakuna hata wakati mmoja wanyama walimaliza maji. Mifugo inategemea mipango ya wanadamu kuhusu uwepo wao,sasa tumefikia hatua ya kuilaumu mifugo? Basi tumekwama kama Taifa. Ni wapi mliutengea maji yao na sasa wanayaacha na kuja kunywa ya wanadamu?

Katika hili sikuuungi mkono. Lakini pia lazima ujue kama wewe ulivyo na hiyi ajira unalipwa mshahara unasomesha wanao ,na mfugaji naye ajira yake ni mifugo ,analisha watu wake,anawasimesha. Anajitibu ,anawabisha kutokana na mifugo. Tangu kuimbwa kwa ulimwengu mifugo ipo.

Ama ukataji wa miti serikali inapaswa kulaumiwa badala ya mwananchi anayekata miti kwa ajili ya mkaa au kuni au ujenzi. Serikali imeshindwa kusambaza gas ya bei nafuu kwa wananchi iliiwe mbadala wa nishati ya kuni. Mmeshindwa kabisa ,badala yake gas ni ghali sana wakati inazalishwa hapa nyumbani.

Vifaa vya ujenzi vingeondokewa kodi ,iwe ni mpango maalumu kwa kipindi cha miaka kumi. Ili watu wamudu gharama za ujenzi hasa vijijini ili kuepuka ukataji wa miti kama vifaa vya ujenzi.
 
🤡🤡🤡
_jt0.jpg
 
Dar es Salaam kuna mgao mkubwa wa maji kwa sababu mto Ruvu umevamiwa na binadamu na kuchepusha maji.

Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku.

Tatu ni ukataji miti hovyo hali inayoharibu ikolojia ya nchi.

Nne ni tatizo la tabia nchi.

Hivyo mgao wa maji hauepukiki

Na kwahiyo naagiza Wakuu wote wa mikoa kuweka ulinzi katika mito yote ili kulinda maji ya watu wetu.

========

Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua Miji mingi mikubwa inakabiliwa na uhaba wa maji unaopelekea mgao wa maji na upungufu wa umeme

Amesema hiyo imetokana na mambo mawili makubwa ambayo ni Ubishi na ukaidi wa wanadamu na Kudra za Mungu

Amefafanua, "Bado kuna wananchi wengi wameendelea kuvamia vyanzo vya maji kwa kuyachepusha kwa ajili ya matumizi mengine. Pia, kuna watu wanalima karibu na vyanzo vya maji. Haya yote yanapelekea Vyanzo vya Maji kupungua"

"Nimefatana na viongozi wote hawa wa dini kwanza, kufuatana na viongozi wa dini wote hawa ni baraka kama kuna mapepo huko njiani yanapeperuka, pili nimeipa heshima Mwanza, tutaanza hapa dua za kuomba mvua zenye neema kwa Taifa letu"-Rais Samia.
Dar es Salaam kuna mgao mkubwa wa maji kwa sababu mto Ruvu umevamiwa na binadamu na kuchepusha maji.

Pili maelfu ya mifugo yanayoingizwa kwenye mito kunywa maji yamepunguza kiasi cha maji kwani ng'ombe mmoja kwa mfano hunywa lita 40 za maji kwa siku.

Tatu ni ukataji miti hovyo hali inayoharibu ikolojia ya nchi.

Nne ni tatizo la tabia nchi.

Hivyo mgao wa maji hauepukiki

Na kwahiyo naagiza Wakuu wote wa mikoa kuweka ulinzi katika mito yote ili kulinda maji ya watu wetu.

========

Rais Samia Suluhu Hassan amesema anatambua Miji mingi mikubwa inakabiliwa na uhaba wa maji unaopelekea mgao wa maji na upungufu wa umeme

Amesema hiyo imetokana na mambo mawili makubwa ambayo ni Ubishi na ukaidi wa wanadamu na Kudra za Mungu

Amefafanua, "Bado kuna wananchi wengi wameendelea kuvamia vyanzo vya maji kwa kuyachepusha kwa ajili ya matumizi mengine. Pia, kuna watu wanalima karibu na vyanzo vya maji. Haya yote yanapelekea Vyanzo vya Maji kupungua"

"Nimefatana na viongozi wote hawa wa dini kwanza, kufuatana na viongozi wa dini wote hawa ni baraka kama kuna mapepo huko njiani yanapeperuka, pili nimeipa heshima Mwanza, tutaanza hapa dua za kuomba mvua zenye neema kwa Taifa letu"-Rais Samia.

Hii ni ishara nzuri kwa kiongozi wa nchi kuwa mstari wa mbele kuliombea taifa. Ni vyema kuwa na maombi ya kitaifa ya kufunga na kuomba ili kuomba Rehema za Mungu dhidi la hili janga la ukosefu wa mvua na majanga mengine yanayotukabili kama taifa.
Mungu Ibariki Tanzania.
Amen
 
Kabla ya kuomba mvua Hangaya tubu dhambi ya kutotambua Mungu aliiponya Tanzania janga la Corona, unalazimisha kwamba Corona ni tishio mpaka Sasa, unalazimisha watu wavae barakoa,watu wachanjwe misumu,ili uwafurahishe wazungu.
Usipotubu Mungu atakufedhehesha kila Kona.
 
Hii ni ishara nzuri kwa kiongozi wa nchi kuwa mstari wa mbele kuliombea taifa. Ni vyema kuwa na maombi ya kitaifa ya kufunga na kuomba ili kuomba Rehema za Mungu dhidi la hili janga la ukosefu wa mvua na majanga mengine yanayotukabili kama taifa.
Mungu Ibariki Tanzania.
Amen
Hayo maombi mbona aliyakataa kwenye corona? Akataka sayansi
Kwa nini kwenye maji na umeme hataki sayansi?
 
Hivi solution ya haya mama aliyoelezea leo ni nini? Kwa sasa vyanzo vingi vya maji, sehemu mbalimbali nchini vimevamiwa na wakulima na wafugaji (nenda Morogoro na Nyanda za Juu kusini, n.k), watu wanalima hadi mabonde ya mito, miti inakatwa hovyo kuchoma mkaa na kupata maeneo ya kilimo, n.k.Kama nchi nachelea kusema tumekalia maneno bila vitendo huku tukijua wazi hatari iliyopo mbele yetu.

China kwa mfano, kupitia Shelterbelt Program ina mpango wa kuondoa jangwa kwa ekari milioni 87 ifikapo 2050 na hadi sasa wameshapanda miti kwa zaidi ya ekari 13 milioni.

Ni imani yangu tunaweza kuibadilisha sehemu kubwa ya nchi yetu ikawa ya kijani ndani ya miaka 10 ikiwa watu watahamasishwa na kuwa na mipango madhubuti. Ili hili litokee kuna haja ya:

1. Kila halmashauri, kata na kijiji kupewa lengo l miti ya kupanda kila mwaka na ukaguzi wa dhati wa kilichofanyika uwepo.

2. Shule zote zipewe lengo la idadi ya miti kupanda na kuikuza kila mwaka.

3. Kambi zote za jeshi zipewe pia malengo.

4. Maeneo yote public ikiwa ni pamoja na mbuga zipewe JKT na mashule kupanda miti.

5. Kila mtanzania mwenye eneo la shamba apewe idadi ya miti kupanda (mfano miti kumi kuzunguka shamba kwa kila ekari moja).

Nawasilisha.
Hiyo ndiyo tofauti ya Uongozi wa magufuli na wapuumbavuu
Magufuli ni MAJIBU
Ila uongozi tulionao ni MASWALI
 
Aisee wewe jamaa wa ajabu sana. Kwa hiyo ulitegemea Mama Samia awe amefikisha maji ya ziwa victoria Dar na maeneo mengine ndani ya kipindi kifupi alichoshika madaraka? Mbona walaumu bila kuwa na sababu za msingi?

Au ni chuki zako tu kwake? Au hujui pia mabadiliko ya tabia ya nchi yaweza kusababisha hata kina cha maji ya ziwa kupungua sana na kuicha mitambo ya kutape maji ikielea tu?
mkuu hivi unauelewa vizuri kichwani
 
Gesi asilia toka igunduliwe miaka ya sabini haijawahi kuwekwa kwenye mtungi,gesi inayotumika inatoka nje. Labda tuwaulize hao serikali kwanini imeshindikana au tuna ombwe la uongozi?
Kuna mradi wa kumwezesha magari madogo kutumia gesi badala ya petroli lakini mwaka wa kumi na ushee huu kituo Cha kuuzia gesi Ni kimoja TUUH na magari yaliyofungwa hayafiki mia
 
KINACHOENDELEA KTK TAIFA LETU HASA KWENYE ISSUE YA UMEME TUNA ANDALIWA TARATIBU,KIJANJAJANJA KUAMINISHWA UPUUZI KWAMBA MAJI HAYATOSHI,MARA MIUNDOMBINU CHAKAVU.WATANZANIA TUNAPASWA KUELEWA KWAMBA WALE WALIOKUWA WANAFANYA JUHUDI ILI TAIFA KUBWA KAMA HILI LISIJITEGEMEE KWA NISHATI YAKE YA UMEME NDIO WAMEPEWA KITENGO HICHO,TUKUMBUKE MCHWA WAMEVAMIA NYUMBA.TUANDAE MAJENERETA YAKUTOSHA MAANA NDIO LENGO KUU LILILOPO MEZANI.
 
TAIFA linaendelea kupendeza na bidhaa nyingi zinaendelea kushuka bei mfano mbolea bei ilikuwa Tshs 65000/=zamani sasa imeshuka mpaka 130,000/=,Bati tulinunua Tshs 350,000/=,sasa bei imeshuka hadi Tshs 420,000/= na bado watanzania eti wanataka mbolea ishuke hadi Tshs 300,000/=na Bati lishuke hadi Tshs 600,000/= kwa bandro 1 sijui tunataka serikali itutendee nini ndio tuelewe kwa inatupenda kuliko kawaida.
 
Janga gani na wewe? Yaani huoni haya mabadiliko ya tabia ya nchi? Joto kali sana na maeneo mengine kama Morogoro mvua haijanyesha kabisa, na hii ni November inaenda mwishoni. Yeye afanyeje kama maji yamepungua kutokana na sababu hizo? Kazi tu kukariri corus bila ya kufanya tafakari.
inamana kwani hata ziwa viktoria kina cha maji kimepungua kiasi cha wakazi wa maeneo lengwa kukosa maji?
 
Back
Top Bottom