Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 28,722
- 20,610
Ndugu zangu Watanzania,
Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan, Anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika kongamano la kwanza la kiswahili kimataifa litakalofanyika Havana Nchini Cuba kuanzia Tarehe 7 November hadi 10 November.
Ambapo kongamano hilo litawakutanisha washirika zaidi ya mia 6 yaani 600 kutoka maeneo mbalimbali.lakini pia katika kongamano hilo litahudhuriwa pia na Rais wa Nchi hiyo ya Cuba.
Ikumbukwe ya kuwa kiswahili kimefanikiwa kutambulika au kutambuliwa na UNESCO kuwa Lugha ya saba ya kimataifa,ikiwa na wazungumzaji zaidi ya Millioni 500 Duniani kwote.hivyo hatua hii ni katika muendelezo wa kukipeleka na kukitambulisha kiswahili katika anga la kimataifa.
Siku hiyo na siku hizo za kongamano kutafanyika pia semina mbalimbali pamoja na uzinduzi wa kamusi ya kiswahili na kispaniola iliyoandaliwa na chuo kikuu cha Dar es salaam.
Mimi Mwashambwa Lucas Napongeza sana hatua hii ya Mheshimiwa Rais na juhudi zake za kukipeleka kiswahili kimataifa.lakini Rai yangu ni kuomba sisi kama Taifa kuwa mstari wa mbele katika kukitumia katika maeneo mbalimbali ya kiutawala na maamuzi.
Mfano bado haijafahamika vizuri kwanini mpaka leo unakuta kesi mahakamani inasikilizwa kwa kiswahili halafu hukumu na mwendo mzima wa kesi unatolewa kwa lugha ya kiingereza.jambo ambalo linawanyima haki watu wasio na uelewa na lugha hiyo ya kiingereza hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa hata tu waliosoma na kufika vyuo vikuu unakuta umahiri katika lugha hii ya kigeni ni tia maji tia maji tu.
maana wengi wamekariri na walikariri kwa ajili ya kujibia mitihani ya darasani tu.ambapo unakuta mtu amemaliza chuo kikuu lakini hawezi kuongea hata kwa dakika mbili kiingereza kilichonyooka kama rula bila kusoma mahali popote pale.
Sasa kwanini tuendelee kuwatesa watanzania na kuwapa kazi ya kutafuta wakalimani wa lugha ya kiingereza kuwafafanulia kilichoandikwa na jaji.kwanini hukumu na mwenendo mzima wa kesi usiandikwe kwa kiswahili tu ieleweke.
Pili huwa nashangaa unakuta viongozi wetu wengine yupo kwenye hadhira ya huko vijijini lakini unakuta anachanganya na kutoa ufafanuzi kwa kuchanganya kiswahili na maneno ya kiingereza.sasa lengo Sijuwi huwa ni nini.maana jambo hilo huwaacha wananchi hewani kwa kushindwa kuelewa baadhi ya hoja.
Pia sisi kama Taifa tunatakiwa ndio viongozi wetu wawe mstari wa mbele katika kutumia lugha hii ya kiswahili katika hotuba zao hususani kunapokuwa na wageni wameingia Nchini mwetu.cha kufanya ni kutafuta wakalimani wa kufanya kazi hiyo ya kufasili. Ofisi zote za umma na matangazo yao nayo pia yawe yanatolewa kwa kiswahili.
Tuache kukitukuza sana kiingereza.maana imefika wakati inaonekana mtu anayezungumza kiingereza ana akili sana na msomi sana kuliko yule anayezungumza kiswahili.ndio maana ukizungumza kwa kiingereza jambo hata la kijinga utaonekana una akili nyingi na utaona watu wakikushangilia na kukusifia sana kwa kuwa tu umeongea kiingereza.
Naomba niishie hapa kwanza maana najuwa wengi hawapendi maandiko marefu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Rais wetu Mpendwa na Jemedari wetu kipenzi Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan, Anatarajiwa kuwa mgeni Rasmi katika kongamano la kwanza la kiswahili kimataifa litakalofanyika Havana Nchini Cuba kuanzia Tarehe 7 November hadi 10 November.
Ambapo kongamano hilo litawakutanisha washirika zaidi ya mia 6 yaani 600 kutoka maeneo mbalimbali.lakini pia katika kongamano hilo litahudhuriwa pia na Rais wa Nchi hiyo ya Cuba.
Ikumbukwe ya kuwa kiswahili kimefanikiwa kutambulika au kutambuliwa na UNESCO kuwa Lugha ya saba ya kimataifa,ikiwa na wazungumzaji zaidi ya Millioni 500 Duniani kwote.hivyo hatua hii ni katika muendelezo wa kukipeleka na kukitambulisha kiswahili katika anga la kimataifa.
Siku hiyo na siku hizo za kongamano kutafanyika pia semina mbalimbali pamoja na uzinduzi wa kamusi ya kiswahili na kispaniola iliyoandaliwa na chuo kikuu cha Dar es salaam.
Mimi Mwashambwa Lucas Napongeza sana hatua hii ya Mheshimiwa Rais na juhudi zake za kukipeleka kiswahili kimataifa.lakini Rai yangu ni kuomba sisi kama Taifa kuwa mstari wa mbele katika kukitumia katika maeneo mbalimbali ya kiutawala na maamuzi.
Mfano bado haijafahamika vizuri kwanini mpaka leo unakuta kesi mahakamani inasikilizwa kwa kiswahili halafu hukumu na mwendo mzima wa kesi unatolewa kwa lugha ya kiingereza.jambo ambalo linawanyima haki watu wasio na uelewa na lugha hiyo ya kiingereza hasa kwa kuzingatia ukweli kuwa hata tu waliosoma na kufika vyuo vikuu unakuta umahiri katika lugha hii ya kigeni ni tia maji tia maji tu.
maana wengi wamekariri na walikariri kwa ajili ya kujibia mitihani ya darasani tu.ambapo unakuta mtu amemaliza chuo kikuu lakini hawezi kuongea hata kwa dakika mbili kiingereza kilichonyooka kama rula bila kusoma mahali popote pale.
Sasa kwanini tuendelee kuwatesa watanzania na kuwapa kazi ya kutafuta wakalimani wa lugha ya kiingereza kuwafafanulia kilichoandikwa na jaji.kwanini hukumu na mwenendo mzima wa kesi usiandikwe kwa kiswahili tu ieleweke.
Pili huwa nashangaa unakuta viongozi wetu wengine yupo kwenye hadhira ya huko vijijini lakini unakuta anachanganya na kutoa ufafanuzi kwa kuchanganya kiswahili na maneno ya kiingereza.sasa lengo Sijuwi huwa ni nini.maana jambo hilo huwaacha wananchi hewani kwa kushindwa kuelewa baadhi ya hoja.
Pia sisi kama Taifa tunatakiwa ndio viongozi wetu wawe mstari wa mbele katika kutumia lugha hii ya kiswahili katika hotuba zao hususani kunapokuwa na wageni wameingia Nchini mwetu.cha kufanya ni kutafuta wakalimani wa kufanya kazi hiyo ya kufasili. Ofisi zote za umma na matangazo yao nayo pia yawe yanatolewa kwa kiswahili.
Tuache kukitukuza sana kiingereza.maana imefika wakati inaonekana mtu anayezungumza kiingereza ana akili sana na msomi sana kuliko yule anayezungumza kiswahili.ndio maana ukizungumza kwa kiingereza jambo hata la kijinga utaonekana una akili nyingi na utaona watu wakikushangilia na kukusifia sana kwa kuwa tu umeongea kiingereza.
Naomba niishie hapa kwanza maana najuwa wengi hawapendi maandiko marefu.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.