Rais Samia muulize Bilionea Alhaj Aliko Dangote alitaka umpe nini ambacho hajapewa?

Rais Samia muulize Bilionea Alhaj Aliko Dangote alitaka umpe nini ambacho hajapewa?

Simfahamu

Ila nimefata hoja sio mtoa hoja
Hakuna mchumia tumbo mwenye hoja , Magufuli alimwalika Dangote , akamwalika Rostam hadi mdogo wake jangili wa meno ya tembo akafutiwa kesi ya ujangili , na ccm ikahongwa Channel 10 , uliona Huyu njaa kali Maghembe akiandika huu utopolo wake ? unadhani ni kwanini ?
 
Hivi kwann kila siku Dangote ni yeye tu Ikulu kwa kila Rais anayeingia?
Je hata viwanda vingine vya cement wako hivyo?

Mi napata mashaka na Huyu bilionea wa Africa,huenda utajiri wake umegubikwa na favor nyingi ambazo kuna watu chini kwa chini wananufaika nate.
Daily Ikulu??????
dangote ameenda siku moja unadai kila siku?
check your facts kwanza
 
Barua ya mualiko ulitoa wewe?
Acha kujifanya unajua kumbe pangu pakavu,sisi ndo wafanya biashara tunaelewa haya,wewe mkusanya documents ofisini subiri mshahara mwisho wa mwezi
Nyinyi ni wafanya biashara, au wanyang'anyi wa mali za waTanzania?

Kama wewe ni mfanya biashara huwezi kuogopa kufanya mambo yako kwenye uwazi na taratibu zinazofahamika.

Haya, tueleze wewe 'mnyang'anyi' unayejipambanua kuwa mfanya biashara, hiyo mialiko mnayopewa kwenda huko, inatofauti gani na taratibu za kibishara mnayoitumia sasa, maanake sisi hatuijui, au ni siri yenu nyinyi pekee na huyo anayewapa hiyo mialiko?

Tukilisemea hilo unatoana ni wajinga na kutuona "wakusanya 'documents' ofisini"?
 
Wazo sio kubwa kuliko dangote..
kwa sasa Dangote ndio kiwanda kikubwa interms of production tonnage per day..

Dangote aliomba auziwe gas kwa bei ya Mtwara sio ya Dar es salaam..., gas pipeline limepita upande wa pili wa kiwanda ukivuka barabara...mweye jukumu la kusupply ni TPDC, Dangote yeye amejenga gas plant kwa gharama zake...

Ugomvi wa Dangote ni kugeukwa na awamu ya tano nje ya makubaliano ya awamu ya nne....complain yake ni yeye kuja kuwekeza based taratibu na makubaliano yake na awamu ya nne....awamu ya tano ghafla bin vuu inabadili taratibu na kuleta taratibu mpya na hawataki mazungumzo....wewe ungefanyaje?...

Dangote ananunua gas, Dangote ananunua maji, Dangote ametoa ajira kwa watu zaidi ya 2000, PAYE za watu zaidi ya 2000, NSSF zaidi ya watu 2000...Dangote anasupplier wakibongo wanaolipa kodi....unajua faida ya watu 2000 wakiwa na ajira kwenye mji?... Dangote ameleta cement sokoni kwa 10K cheaper than all...road toll ya magari zaidi ya 500....nk nk nk..

La msingi ni Serikali kumshinikiza Dangote alipe vizuri watu wetu, Aajiri wazawa wengi na kuwapa training, Dangote amentain price ya cement 10k au kushuka chini...nk nk
Mkuu hebu weka wazi jinsi awamu ya tano ilivyo kiuka makubaliano baini ya serikali na Dangote.tunaome uyaweke wazi tuache hisia...
Swala la kuletewa gas kiwandani kwake lilifanywa awamu gani na nani aliagiza?
swala la kupewa mgodi wa kuchimba coal lilifanywa awamu gani? nani aliaGIZA?
Alipo kuwa anaingiza magari yake nakumbuka serikali iliingilia kati nakuamuru yatolewe pale bandarini mtwara haraka... hivi hii ilikuwa awamu gani?
Hebu twambieni Magufuli alimnyima nini Dangote ambacho Mama anataka kumpatia?
Ni serikali ipi imekuwa ikitatua kila leo migogoro ya wafanyakazi wake pale kiwandani?
Nakumbuka hadi wawekezaji wa ndani walianza kulalamika kuwa Dangote anapendelewa sana ...
Naomba useme hapa serikali ya awamu ya tano ilimfanyia nini kibaya Dangote?
 
Hoja ya msingi mnakimbia matusi,Kwa nn hao Twiga,Tanga,mbeya,camel cement n.k walowekeza miaka hawaendi endi Ikulu kulialia,anaenda Dangote ambaye hata nchini mwao wanamtilia shaka biashara zake za kubebwa
Na hapa nataka waweke wazi ni kitu gani kibaya Dangote kafanyiwa na awamu ya tano?
 
Mkuu hebu weka wazi jinsi awamu ya tano ilivyo kiuka makubaliano baini ya serikali na Dangote.tunaome uyaweke wazi tuache hisia...
Swala la kuletewa gas kiwandani kwake lilifanywa awamu gani na nani aliagiza?
swala la kupewa mgodi wa kuchimba coal lilifanywa awamu gani? nani aliaGIZA?
Alipo kuwa anaingiza magari yake nakumbuka serikali iliingilia kati nakuamuru yatolewe pale bandarini mtwara haraka... hivi hii ilikuwa awamu gani?
Hebu twambieni Magufuli alimnyima nini Dangote ambacho Mama anataka kumpatia?
Ni serikali ipi imekuwa ikitatua kila leo migogoro ya wafanyakazi wake pale kiwandani?
Nakumbuka hadi wawekezaji wa ndani walianza kulalamika kuwa Dangote anapendelewa sana ...
Naomba useme hapa serikali ya awamu ya tano ilimfanyia nini kibaya Dangote?
Na hayo uliyoomba yakishasemwa hapa, tunaomba pia ni yapi aliyoahidiwa hivi juzi hadi akafurahi na kusifu sana, na kuahidi kuvuta wawekezaji zaidi waje kuwekeza.

Haya ndiyo tunayotaka kuyafahamu, yasiwe mambo ya kufanyia gizani tu, huku tukisifu vitu tusivyovijuwa!
 
Hivi kwann kila siku Dangote ni yeye tu Ikulu kwa kila Rais anayeingia?
Je hata viwanda vingine vya cement wako hivyo?

Mi napata mashaka na Huyu bilionea wa Africa,huenda utajiri wake umegubikwa na favor nyingi ambazo kuna watu chini kwa chini wananufaika nate.
Daily Ikulu??????
Ex prezida wa Nigeria ni big shareholder ndio maana kila mgogoro ukiibuka Obasanjo huja Tz .
"Ikulu kuna nini , ikulu ni eeo takatifu." Nyerere voice
 
Mkuu mengii uneandika Ika Sijaona Uliposema pia Ameajiri Management yooote ni Wahindi.

Si ni Bora nikauza Ndizi kuliko kusimamiwa na Muhindi!Yaani Kazi ambazo Watanzania wanaweza kuzisimamia Yeye Kaweka Muhindi,Kenya hii kitu Haipoooo,Hata Kwao Nigeria haipooo.

Watanzania wakilata Nafasi za Management hapo watalipa Kodi,Watalipa Nssf,Kutakuwa na Multplier effect kwa Jamii nk nk!
Watanzania wezi sana...fanya biashara halafu muweke mtanzania wiki tu utaanza kulia

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Mpendwa Rais wangu umejitahidi sana kututoa hofu wa Tanzania kuwa unaweza na jinsia yako sio kitu cha kushindwa kuongoza jahazi na tumekubali na kukupokea kwa mikono miwili yawekana kabisa ukaja kuwa mkombozi wetu kwa nchi yetu.

Naamini kwa muda mrefu taifa lilikosa mtu kama wewe na moderating factor katika Governance.

Kuna tahadhali tunayo sisi wananchi wako hasa kuhusu wawekezaji wanaokuja kukuona na kutoa maomba mbali mbali. Na mfano mzuri ni Dangote, hatujui aliomba nini zaidi mbali ya aliyotunukiwa mpaka muda huu.


DOCUMENTS NDIYO ZITASEMA UKWELI KAMA HAYA YAFUATAYO ALIZAWADIWA DANGOTE BURE.

1) @ &#%*^/#%_=÷×+
2) Mliimpa ardhi bure bila kulipia senti tano.
3) Mliimpa eneo la kuchimba lime bure bila kulipia senti tano.
4) Milimpa bure eneo la kuchimba gypsum bila kulipia senti tano.
5) Mlimmpa uhuru wa kuingia wafanyakazi anavyoona na wengi hawakupata na vibali.
6) Mlimsaidia kuingia magari ya kusambaza sementi bure bila kulipia ushuru mbali ya mntambo.
7) Alipo lalamika kuhusu coal makaa ya mawe mliimpa bure ili achimbe mwenyewe bila kujali sheria ya madini inasameje.
8) Alipata tax holiday ya miaka mitano, afanye biashara yake bila kulipa kodi.
9) Mlimpelekea bomba lá gesi mpaka kiwandani kwake wakati wawekezaji wengine hugharamia wenyewe.
10) Kiwanda bado ni kidogo kuliko Twiga Cement (wazo) ambao yote hayo walilipia kuwapata na hata kodi ya ardhi wao wanalipa.
11) Je, hii ya kuzoea bure kuna fanya malipo ya statuary contributions kama NHIF, NSSF, WORKERS COMPENSATION FUNDS, na michango mingine pamoja na Corporate social responsibility aone atapata bure?

Mkidai kodi halisi anasema anapata hasara yaani mumempa kila kitu bure na sasa anapata hasara na wazalishaji wengine kodi na kulipia huduma zote na kodi kama Twiga Cement, Simba Cement, Mbeya ya cement na viwanda vingine 19 vya kuzalisha cement. Viwanda vyote vingine vinapata faida na kulipa kodi. Haya tutafika.

Marais waliopita ama walikuwa too soft ama extremists lakini mama kuingia kwako tunaamini kuna mazuri yanakuja. Kwa uchache tuu tunaomba ujielekeza kwenye mambo machache muhimu lakini ndio yatakuwa game changer kwa nchi yetu.
Ampe nini mengine ni faragha zao
 
Kwani Kiwanda cha saruji cha Dangote kilianza uzalishaji rasmi lini hapa nchini?

Mwanzo huwa ni mgumu mara nyingi.

Si sawa kulinganisha kiwanda cha saruji Twiga ambacho kina zaidi ya miaka 50 ya uzalishaji n.k

Mwanzoni kunakuwa na gharama nyingi za uzalishaji ambazo ni fixed bila kujali umezalisha au la unlike kina twiga wenyewe wapo kwenye longrun production ambapo in most cases costs zao ni variable.

Kwa hiyo sishangai kama wamekuwa wakipata hasara mfululizo, ni kawaida kabisa sometimes.

Cha maana ni kuwepo na independent auditors wa kuhakiki hizo hasara kama ni genuine au la.

Mimi naona kwenda kwake Ikulu hakuna neno na uwepo wa kiwanda chake una manufaa ila kama mkataba unakasoro upitiwe urekebishwe.
 
Labda Kama unafanya biashara ya masaburi yako, acha Dangote azalishe cement kwa wingi bei ishuke Kama kipindi kile, ili kila mtanzania ajenge pakuweka ubavu


Mnataka mama awe Kama dikteta mwendazake ambae alikuwa anakula mgao kwa viwanda vya ndani ili kumvuruga Dangote
Unafikiri ujenzi wa nyumba unaitaji cement peke yake?
 
Umesahau waliimpa eneo la bahari iwe bandari yake kwa kijiji cha MSIJUTE
 
Weka ushahidi wa documents,kama hauna basi hizi ni porojo za vijiweni.
Jiwe alikuwa shetani,hatabiriki,
Turudi nyuma,Tajiri mkubwa Afrika,Mo anatekwa mchana kweupee,na Serikali inasema haijuhi alipo!!
Lakini serikali hiyo hiyo iliweza kudukua nyaraka za Barick gold zote!!
We unafikiri mfanyabiashara gani hatashituka!Kipindi Cha jiwe,sera na sheria za biashara alikuwa anazitunga akiwa anakata gogo,au "atakavyo amka"mazingira yalikuwa hatabiriki,
Hapa chief Dangote ameenda kupata "assurence"kutoka kwa mwenye mbwa!hawa mbwa wengine hawana akili.
Huu ushuzi .....
 
Hivi kwann kila siku Dangote ni yeye tu Ikulu kwa kila Rais anayeingia?
Je hata viwanda vingine vya cement wako hivyo?

Mi napata mashaka na Huyu bilionea wa Africa,huenda utajiri wake umegubikwa na favor nyingi ambazo kuna watu chini kwa chini wananufaika nate.
Daily Ikulu??????
Pamoja na kuwa tajiri zaidi mweusi ulimwenguni Dangote ana tabia ya kukwepa kulipa kodi na kuwatumia viongozi wengiwa nchi za Kiafrika kwa njia anazojua yeye za asilimia 10, kuna wakati aliwahi kukimbilia nje kutokana na tuhuma za milungura na ukwepaji kodi huko kwao. Dangote si tu ni mjanja kwenye mambo ya biashara bali yeye anachojua ni kushindatu kwa kila dili analolifanya, kifupi Dangote sio mwekezaji mzuri bali ni dhulumati mkubwa.
 
Back
Top Bottom