Rais Samia, nani kakushauri kununua Treni zenye muundo mbovu namna hii?

Rais Samia, nani kakushauri kununua Treni zenye muundo mbovu namna hii?

Sasa nisemeje maana kila kitu wataalamu na waamuzi wa mwisho utafikiri wamo humu [emoji23][emoji23]
Imagine mtu anampa Amri Rais
Rais ni mtumishi wa umma ambao ndiyo sisi. Yeye sio Queen. Sisi tumempa Mandate ya kutuongoza na sio kutuamulia mambo tusiyo yataka. Akiendelea hivyo tuna uwezo wa kumtoa kwa kura zetu na kumchagua mwingine.
 
Hii point wanaipita tu,, hawajui ndio point ya msingi...

Yatima hadeki,, Kawaida maskini huwa unapata unachostahili na sio unachotaka.
Unakuta kuna wanataka mabasi ya mwendo kasi yawe na AC halafu nauli ibaki mia sita😀😀
 
Tena ni light-speed kama tunazoletewa na muonekano mzuri pia
Watu wanaponda muonekano tu ila tutamuita fundi maiko asawazishe [emoji23][emoji23]
Wakileta hio mzee baba itakuwa Magoli sana! Hata wale majirani Kunyans tutawanyoosha kilomolomo
 
Mtoa mada treni unazozitamani zina spidi ambayo reli yetu haiwezi kuhimili. Sasa huoni kama ni upotevu wa rasilimali. Unanunua treni ya zaidi kilomita 300 kwa saa wakati reli yako uwezo wake ni kuhimili chini ya kilomita 200 kwa saa?
 

Kusema kweli leo nimesikitika sana kuona aina ya muundo wa treni ambayo serikali yetu imeweka mkataba na kampuni ya Hyundai-Rotem ni treni zenye mwonekano wa ki-Hitler!

Mimi nilifikiri tunaondokana na treni zenye muundo wa kutisha za enzi za George and Robert Stephenson na kuingia kwenye era ya treni za umeme zenye kuburudisha macho kwa design kama za wenzetu wajerumani.

Mama samia Suluhu Hassan Rais wetu nani kakupa ushauri wa kutua saini ya makubaliano ya kununua treni za aina hiyo? Mimi sitaki kuamini na sikutegema kama aina ya treni ambazo zitatereza kwenye reli yetu zingekuwa na mwonekano huo kwenye hiyo picha ya taarifa tuliyoipata kwenye Website ya hiyo kampuni iliyo shinda zabuni ya Hyndai-Rotem. Mbona inatisha?

Nitashangaa sana kama upande mmoja tumejitahidi kutengeneza Stations nzuri, za kisasa na zenye mwonekano mzuri na wa kupendeza na kupata system yenye technology mpya, alafu leo tunaambiwa kuwa tunapata treni zenye vichwa na mabehewa ya enzi za Hitler? Ama kweli Tanzania tunawatu ambao kweli hawajui kwenda na na wakati. Watu wasiokuwa na test ya biashara. Mnategemea nani mtampata kwenye kwenye hayo ma-wreck yenu?

Mkurugenzi Kadogosa hii sio treni ambazo models zake mtangazaji wako Beni Mwanantala amekuwa akituonyesha kwenye maonyesho uwanja wa sabasaba kurasini.

That's awful! Are you really serious with this mkurugenzi?

Sasa naomba niambie kuna tofauti gani na SGR ya kenya kimwonekano? Inamaana mnatufanya sisi ni masokwe mpaka mnatuletea matakataka kama haya ambayo hakuna mtu anaye yataka?

Waziri wa Ujenzi na uchukuzi hivi ni sahihi kweli sisi watanzania mtusweke kwenye ma-wagon yanayo onekana kama treni za kusafirisha mizigo na wanyama kama haya ambayo hata hayavutii? Mmepewa bure nini? Ama ndiyo tuseme mmedhamiria nini kutuletea? Tuambieni?

Nilipokuwa kwenye jengo lenu la maonyesho ya sabasaba mwaka jana na kujionea mwenyewe models za treni na mabehewa ambayo Mr. Mwanantala alitupa maelezo yake, aisee, nilifarijika sana sana moyoni na niliwaombea baraka nyingi kwa muumba wetu za kuwaongoza vizuri katika shughuli zenu za kuwatumikia Watanzania.

Sikutegemea kabisa kuwa leo ingekuwa siku ya majonzi makubwa kwa kuona au kusikia mashine zitakazo tereza kwenye reli yetu ya kisasa ya SGR kumbe ni madudu ambayo yamepitwa na wakati na yasiyo na mvuto hata lidogo. ES IST SCHRECKLICH!

Tumeshindwa kufika bei kwenye miundo inayovutia. Umesahau msemo MKIA WA MBUZI UNAJIKUNA UNAPOISHIA!!?
 
Rais ni mtumishi wa umma ambao ndiyo sisi. Yeye sio Queen. Sisi tumempa Mandate ya kutuongoza na sio kutuamulia mambo tusiyo yataka. Akiendelea hivyo tuna uwezo wa kumtoa kwa kura zetu na kumchagua mwingine.

Sio kwetu mkuu
Humu tunajifurahisha tu
Hata alietangulia alituburuza alivyotaka na tulishindwa kufanya kitu

Hii ni jamhuri ya JF acha tufurahie uhuru wetu hapa tukiwa kwenye bubble
 
Toka awali kwenye tenda walishaonyesha sample ya injini zitakazotumika, kulinganisha na bajeti , kwa hiyo wewe unachofahamu zenye kutumia umeme ni zile tu zenye kichwa kama cha nyoka?!!!hahaaa, inayokwenda km 320 kwa saa!!kazi kweli kweli, toka SGR, ina dizainiwa walijua ni mabehewa ya aina gani na injini zake, sasa leo mnataka kama zile za ulayaaaa?!!jamani jamani!!ndio maana wameshakuambia hiyo itakimbia km 160/saa!! Sasa hayo mambo ya eti mizania ni mtazamo wako na sio wa kihandisi.
Kwanini sasa tuwe na reli kama za Ulaya?
 
Hahaaaaa!!!hicho kitu kwa hii SGR yenu ni sawa gari aina ya limozini kuitumia ktk barabara za DRC!!hasa za mashariki mwa congo!!haitaweza kutembea hata hatua moja!!!weeee usilete utanii na hilo dude kichwa tu kama MJUSI KAFIRI!!!!
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Badala ya kujua specifications za hizo treni anaangalia muonekano. Halafu hela ya kununua treni anayotaka hana. Kazi kweli kweli
Ndugu Ndhani usidhani baada ya Rais kuapishwa March 19 ndo mchakato wa kununua mabehewa hayo ulipoanza. La hasha. Michakato kama hii huanza takribani mwaka mmoja kabla kabla ya ununuzi kufanyika. Hivyo hapa mchakato utakuwa ulianza tangu mwaka jana. It is a long process. Rais Samia amerithi kile kilichoanza na inambidi aendeleze tu.
 
kama ni hii kitu ni kweli sijui tutaficha wapi sura zetu wakija kina MK254 maana tulikuwa tunawakashu sn yale matreni yao ya makaa ya mawe....tumekwisha
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Kwa ninavyojua hiyo ni kampuni hawaja ainisha which model exactly ndio italetwa maana wana model nyingi za trains

Kama ilivyo Toyota or any other company
IMG_3795.jpg

IMG_3793.jpg

IMG_3795.jpg
 
Wabongo sijui huwa hatuna uwezo wa kufikiri, mtu kawekewa just a random photo "courtesy of..." tayari kashatunga na habari tokea kwenye picha...

"Electric trains are worth 215.7 billion won and electric locomotives 119.7 billion won. They will be delivered to Tanzania by 2024.", hadi sasa hakuna behewa lililoundwa...
 
Garama gani unazozizungumzia? Kwani watu watapanda hizo treni kusafirisha mizigo yao bure? Sie kitega uchumi cha taifa ili kituingizie mapato?
Kuna vitu vinaangaliwa ili wasiwabebeshe mzigo wanyonge kulipishwa kodi ili serikali iweze kutoa ruzuku kwa TRC ikijiiendesha kwa hasara, si umeona shirika la ndege ripoti ya CAG inasemaje? Kikubwa hivyo vichwa vihimili mikikimikiki ya kwetu mara gari limegonga treni mara ng'ombe wamegonga treni tena kwenye kichwa pale mbele nashauri waweke chuma cha pua atakae jipendekeza afyekelewe mbali na treni iendelee na safari.
 
Back
Top Bottom