Rais Samia: nataka itumike "Single Source." Je, "Force Account" za JPM na "Zabuni Shindanishi" za JK zimeishia wapi? Sheria ya manunuzi imefutwa?

Rais Samia: nataka itumike "Single Source." Je, "Force Account" za JPM na "Zabuni Shindanishi" za JK zimeishia wapi? Sheria ya manunuzi imefutwa?

Single source hukubalika tu iwapo anakosekana aliye na uwezo wa kufanana na anayechaguliwa kwenye tendainayohitaji utaalamu mkubwa ama kama chombo kinachohitajika hakipatikani kwingine!!
 
Mkuu mbona alifafanua vizuri kabisa,kwamba hizi pesa tulizopewa inabidi tuzitumie kwa muda wa miezi Tisa kukamilisha hiyo mipango yetu...

Sasa tukisema tufuate taratibu za manunuzi ya serikali au kugawa tenda basi miezi Tisa itafika na tutakua hatujafanya jambo lolote maana taratibu za ugawaji tenda au manunuzi za serikalin zinatumia muda mrefu.

Kwaio akapendekeza itumike njia ya single source ili kukimbizana na muda ...shughuli nyingine za kwenye miradi mingine wataendelea kama kawaida na force account.
Walioleta hizo procurement units katika serikali na taasisi za umma ni hao hao IMF na World Bank. Bila kufuata taratibu za manunuzi IMF na World Bank hawatoi fedha. Sasa sijui wamebadilika lini?

Time frame kuwa IMF wametukopesha fedha zitumike ndani ya miezi 9 ni uongo wa mchana kweupe! Lazima kuna nongwa hapa kwa nini single source?
 
Mbona MTU ukitumia akili vyema utajua sifa za mradi kuwa either nyeti au dharura..! Dharura ni pale umepewa muda maalumu wa kukamilisha mradi ambao ukiúpima unauona ni mdogo ukicompare na scope ya kazi yakufanyika, au mradi kuwa na ulazima wa kukamilika kwa haraka. Na case ya unyeti ni mradi ambao sio kila mtu anapaswa kuona michoro yake kwa ajili ya usalama mfano ujenzi wa ikulu, gereza, benki kuu na mengineyo ya mtindo huo, hivyo hukifanya tenda shindani yakupasa kuweka na drawings kwa ajili ya makadirio ya gharama kwa wazabuni ambapo michoro hiyo kutakuwa na chance ya kuingia mikono ya watu wabaya.
Katika hizo sifa ulizoainisha ujenzi wa madarasa na vyoo vya shule ni nyeti?
 
Tusipende kila wakati kuwa wapotoshaji. Mama amelisema hili wazi na kwa ufasaha kwamva ile sheria ina ruhusu single sourcing kwahiyo kusema shetia iko wapi ndiyo hiyo ina options na sababu za kutumia hizo options amezisema ni kuhakikisha madarasa yanajengwa kabla ya watoto kuanza shule January.

Tuache kuyumbisha viongozi kwa sababu zisizo za msingi. Kweli tutoe maoni ila maoni hayo yawe na lengo la kujenga siyo kubomoa
Mkuu nani kakwambia hapa anatoa maoni kwa lengo la kubomoa ?
 
Japo nakubaliana na wewe kwa hili, ila urgency ya Mh. Rais pia inamashiko. Chamsingi ni hata hao single sourced wawekwe wazi ni akina nani ili kupunguza upendeleo wa watu wenye makampuni yao.

All in all corruptions hata kwenye hizo tendering zipo tu. Vyombo vyetu vya usalama vikifanya kazi yake vizuri na kulazimisha uwazi wala hakuna tatizo
Unaongea as if unazungumzia nchi nyingine siyo Tanzania
 
Leo wakati Rais akizindua mpango wa maendeleo (tafsiri "matumizi") ya pesa ya Covid kutoka IMF, amesema anaagiza watumie "single source" kwenye manunuzi na kandarasi. Kasema zabuni za kawaida zinatuchelewesha, hataki kuzisikia.

Swali langu lina sehemu mbili tatu:

hivi taratibu za matumizi ya zabuni shindanishi haziko kisheria ?

the biggest political upheaval ever in this country, ukiondoa Nyerere kufukuzwa Ikulu na jeshi kwa masaa 48, ni pale Prime Minister Lowassa na Principle Secretary Msabaha na wengine walipotimuliwa na shinikizo la tume ya Mwakyembe kwa kushindwa kuzingatia taratibu za manunuzi na zabuni, procurement and tendering.

likaja wimbi kubwa la kutilia mkazo mambo ya procurement, watu mpaka mameneja kwenye mashirika na mawizara wakapelekwa vyuoni na kwenye ma semina kusomea kozi za procurement, sheria ikawa amended ikapewa meno, ikaundwa regulatory body inayoshughulikia procurement tu.... tunakumbuka ?????

haya, akaja Marehemu, akawa anauliza maafisa majukwaaani, mnatumia "force account" ? Force account ikawa habari ya mjini.

sasa leo Rais Samia katangaza anaagiza watumie "single source."

Single source ni nini?

Force account ni nini?

Na zabuni shindanishi zimefutwa lini?

na kwa nini zilikuwa haliteti tija ?

na ni wapi wameona single source au force account ni bora zaidi? Kwa ripoti gani?

tumeacha kupigwa kwenye makandarasi toka single source and force account zije ?

Na Rais anawezaje kufuta sheria ya bunge thabiti jukwaani ?????



Single source? dangerous......a joke! Unless is unaccounted money...
 
Wanajaribu kututisha ili tuogope KUHOJI madudu yao Mkuu lakini wanasahau baadhi ya Watanzania wa 2021 si kama wale wa miaka ya nyuma.

Ndiyo maana wamekuwa wakali sana siku hizi
 
Wanajaribu kututisha ili tuogope KUHOJI madudu yao Mkuu lakini wanasahau baadhi ya Watanzania wa 2021 si kama wale wa miaka ya nyuma.
Jamaa wamejipanga kuiba kweli kweli kwenye hii awamu.

Muda utasema aisee
 
  • Nzuri
Reactions: BAK
Mbona huwa mnapenda kupotosha mambo bila sababu?

Utaratibu wa single sourcing upo kisheria,na umekuwa ukitumika mara nyingi katika manunuzi ya serikali pale inapohitaji huduma za dharura.

Iko hivi, angalau watoa huduma watu wanaombwa kutoa bei zao,halafu mwenye bei ya kuridhisha anapewa kazi.
Wewe ndio unapotosha. Single source hauiti watu zaidi ya mmoja watoe watoe bei zao. Ukifanya hivyo itakuwa "competitive bidding " na sio single source. Ni kweli single force inatumika kwa kazi za dharura ambazo haziruhusu kufanya tathmini ya maombi tofauti. Kwa mfano, kuna kisima cha mafuta kinawaka moto na mkichelewa kuuzima kitaleta athari kubwa kwa maisha na mali za watu.

Sehemu nyingine ni pale huduma hiyo au kivaa hicho kinapatikana kwa mtu mmoja. Mathlani mnataka spare part ya ndege ya Boeing. Bila shaka mtamuambia Boeing alete quotation yake na sio Airbus au Embraer. Sehemu nyingine ni unyeti wa mradi. Single source itatumika ili kupunguza idadi ya watu kujua mnachonunua. Kwa wenzetu hata silaha za kivita wanashi wazabuni.

Kwenye hili, sioni udharura au unyeti wa kujenga madarasa au ununuzi wa vifaa vya x-ray n.k. Aidha, hauwezi kusema kuwa kuna watu wachache tu wenye uwezo wa kujenga madarasa au kutuuzia vifaa tunavyotaka kununua. Kama tunataka madarasa ya dharura basi ni bora tungegeuza makontena kuwa madarasa.

Mwisho ni kuwa mpangilio wa matumizi ya hizi fedha ni uamuzi wetu. Tungeweza kuamua kuwasaidia wenye biashara za utalii kupunguza madeni waliyoingia baada ya watalii kuacha kuja Tanzania. Tungeweza kuzipa hospitali binafsi pesa ili zipunguze gharama za huduma kwa ajili ya watu wenye wagonjwa hawa. Tungeweza kuwasaidia wakulima wa mbogamboga na matunda kufidia hasara waliyopata baada ya ndege kuacha kuja Tanzania. Hatulazimishwi kujenga majengo yeyote. Kama tunaona yana umuhimu, basi tungetumia kwa ajili ya awamu za mwanzo za ujenzi halafu tungemalizia kwa fedha zetu baada ya muda uliowekwa kama sharti la mkopo utakapomalizika. Single source kwa hali hii sio nzuri.

Amandla...
 
Single source na force account zipo kwenye sheria mkuu. Ulishaona tenda za vifaa vya majeshi ya ulinzi na usalama vinatangazwa magazetini mkuu?
Zinatangazwa sana tu
 
Mkuu single source hutumika kwa case ya miradi ya dharura( uharaka) au miradi yenye unyeti( confidential) hivyo mh. Rais ameona time tuliyonayo ni ndogo kwa mpango husika kwa hiyo miradi mingine itaendelea kufuata utaratibu wa kawaida either forced account au competitive tendering.
Rais ameona mbali, uzalendo na adabu ya kutumia pesa lazima, usipofanya unafungwa over
 
Mkuu mbona alifafanua vizuri kabisa,kwamba hizi pesa tulizopewa inabidi tuzitumie kwa muda wa miezi Tisa kukamilisha hiyo mipango yetu...

Sasa tukisema tufuate taratibu za manunuzi ya serikali au kugawa tenda basi miezi Tisa itafika na tutakua hatujafanya jambo lolote maana taratibu za ugawaji tenda au manunuzi za serikalin zinatumia muda mrefu.

Kwaio akapendekeza itumike njia ya single source ili kukimbizana na muda ...shughuli nyingine za kwenye miradi mingine wataendelea kama kawaida na force account.
Hapa sawa
 
Kwa mtindo huu rushwa itatamalaki na vikampuni vya mifukoni vingi vitaanzishwa, mwendazake alilaumiwa kwa Mayanga Construction huyu nae anajitengenezea mazingira.
Vikianzishwa sio tatizo ishu ya muhimu wafanye delivery na value for money ionekane.
 
Back
Top Bottom