Rais Samia ni kazi kwako kuwaacha au kuwaondoa ‘for the sake of the nation and the party’

Rais Samia ni kazi kwako kuwaacha au kuwaondoa ‘for the sake of the nation and the party’

Kodi halali ya Serikali lazima tulipe, tusitegemee kuonewa huruma kwenye mapato ya Serikali.
Kama yule mama anadaiwa Kodi ya billioni 3 halafu anataka kukwepa eti alipe milioni 150!!!
hili haliwezekani, Kodi halali lazima ilipwe.

Nasema wakwepa Kodi wa kubwa ni wafanyabiashara wakubwa hawa ndio wanaongoza kukwepa Kodi na kutoa rushwa kwa TRA
Sawa Ng'wigulu
 
Kampeno gani mkuu
Andiko lako linaonyesha wazi kwamba kuna watu unawalenga na siyo matatizo yaliyopo kutatuliwa.

Unapokuja namna hiyo kwenye mada, kuonyesha ushabiki badala ya utatuzi wa matatizo, unakuwa kama mpiga kampeni tu.

Hakuna ninayemtetea hapa kwenye haya maswala ya wafanya biashara na mfumo mzima mbovu wa ukusanyaji wa kodi. Pande zote mbili ni hovyo kabisa, na sitegemei kwamba kutakuwa na utatuzi wa maana kwenye swala hili.
 
Kama mpaka sasa hakuna PDF maza anachemka
 
Uchawi upo mpaka Sada hii nasoma Ikulu mawasiliano no press release
Nilijua mkutano ungeisha tu basi mwigulu out
 
Andiko lako linaonyesha wazi kwamba kuna watu unawalenga na siyo matatizo yaliyopo kutatuliwa.

Unapokuja namna hiyo kwenye mada, kuonyesha ushabiki badala ya utatuzi wa matatizo, unakuwa kama mpiga kampeni tu.

Hakuna ninayemtetea hapa kwenye haya maswala ya wafanya biashara na mfumo mzima mbovu wa ukusanyaji wa kodi. Pande zote mbili ni hovyo kabisa, na sitegemei kwamba kutakuwa na utatuzi wa maana kwenye swala hili.
Kuna nyuzi zaidi ya 7 za watu wametajwa na majina kabisa mimi sijamtaja mtu
 
Kama mimi nimefanya biashara ya 100 Million na nikapatq Faida ya 20 M kwa nini nilipe kodi kwenye 120 M badala ya 20 M ambayo ni profit..?
Mkuu, hiyo ndo shida ya serikali, kuna kitu inaitwa PAYE, mtumishi wa serikali na taasisi zake, PAYE inakatwa kwenye BASIC tu ILA kwa mtumishi wa sekta binafsi, PAYE inakatwa kwenye GROSS.

Jua, watumishi hawana namna yoyote ya kukwepa au ku-negotiate na afisa wa kodi!

Wakate kodi zote kwenye kuingiza mzigo, basi!
 
Simtetei mtu ila binafsi sioni kosa so Hakuna wa kuondoa na waondoke Kwa lipi? Kodi zote zimetungwa na Bunge ,hapo ni kubadili mechanism au approach ya kukusanya ila sio ishu ya Waziri hapo.
Yaani hili Bunge kibogoyo sana. Spika yupo busy kuongezea maisha magumu wananchi kwa kutaka jimbo lake. Maisha yanakuwa magumu kwa pesa zetu kutumika kijinga sana. Hili suala la kuwa na wabunge wa vitimaalum ni upuuzi sana.
 
Hao Wafanyabiashara walimkataa Hadi Mkuu wa Mkoa walidai Rais huu ni utoto wa Nidhamu na kuyumbisha Nchi..

Rais atafanya kazi ngapi? Nini maana ya kuwa na wasaidizi?

Mwisho ndio maana katika mchango Fulani nilisema Kuna madai geguine mfano unaenda Polisi kumshitaki afisa wa TRA ,then wewe unakuja kugeuziwa kibao ,hii inatakiwa kuwa addressed..

Mojawapo ya njia za kutatua Hilo ni Kwa Mkuu wa Mkoa pamoja na maofisa wa TRA walau kuwa na mkutano mara 1 Kila baada ya miezi 3 kujadili kero na utatuzi wake,ikifanyika hivyo hatutafikia Kwa PM au Waziri..

Kama Kuna mambo ya kisera ndio Waziri anaweza kuja kutoa ufafanuzi au kuchukua kuyapeleka huko Baraza la Mawaziri Kwa hatua zaidi..
Kitu ambacho hukijui
Wafanyabiashara wa sasa wana uelewa mkubwa sana tofaut na Wale wa zamani
Nazani umeona hoja zao
 
Kipekee nakushukuru kwa kuchukua hatua za dhati za kunusuru soko la kariakoo kwa kumtuma Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa. Kwa kweli amefanya kazi kubwa ya kunusuru uchumi wetu.

Pamoja na yote yaliyojadiliwa kuna kiu cha uwajibikaji. Imedhihirika baadhi ya watendaji wako wana uwezo mdogo na wengine ni wazembe na wenye zarau

Ni ombi letu na kama itakupendeza wachukulie hatua au wahamishe au wasimamishe kazi wote walioonekana ni kikwazo kwa wafanyabiashara na uchumi wetu. Na katika hili usiwaache kambare ukaondoa dagaa utakua haujafanya kitu.

Kwa macho yako umeona kiu cha wale ambao wanalalamikiwa ni kazi kwako kuwaondoa au kuendelea kuwafuga.

Nakukumbusha Mh. Jakaya alimuondoa Kalamagi, Nchimbi, Lowasa. Pia Chuma JPM aliwaondoa Kangi Lugola, Mwigulu, Simbachawene nk ili kuleta ustawi na kuonesha uwajibikaji kwa watanzania

Sasa kama hautakuwa na serikali ya uwajibikaji au hata kuhamisha watendaji na mawaziri au hata kuwaondoa basi madhara yatakayotokea ni juu yako na utawala wako.

Chukua hatua
Achana na matumizi ya siasa katika kutatua matatizo kwa maneno tu. Hapa sheria itumike ili kubadilisha mambo ya Kodi. Jamaa wanafuata sheria ambayo imetungwa na hao hao wanasiasa. Ili yaliyoongelewa yaweze kutendeka shurti yapitishwe na kuwa sheria. Vinginevyo ni usanii kama usanii mwingine.
 
Ukiona watu wanamtaka mama maana yake hawasikikizwi! Nikuambie tu watanzania wetu tumechoka, TRA wamekuwa wezi wakubwa na rushwa mingi, acheni watu wagome
Yaani kwani haiwezekani, kubadilisha team za wafanyakazi wa TRA kutoka sehemu moja nyeti kama bandarini, long room au mipakani, kwenda sehemu nyingine(benchi), kila baada ya kipindi fulani', Ili kupunguza kiburi wanapokaa sehemu moja kwa muda mrefu, na matokeo yake ndo haya ya kuikosesha serikali mapato yaliyokusudiwa kutokana na wafanyakazi hao kutumia 'kanuni kandamizi za TRA vibaya....mie naona labda ikiwapendeza, hili nalo pia wakalitizame......
 
Niliwahi kipewa makadirio ya 54 Million kutokana na ongezeko la Mapato
Nilibishana na TRA kwa miezi miwili
Kwenye rerun ya mwaka unaofata zile tenda sikupata tena kwaoo income ikashuka nikarud TRA kuwauliza wa review kodi yao

Baada ya purukushani sana wakatoa kodi currently 20Million

Kwaio kwa watu ambao Havana uelewa wanaumizwa sana na TRA
TRA ni wahuni sana, walimkadiria ndugu yangu kodi ya laki 6 kwa mwaka akalipa, kabla ya mwaka kuisha akawa amepata kazi ya madarasa ya covid, mwaka kuisha acc yake ikawa inasoma parefu lkn tayari kazi za covid zimeisha, aliporudi kujadiriwa tena mwaka unaofuata wakamwambia mwaka jana tulikadiria vibaya kwahiyo kuna kodi ilisaulika ya sh 2.8mln unatakiwa uilipe ndipo tuendelee na makadirio ya mwaka huu.Unaona huo ujinga.
 
Kipekee nakushukuru kwa kuchukua hatua za dhati za kunusuru soko la kariakoo kwa kumtuma Waziri Mkuu Mh. Kassim Majaliwa. Kwa kweli amefanya kazi kubwa ya kunusuru uchumi wetu.

Pamoja na yote yaliyojadiliwa kuna kiu cha uwajibikaji. Imedhihirika baadhi ya watendaji wako wana uwezo mdogo na wengine ni wazembe na wenye zarau

Ni ombi letu na kama itakupendeza wachukulie hatua au wahamishe au wasimamishe kazi wote walioonekana ni kikwazo kwa wafanyabiashara na uchumi wetu. Na katika hili usiwaache kambare ukaondoa dagaa utakua haujafanya kitu.

Kwa macho yako umeona kiu cha wale ambao wanalalamikiwa ni kazi kwako kuwaondoa au kuendelea kuwafuga.

Nakukumbusha Mh. Jakaya alimuondoa Kalamagi, Nchimbi, Lowasa. Pia Chuma JPM aliwaondoa Kangi Lugola, Mwigulu, Simbachawene nk ili kuleta ustawi na kuonesha uwajibikaji kwa watanzania

Sasa kama hautakuwa na serikali ya uwajibikaji au hata kuhamisha watendaji na mawaziri au hata kuwaondoa basi madhara yatakayotokea ni juu yako na utawala wako.

Chukua hatua
Nyerere alishasema ukiona serikali inaangaika angaika na vikodi vidogovidogo ujuwe ni serikali ya Wala rushwa, r.i.p jpm wewe uliangaika na Kodi za wakubwa ambao Sasa wanapeta
 
Sasa anajikadiria Kodi mwenyewe eti alipe 150millioni!!!!!

Huyu ni mkwepaji mkubwa wa kulipa Kodi halali na anataka kutumia kichaka Cha mazungumzo haya, alipe anacho daiwa aache janjanjanja
Sasa kwanini TRA wakashuka tena from 30bil to 10bil baada ya yule mother kuyasusa makontena bandarini? Mpaka hapo hupati kitu akilini kuwa TRA wanapanga kodi kwa mafikirio on capital invested and not on profit?
 
Inatakiwa udondoshwe mbuyu, bila hivyo mambo yatarudi palepale. TRA wanafata wafanyabiashara nyumbani, kama si kwenda kuchukua rusgwa ni nini? Tena wote hao watolewe, ili watakaokuja wajihami.
Na ni wepesi kweli kupiga simu "Unadaiwa Mill kadhaa, na inaongeleka kupata punguzo" alafu ukiwajia juu hawapigi tena🤣🤣
Ifikie kipindi hizi kodi za mafikirisho ili kutengeneza mianya ya rushwa kwa watumishi wa TRA idhibitiwe kwa kuwawajibisha wahusika.
 
Back
Top Bottom