Tafakari yetu
JF-Expert Member
- Apr 19, 2021
- 1,505
- 4,427
Anaweza kubezwa leo kwa anachofanya lakini akakubwa kesho na kiongozi bora hafanyi kwa ajili ya leo tu anafanya kwa ajili ya kesho. Baadhi ya nukuu na hotuba za Mwalimu Nyerere bado zinaishi mpaka leo na ukizisikiliza unaweza kufikiri ni leo ndio anazungumza. Kipindi Cha Mwalimu kuna walioshindwa kumuelewa hapo hapo na siku zinaposonga ufahamu wa kuelewa ukiongezeka wanamwelewa na Kuna wengine hawakumuelewa kabisa. Mwalimu aliishi kizazi Cha mbele Sana.
Rais Samia anajua mahitaji ya watu, ni mbeba maono. Ni kiongozi bora Sana. Inawezekana aina yake ya uongozi tukashindwa kuilewa leo lakini kesho ni mtaji wa kisiasa. Anatuandalia mazingira ya kesho.
Sio rahisi, halijawahi kuwa Jambo rahisi kwa watawala kuamua kukutana na watu ambao wakigeuka nyuma wanakutukana na hapohapo wanataka mkubaliane. Rais Samia kwa kujua yote bado anakaa na watu hao anafanya hivyo kwa ajili ya Tanzania, ni maono na matarijio ya watu. Mwalimu aliwahi kusema kiongozi bora ni yule aliyebeba matarajio ya wananchi hasa ya mpigakura.
Licha ya kutambua anachofanya Cha kukutana na upinzania pengine CCM hakiwaridhishi kabisa lakini kwa ajili ya Tanzania ameona njia hiyo ni salama na bora. Hapo ndipo tunapoona kabeba maono ya wananchi wote na si ya wana-CCM pekee.
Nasema tena, ukishindwa kuelewa anachofanya Rais Samia Sasa usilazimishe kujifanya unajua unatakiwa uwe mvumilivu wakati utafika utamuelewa.
Tunaomuelewa Sasa Rais Samia hatuteswi na kivuli Cha kuona atashindwa kuifikisha Tanzania mbele ila tunaiona Tanzania yenye maendeleo, maono ya Rais Samia ni kamili na hayana danadana wala kubumba na yanatimia kadiri mshale wa saa unaposonga mbele.
Rais Samia anajua mahitaji ya watu, ni mbeba maono. Ni kiongozi bora Sana. Inawezekana aina yake ya uongozi tukashindwa kuilewa leo lakini kesho ni mtaji wa kisiasa. Anatuandalia mazingira ya kesho.
Sio rahisi, halijawahi kuwa Jambo rahisi kwa watawala kuamua kukutana na watu ambao wakigeuka nyuma wanakutukana na hapohapo wanataka mkubaliane. Rais Samia kwa kujua yote bado anakaa na watu hao anafanya hivyo kwa ajili ya Tanzania, ni maono na matarijio ya watu. Mwalimu aliwahi kusema kiongozi bora ni yule aliyebeba matarajio ya wananchi hasa ya mpigakura.
Licha ya kutambua anachofanya Cha kukutana na upinzania pengine CCM hakiwaridhishi kabisa lakini kwa ajili ya Tanzania ameona njia hiyo ni salama na bora. Hapo ndipo tunapoona kabeba maono ya wananchi wote na si ya wana-CCM pekee.
Nasema tena, ukishindwa kuelewa anachofanya Rais Samia Sasa usilazimishe kujifanya unajua unatakiwa uwe mvumilivu wakati utafika utamuelewa.
Tunaomuelewa Sasa Rais Samia hatuteswi na kivuli Cha kuona atashindwa kuifikisha Tanzania mbele ila tunaiona Tanzania yenye maendeleo, maono ya Rais Samia ni kamili na hayana danadana wala kubumba na yanatimia kadiri mshale wa saa unaposonga mbele.