Rais Samia: Nilidhani ningefika nao upande wa pili lakini ajali zinatokea

Analogia Malenga

JF-Expert Member
Joined
Feb 24, 2012
Posts
5,108
Reaction score
10,191
Rais Samia amesema Waziri mmoja amedondoshwa kwa kuwa ni kawaida kwenye safari kuna ajali zinatokea. Amesema hayo katika hotuba yake baada ya kuwaapisha wateule wake aliowateua hivi karibuni.

Rais amesema alitamani team yake ya awali amalize nayo hadi kufika ngwe ya pili (Muhula wa pili wa uongozi) hata hivyo hali imekuwa tofauti.

Amesema kwa Makatibu wakuu wengi wamebaki ila sio kama hawana makosa bali 'mama analea'.

Aidha amejibu hoja za watu wa mtandaoni wanaosema kuwa mama anawachukua watu wenye akili kwenye maeneo tofauti, amesema watu hao wakibaki huko huwa wanakosoa sana hivyo ni bora waingie serikalini wajue ilivyo ngumu kutekeleza. Pia amesema mtu akiwa na akili ndio anamuhitaji zaidi lakini watanzania wote wana akili.
 
Ajali wapi ipo kidini zaidi na sio ajali

USSR
 
Ajali wapi ipo kidini zaidi na sio ajali

USSR
Hakuna kitu mbaya kama ulikua unashabikia utawala unaokupa kula ghafla ukatoweka na kubaki mpenz mliaji kila cku 🤣🤣🤣🤣
 
Hatukupingi mama much love huku ataujumbe me napokea
 
Naona wakosoaji wa nje wamechukuliwa wakawekwa ndani ili wajionee uhondo wa ngoma kwa namna ya mchawi mpe mwanao akulelee.

Ajabu ni pale Rais anapotamka amewachukua wasomi wa nje na kuwapeleka serikalini ili wajionee ugumu wa utekelezaji majukumu, binafsi sioni sababu kwanini ugumu uwepo kama nyenzo na vitendea kazi vinakuwepo maeneo husika.

Mambo mengine kama uzembe wa watendaji ni kushughulika nao instantly, sio kulalamika ugumu, ikiwa uwezo wa kuwashughulikia unao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…