Rais Samia, Ondoa RC Tabora na DC Nzega, Hawajitambui

Rais Samia, Ondoa RC Tabora na DC Nzega, Hawajitambui

Bams

JF-Expert Member
Joined
Oct 19, 2010
Posts
19,362
Reaction score
48,879
Nchi hii inashindwa kufika mahali ilipotakiwa kufika kwa sababu ya kuongozwa na watu wasiojitambua, wasiojua wajibu wao wala mipaka ya mamlaka yao.

Kuna habari zinazunguka mitandaoni kuwa eti DC wa Nzega ameamuru mkuu wa Chuo Cha Madini Nzega awekwe ndani kwa sababu alishindwa kumjibu mkuu wa Mkoa wa Tabora alipotembelea chuo hicho.

Kwanza, hawa viongozi, wote wawili ni dhahiri inaonekana hawana uelewa wa chochote kwenye mifumo ya utawala.

Chuo cha madini Nzega kipo chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kama kuna matatizo kwenye branch hiyo ya UDSM, walitakiwa kuwasilidha malalamiko yao kwa mkuu wa Chuo Kikuu, UDSM, ambaye ni Rais Mstaafu Jakaya Kikwete au Vice Chancelor wake.

Bila shaka hawa viongozi ni wale malimbukeni wa madaraka. Kwa vile tu sheria inatamka kuwa wanaweza kutoa amri ya kumweka mtu ndani kwa muda usiozidi masaa 48, kwa ujinga wa kutojua mantiki ya sheria hiyo, wanaichukulia kumweka mtu ndani ni kama adhabu, wakati lengo la sheria hiyo lilikuwa kwa kuzingatia mazingira ya nyakati na mahali. Mathalani mtu anaonekana akiwa huru anaweza kuendelea kudhuru au kudhuriwa, na vyombo vya kisheria vya udhibiti havipo eneo la karibu, basi mkuu wa mkoa au wilaya, alipewa mamlaka hayo ili kipindi hicho akiwa ndani, kitumike kuwasiliana na mamlaka husika. Unajiuliza, huyo mkuu wa hiyo branch ya UDSM alikuwa anamdhuru nani hadi awekwe ndani, jibu linakuwa moja tu, kuwa huyo DC inaonekana ni empty kabisa kichwani kwa masuala ya utawala na sheria.

Rais anapoteua watu kwenye nafasi fulani, hasa kwa nchi iliyojaa machawa, rushwa na vyombo dhaifu vya vetting, inakuwa ni kubahatisha, lakini inapodhihirika, kama ilivyo kwa hawa watu, kuwa wateule ni watu duni kiutendaji, inatakiwa kuwafukuza mara moja kabla hawajaleta madhara makubwa zaidi.
 
Nchi hii inashindwa kufika mahali ilipotakiwa kufika kwa sababu ya kuongozwa na watu wasiojitambua, wasiojua wajibu wao wala mipaka ya mamlaka yao.

Kuna habari zinazunguka mitandaoni kuwa eti DC wa Nzega ameamuru mkuu wa Chuo Cha Madini Nzega awekwe ndani kwa sababu alishindwa kumjibu mkuu wa Mkoa wa Tabora alipotembelea chuo hicho.

Kwanza, hawa viongozi, wote wawili ni dhahiri inaonekana hawana uelewa wa chochote kwenye mifumo ya utawala.

Chuo cha madini Nzega kipo chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kama kuna matatizo kwenye branch hiyo ya UDSM, walitakiwa kuwasilidha malalamiko yao kwa mkuu wa Chuo Kikuu, UDSM, ambaye ni Rais Mstaafu Jakaya Kikwete au Vice Chancelor wake.

Bila shaka hawa viongozi ni wale malimbukeni wa madaraka. Kwa vile tu sheria inatamka kuwa wanaweza kutoa amri ya kumweka mtu ndani kwa muda usiozidi masaa 48, kwa ujinga wa kutojua mantiki ya sheria hiyo, wanaichukulia kumweka mtu ndani ni kama adhabu, wakati lengo la sheria hiyo lilikuwa kwa kuzingatia mazingira ya nyakati na mahali. Mathalani mtu anaonekana akiwa huru anaweza kuendelea kudhuru au kudhuriwa, na vyombo vya kisheria vya udhibiti havipo eneo la karibu, basi mkuu wa mkoa au wilaya, alipewa mamlaka hayo ili kipindi hicho akiwa ndani, kitumike kuwasiliana na mamlaka husika. Unajiuliza, huyo mkuu wa hiyo branch ya UDSM alikuwa anamdhuru nani hadi awekwe ndani, jibu linakuwa moja tu, kuwa huyo DC inaonekana ni empty kabisa kichwani kwa masuala ya utawala na sheria.

Rais anapoteua watu kwenye nafasi fulani, hasa kwa nchi iliyojaa machawa, rushwa na vyombo dhaifu vya vetting, inakuwa ni kubahatisha, lakini inapodhihirika, kama ilivyo kwa hawa watu, kuwa wateule ni watu duni kiutendaji, inatakiwa kuwafukuza mara moja kabla hawajaleta madhara makubwa zaidi.
Hehehe
 
Mkuu wa chuo alikuwa "ndwii" yule hajitambui!

RC na DC wako Sabihi walikuwa wanatekeleza majukumu yao katika eneo lao la kazi!


Kama wanaamini kuna kosa amefanya wanatakiwa kupeleka malalamiko yao kwa mwajiri wake, ambaye ni UDSM.


Ni lini uliwahi kusikia RC wa Dar au Dodoma, walienda UDSM au UDOM kuwafukuza wafanyakazi au kuwaweka ndani kwa sababu wameshindwa kutekeleza wajibu wao.

Huyo DC na RC, ni limbukeni wa madaraka wasiojua ukomo wa madaraka yao.
 
Mleta mada hujui mkuu wa mkoa na wilaya ni akina nani

Hao kwanza ni viongozi wawakilishi wa Raisi kwenye maeneo yao Ni maamiri jeshi wa maeneo yao ndio maana hupigiwa saluti na vyombo vya ulinzi na usalama
Wao ndio viongozi wakuu wa kusimamia taasisi za serikali katika maeneo yao

Kuajiriwa Chuo kikuu cha Dar hakumfanyi yeye kuwa juu ya mkuu wa mkoa au wilaya yuko chini yao kama alivyo chini ya Raisi
Kama ambavyo mkuu wa UDSM yuko chini ya Raisi
 
Kama wanaamini kuna kosa amefanya wanatakiwa kupeleka malalamiko yao kwa mwajiri wake, ambaye ni UDSM.


Ni lini uliwahi kusikia RC wa Dar au Dodoma, walienda UDSM au UDOM kuwafukuza wafanyakazi au kuwaweka ndani kwa sababu wameshindwa kutekeleza wajibu wao.

Huyo DC na RC, ni limbukeni wa madaraka wasiojua ukomo wa madaraka yao.
Hujaelewa, hicho chuo cha madini kipo eneo lao la kazi means Kiko Tabora. Fikiria kukitokea uvunjifu wa amani na hao wachimbaji wadogo wadogo wataita FFU wa UDSM?
 
Nchi hii inashindwa kufika mahali ilipotakiwa kufika kwa sababu ya kuongozwa na watu wasiojitambua, wasiojua wajibu wao wala mipaka ya mamlaka yao.

Kuna habari zinazunguka mitandaoni kuwa eti DC wa Nzega ameamuru mkuu wa Chuo Cha Madini Nzega awekwe ndani kwa sababu alishindwa kumjibu mkuu wa Mkoa wa Tabora alipotembelea chuo hicho.

Kwanza, hawa viongozi, wote wawili ni dhahiri inaonekana hawana uelewa wa chochote kwenye mifumo ya utawala.

Chuo cha madini Nzega kipo chini ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam. Kama kuna matatizo kwenye branch hiyo ya UDSM, walitakiwa kuwasilidha malalamiko yao kwa mkuu wa Chuo Kikuu, UDSM, ambaye ni Rais Mstaafu Jakaya Kikwete au Vice Chancelor wake.

Bila shaka hawa viongozi ni wale malimbukeni wa madaraka. Kwa vile tu sheria inatamka kuwa wanaweza kutoa amri ya kumweka mtu ndani kwa muda usiozidi masaa 48, kwa ujinga wa kutojua mantiki ya sheria hiyo, wanaichukulia kumweka mtu ndani ni kama adhabu, wakati lengo la sheria hiyo lilikuwa kwa kuzingatia mazingira ya nyakati na mahali. Mathalani mtu anaonekana akiwa huru anaweza kuendelea kudhuru au kudhuriwa, na vyombo vya kisheria vya udhibiti havipo eneo la karibu, basi mkuu wa mkoa au wilaya, alipewa mamlaka hayo ili kipindi hicho akiwa ndani, kitumike kuwasiliana na mamlaka husika. Unajiuliza, huyo mkuu wa hiyo branch ya UDSM alikuwa anamdhuru nani hadi awekwe ndani, jibu linakuwa moja tu, kuwa huyo DC inaonekana ni empty kabisa kichwani kwa masuala ya utawala na sheria.

Rais anapoteua watu kwenye nafasi fulani, hasa kwa nchi iliyojaa machawa, rushwa na vyombo dhaifu vya vetting, inakuwa ni kubahatisha, lakini inapodhihirika, kama ilivyo kwa hawa watu, kuwa wateule ni watu duni kiutendaji, inatakiwa kuwafukuza mara moja kabla hawajaleta madhara makubwa zaidi.
Tuliza makalio hakuna unachojua, umeandika upupu. Huelewi ht RC ni nani. RC yuko kwa niaba ya Rais ktk eneo lake la utawala. Tuambie mipaka ya Rais? Anahitaji pongezi kubwa sana amani ingevunjika eneo lile ungeenda wewe? Ur empty headed
 
Kama wanaamini kuna kosa amefanya wanatakiwa kupeleka malalamiko yao kwa mwajiri wake, ambaye ni UDSM.


Ni lini uliwahi kusikia RC wa Dar au Dodoma, walienda UDSM au UDOM kuwafukuza wafanyakazi au kuwaweka ndani kwa sababu wameshindwa kutekeleza wajibu wao.

Huyo DC na RC, ni limbukeni wa madaraka wasiojua ukomo wa madaraka yao.
Rubbish
 
Naunga mkono hoja japo RC na DC wanawaklisha akili na tabia za viongozi wengi kwenye utawala wa CCM.

Viongozi wengi wakishakuwa viongozi basi wanaoamini kwenye kusujudiwa na utiifu na walisemalo na kutenda ndio Sheria na watu wote wanapaswa kufuata.

Kosa la yule jamaa ni kosa la kinidhamu, kuja kazini akiwa amelewa na kushindwa kutekeleza majukumu yake, ile amri waliyotoa imedhihisha ulimbukeni wao na kutojua nini maana ya uongozi, watu wale siku wakiwa na madaraka makubwa itakuwa ni hatari zaidi.
 
Sio kufukuza hao wawili tu inatakiwa wafukuzwe wote nchi nzima hizi nafasi zifutwe hazina tija yeyote
 
Back
Top Bottom