Rais Samia peleka fedha za kutosha TANAPA, NCAA & TAWA

Rais Samia peleka fedha za kutosha TANAPA, NCAA & TAWA

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Mh Rais Mama Samia nakusalimu kwa jina la JMT.

Naomba kukupongeza na kukushukuru namna unavyopigania kuinua UTALII kupitia ROYAL TOUR.Ni wazi tena pasipo shaka kwamba ROYAL TOUR inakwenda kusaidia kuongeza idadi ya watalii Tanzania.Hili ni jambo jema linastahili pongezi za dhadi kwakuwa idadi ya WATALII ikiongezeka maana yake fedha za kigeni zitaongezeka mara dufu,ajira zitaongezeka na kipato cha mwananchi mmoja mmoja kitaongezeka.

Baada ya jitihada zako binafsi na serekali yako,naomba kwa moyo wa dhati kukufahamisha hali ya kifedha katika hifadhi zetu ni mbaya sana.Hifadhi zetu zipo shughuli nyingi zinazohitaji fedha kama ujenzi wa madaraja,ukarabati wa barabara ambazo zinatakiwa kufanyiwa matengenezo mara kwa mara.Ununuzi wa Magari na mitambo,ununuzi wa spare parts,posho za maaskari kwaajili ya shughuli za ulinzi na nk.

Mambo yote yanahitaji fedha bahati mbaya kupitia Waziri wa fedha kipindi cha Rais Magufuli Bunge lilipitisha sheria ya kuchukua mapato yote ya taasisi za umma hasa TAWA,TANAPA & NCAA.Kinachotokea sana taasisi hizi zinatakiwa kuomba fedha kwaajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo HAZINA.Mara nyingi fedha zinazoombwa zinaletwa kidogo sana na wakati mwingine kwa kuchelewa.

Majangili wa wanayamapori wakifahamu kwamba sasa taasisi hizi zipo hoi kifedha maana yake utapatikana mwanya wa kuanza kuwinda wanyama pori wetu kwa speed kubwa na kupelekea wanyama wengi kupungua na wengine kutoweka.Jitihada zako kupitia ROYAL TOUR itakuwa kazi bure kwakuwa hifadhi zetu nyingi zitakuwa na upungufu mkubwa wa wanyamapori.

Kazi ya kulinda MAPORI & HIFADHI za wanyama si lelema,tukifanya makosa ya kukumbatia fedha pale HAZINA mambo mengi yataharibika na Serekali yako italaumiwa kwa kushindwa kulinda maliasili ya taifa.

Naomba kuwasilisha, Dr Ngongo kwasasa Tarangire National Park.
 
Siyo kipaumbele kwa sasa...

Kipindi cha Kikwete hali ilikuwa mbaya sana,niliwahi kutembelea Serengeti ilikuwa shida sana kuwaona Tembo au Simba.Kama hali itaendelea hivi tunaweza kurejea kule kule.
 
Usikurupuke kujibu,Mimi si muajiriwa wa hizi taasisi.Sijawahi kuajiriwa katika maisha yangu ndio maana sasa niko Tarangire nawashangaa wanyama na uumbaji wa Mungu wakati wewe upo Tandika hujui leo utakula nini?.
Ananilisha baba ako?
 
Wakati ule pesa inaanzia mikononi mwa hizo taasisi watu walitajirika kweli kweli, yaani tunaposema kutajirika uelewe, yaani tip hazikosekani asee, haya mambo kama upo nje au uelewi unaweza kudhani serikali ni wajinga.

Kuna watu wa hizo taasisi yaani walikuwa hawalali nyumbani per week analala weekend tu, but siku nyingine zote huyo site ahahahaaa, deals zilikuwa za kutosha, tours operators hawafiki ofisini ni juu kwa juu tu, nk.

Hii nchi hii ahahahaaa acha kabisa.
 
Mh Rais Mama Samia nakusalimu kwa jina la JMT.

Naomba kukupongeza na kukushukuru namna unavyopigania kuinua UTALII kupitia ROYAL TOUR.Ni wazi tena pasipo shaka kwamba ROYAL TOUR inakwenda kusaidia kuongeza idadi ya watalii Tanzania...
WATU WAMEKAA MKAO WA KUZISUBIRI WAZIPIGE ni kula bila Kuvimbiwa
1644468513817.jpg
 
Usikurupuke kujibu,Mimi si muajiriwa wa hizi taasisi.Sijawahi kuajiriwa katika maisha yangu ndio maana sasa niko Tarangire nawashangaa wanyama na uumbaji wa Mungu wakati wewe upo Tandika hujui leo utakula nini?.
Umelipia shilling ngapi kuingia huko ?
 
Kipindi cha Kikwete hali ilikuwa mbaya sana,niliwahi kutembelea Serengeti ilikuwa shida sana kuwaona Tembo au Simba.Kama hali itaendelea hivi tunaweza kurejea kule kule.
Kweli ?... Serengeti ina wanyama 'big 5' wengi mno, tena ni rahisi mno kuwaona.
 
Mkuu umeandika andiko zuri sana. Mimi nakuunga mkono. Ila pamoja na ushauri wako mzuri wengo lengo la kuongeza ufanisi wa kazi katika Taasisi hizi zilizopo chini ya Wizara ya Maliasili na Utalii, ikirudi kama enzi za nyuma upigaji utakuwa kwa kiwango cha juu sana. Mimi naona ni bora fedha iende Hazina moja kwa moja kama ilivo sasa.
La msingi hapa mimi naona ni kwamba Serikali kupitia Hazina wawe wepesi kutoa fedha pindi Taasisi hizi zinapotuma maombi yao. Serikali inachelewesha sana kutoa huo mgao wa hizo fedha.
Naomba nikupe mfano.
Halmashauri ambazo zipo karibu na mapori ya akiba ambapo ndani yake panafanyika Utalii wa Uwindaji, zimekuwa nzito sana kutoa ile 25% ya Gawio la Uwindaji toka TAWA. Ambapo unakuta TAWA wameingiza fedha katika account ya Halmashauri husika na risiti imetumwa na kupokelewa na kitengo chaWanyamapori. Kitengo cha Wanyamapori inabidi kiandike Dodoso kwa DED kuomba hio fedha ili 60% ipelekwe kwenye vijiji jirani na mapori ya akiba na 40% itumike kuimarisha kitengo cha Wanyamapori ndani ya Halmashauri. Lakini hio pesa mpaka itoke daah! Sijui hua kuna shida gani huko kwa ma-DED.
 
Mh Rais Mama Samia nakusalimu kwa jina la JMT.

Naomba kukupongeza na kukushukuru namna unavyopigania kuinua UTALII kupitia ROYAL TOUR.Ni wazi tena pasipo shaka kwamba ROYAL TOUR inakwenda kusaidia kuongeza idadi ya watalii Tanzania.Hili ni jambo jema linastahili pongezi za dhadi kwakuwa idadi ya WATALII ikiongezeka maana yake fedha za kigeni zitaongezeka mara dufu,ajira zitaongezeka na kipato cha mwananchi mmoja mmoja kitaongezeka.

Baada ya jitihada zako binafsi na serekali yako,naomba kwa moyo wa dhati kukufahamisha hali ya kifedha katika hifadhi zetu ni mbaya sana.Hifadhi zetu zipo shughuli nyingi zinazohitaji fedha kama ujenzi wa madaraja,ukarabati wa barabara ambazo zinatakiwa kufanyiwa matengenezo mara kwa mara.Ununuzi wa Magari na mitambo,ununuzi wa spare parts,posho za maaskari kwaajili ya shughuli za ulinzi na nk.

Mambo yote yanahitaji fedha bahati mbaya kupitia Waziri wa fedha kipindi cha Rais Magufuli Bunge lilipitisha sheria ya kuchukua mapato yote ya taasisi za umma hasa TAWA,TANAPA & NCAA.Kinachotokea sana taasisi hizi zinatakiwa kuomba fedha kwaajili ya matumizi ya kawaida na maendeleo HAZINA.Mara nyingi fedha zinazoombwa zinaletwa kidogo sana na wakati mwingine kwa kuchelewa.

Majangili wa wanayamapori wakifahamu kwamba sasa taasisi hizi zipo hoi kifedha maana yake utapatikana mwanya wa kuanza kuwinda wanyama pori wetu kwa speed kubwa na kupelekea wanyama wengi kupungua na wengine kutoweka.Jitihada zako kupitia ROYAL TOUR itakuwa kazi bure kwakuwa hifadhi zetu nyingi zitakuwa na upungufu mkubwa wa wanyamapori.

Kazi ya kulinda MAPORI & HIFADHI za wanyama si lelema,tukifanya makosa ya kukumbatia fedha pale HAZINA mambo mengi yataharibika na Serekali yako italaumiwa kwa kushindwa kulinda maliasili ya taifa.

Naomba kuwasilisha, Dr Ngongo kwasasa Tarangire National Park.
Mbali ya hayo ulio taja, kuna upungufu mkubwa wa askari. Waliopo wanafanyishwa kazi kwa muda mrefu bila mapumziko, bila malipo ya ziada. Kuna idara zinatakiwa kuwa kombania lakini unakuta section 2 (askari 18!) tu. Afya za askari wengi ni duni kwa kufanya kazi muda mrefu.
 
Back
Top Bottom