Rais Samia: Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa zaidi ya siku tatu

Rais Samia: Rais haruhusiwi kukaa mkoa mmoja kwa zaidi ya siku tatu

brazaj

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2016
Posts
31,698
Reaction score
41,733
Mabibi na mabwana mheshimiwa Rais wetu mpendwa mama Samia amepasua mbarika tena leo.

Akiongea na vijana Mwanza, mh. Rais katamka angependa kuendelea kukaa zaidi Mwanza, ila taratibu na sheria hazimruhusu kukaa zaidi ya siku 3 katika mkoa mmoja.

Bila shaka akimaanisha kukaa siku 3 mkoani nje ya ofisi rasmi za Magogoni au Chamwino:



Hizi sheria au taratibu ni mpya zilizoanza baada ya awamu ya sita kuingia ofisini au ndiyo ilivyo ila ilikuwa kupigana ma-changa ya macho?

Kumbukumbu zingali hai kwani si zamani tulipoaminishwa katika awamu ile kuwa rais anaweza kuweka kambi popote na kazi ikaendelea bila ukomo!

Kama aliyosema mama leo ndiyo ukweli wenyewe basi pongezi sana mama Samia kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria.

Unatudhihirishia kwa vitendo kuwa unayo nia ya dhati ya kuhakikisha kuwa kama tunavyowajibika sote kwa mujibu wa sheria wewe kama rais siyo exceptional.

Hongera sana mama Samia kwa kuzingatia utawala wa sheria kazi inapoendelea!
 
Paukwaa Pakawaaa!
Hapo zamani za kale kuna mtawala mmoja wa Tanzania alikuwa matata na Hamnazo kweli kweli! Mara nyingi alikuwa anakaa na kufanya kazi za kiserikali nyumbani kwao kule ndani ndani kulee kwa zaidi ya miezi kadhaa bila kujali hili wala lile...

Kwa ushamba wa asili; Hamnazo aliwaapisha watendaji wake na kuwapokea wageni mashuhuri kwenye mazingira ya kienyeji enyeji sana kule kwao! Alikuwa mjivuni na mdhalilishaji! Alipenda showoffs na media attentions. Alipenda yeye tu ndo aonekane akiwa fontipeji! Kila uzinduzi yeye! Mabango barabarani yeye peke yake!

Alitamani wananchi wawe wanyonge wa kudumu.
Watendaji wake walijifanya kumkubali. Wapo wafuasi waliojua udhaifu wake wa kupenda kuabudiwa. Mithili ya sinema za kijambazi; wafuasi wa Hamnazo walipora mali, waliua na kunyanyasa wote waliokuwa na mawazo mbadala.

Licha ya ulinzi wa kutosha aliojiwekea (unaoonekana na usioonekana) Hamnazo alifanikiwa kwenda zake kuzimu. Wengi walijitokeza kutaka kujiridhisha kama kweli Hamnazo kaenda zake. Maelezo yakawa mengi tofauti tofauti! Kwa kipindi kama mwezi hivi pengine zaidi baada ya shujaa Hamnazo kwenda zake kuzimu wafuasi wake bado hawakuamini kama kweli yule mtawala matata; shujaa wao angelienda zake kirahisi vile. Lakini ndo hivyo ilivyokuwa. Cha ajabu kuanzia aende zake hakuna tena aliyetaka kufuata nyendo zake ovu!
Hamnazo alisahaulika mapema sana.
Baada ya kuona hata mzimu wake nao haukuwa na jipya basi wateule wake wengi walipata mwanya wa kujivua u-hamnazo, kutua misalaba yao na kutema nyongo huku wakikiri wazi wazi kwamba Tanzania ilielekezwa njia ya kuzimu na yule mtukufu Hamnazo, shujaa wao.
Hadithi yangu imeishia hapo.

FUNDISHO: Tujenge taasisi imara na si miungu-watu. Akina Hamnazo hawajaisha! Asanteni
 
Hapo zamani za kale kuna mtawala matata wa Tanzania aliwahi kukaa na kufanya kazi kwa zaidi ya miezi kadhaa... Aliwaapisha watendaji wake na kuwapokea wageni nashuhuri kwenye mazingira ya kienyeji enyeji sana...

FB_IMG_1623760679727.jpg
 
Mabibi na mabwana mheshimiwa Rais wetu mpendwa mama Samia amepasua mbarika tena leo.

Akiongea na vijana Mwanza, mh. Rais katamka angependa kuendelea kukaa zaidi Mwanza, ila taratibu na sheria hazimruhusu kukaa zaidi ya siku 3 katika mkoa mmoja.

Bila shaka akimaanisha kukaa siku 3 mkoani nje ya ofisi rasmi za magogoni au chamwino.

Hizi sheria au taratibu ni mpya zilizoanza baada ya awamu ya sita kuingia ofisini au ndiyo ilivyo ila ilikuwa kupigana ma-changa ya macho?

Kumbukumbu zingali hai kwani si zamani tulipoaminishwa katika awamu ile kuwa rais anaweza kuweka kambi popote na kazi ikaendelea bila ukomo!

Kama aliyosema mama leo ndiyo ukweli wenyewe basi pongezi sana mama Samia kwa kuzingatia maadili, taratibu na sheria.

Unatudhihirishia kwa vitendo kuwa unauo nia ya dhati ya kuhakikisha kuwa wewe kama tunavyowajibika sote kwa mujibu wa sheria wewe kama rais siyo exceptional.

Hongera sana mama Samia Ku kuzingatia utawala wa sheria kazi inapoendelea!
Mmmm haya sisi yetu Macho tu

Sent from my Moto E (4) using JamiiForums mobile app
 
Hapo zamani za kale kuna mtawala matata wa Tanzania aliwahi kukaa na kufanya kazi kwa zaidi ya miezi kadhaa... Aliwaapisha watendaji wake na kuwapokea wageni nashuhuri kwenye mazingira ya kienyeji enyeji sana!
Na wote walijifanya kumkubali...
Alivyoenda zake kuzimu hakuna aliyetaka kufuata nyendo zake ovu!
Hadithi yangu imeishia hapo.
Fundisho: tujenge taasisi imara na si miungu-watu
Ndiyo maana Mungu alichoka na ujinga ule. Bila kumwondoa akina Sabaya mngeyajuaje maovu yao?
 
Back
Top Bottom