Rais Samia, ruhusu watu wanywe bia 24/7 ukuze uchumi

Rais Samia, ruhusu watu wanywe bia 24/7 ukuze uchumi

Thanks,walichukue hili wahusika.inashangaza unaingia bar ipo wazi unaagiza beer unaambiwa wanaogopa kuuza! Aisee
 
Mama, kabla ya 2015 watu walikuwa wanakunywa bia masaa yote. Pombe ni miongoni mwa vyanzo vikuu vya mapato vya nchi yetu pendwa.

Pombe inanywewa wakati wote, wakati wa misiba na wakati wa harusi, wakati wa furaha na wakati wa huzuni.

Pombe ni kiburudisho baada ya kazi. Kuna kazi mbalimbali nchini. Sio wote wanafanya kazi masaa ya asubuhi hadi jioni.

Wengine kazini huingia usiku na kutoka asubuhi, kwa katazo la watu hawa kunywa mchana tunakuwa hatuwatendei haki na nchi inapoteza kipato.

Hebu hili liangaliwe upya kwa ustawi mpana wa uchumi wa taifa letu.
Naunga mkono hoja

USSR
 
Back
Top Bottom