Kwa kawaida Rais anapozungumzia masuala yanayohusu jumuiya ya kimataifa anakuwa anazungumza kwa niaba ya sisi Watanzania kwa maana kuwa anaueleza Ulimwengu Tanzania inasema nini katika agenda inayojadiliwa. Ushauri wangu wa dhati kabisa ni kila mikutano hii mikubwa ambayo Rais wetu anategemewa kuzungumza kwa niaba yetu wote basi atumie hazina ya vipaji vyote vya Watanzania kuhusu somo hilo. Draft ya kwanza (zero draft) itokane na jopo la wataalam wa somo husika. (Ni jukumu mojawapo la Idara ya Utumishi kuwa na data bank ya wataalam mbali mbali waliobobea na wenye uzoefu wa taaluma mbali mbali).Wasaidizi wapendwa wa Rais na Rais mwenyewe watumie hiyo draft ya kwanza kuifinyanga hutoba kwa kuqeka lugha rafiki kwa msomaji, Rais wetu kama anavyotaka lakini substance ya jambo analoongelea itokane na wataalam wa kiwango cha juu kabisa. Uzoefu wa kawaida unaonesha hakuna mtaalam mwenye hekima ya wastani ambaye hawezi kuwa radhi kusaidia Rais wake afanye vizuri kwenye masuala ya heri kama haya. Tusitengeneze, kwa mfano, timu ya mpira ya taifa inayokwenda kwenye mashindano ya world cup inayotokana na ligi ya mpira kutoka daraja la tatu! Watanzania lazima tukubali kuwa kutumia uwezo na vipaji vyote tulivyonavyo ndiyo siri ya hao viongozi wenzetu ambao tunaona wanafanya vizuri!
Yote ni saw a kabisa. Lakini kwa kuongezea tu ni;
1. Waelewe lengo la ziara ni nini. Kama Rais anahudhuria mkutano au kongamano, at the first place wahusika watambue linahusu nini ili wamwandalie hotuba inayobeba maudhui ya kusanyiko hili...
Mf. Ukisikiliza hotuba hii ya Rais wetu, kuna eneo kataja Mlima Kilimanjaro lakini binafsi nimeshindwa kuelewa alitaka hadhira ipate picha gani kuhusu Mount Kilimanjaro in relationship to the global climate changes...
2. Ma Rais wetu waachane na hotuba za mfumo "full text" za kusoma mwanzo mwisho NENO KWA NENO, SENTENSI KWA SENTENSI na AYA KWA AYA. Zimepitwa na wakati na zinadumaza akili..
Badala yake awe na hotuba iliyo katika mtindo wa "mifupa" au "skeleton" na nyama unajaza mwenyewe in the process...
Huu ndiyo mtindo Wa hotuba za Rais wa kwanza wa Tanzania Hayati Mwl J. K. Nyerere...
ββ’ Aidha mtindo huu wa hotuba ndio unaovutia na kuvuta attention ya hadhira/watazamaji na ni kipimo cha uelewa na ufahamu wa mhutubiaji....
Ni mtindo unaotumiwa/uliotumiwa na watu wa aina ya Tundu Lissu, Mwl. J. K. Nyerere, Nelson Mandela, Martin Luther Jr, Rais wa sasa wa Zambia Hakainde Hichilema nk. Ni mtindo wa hotuba zenye kuvuta hisia na kuhamasisha watu kutenda na kushiriki....
ββ’ Aidha, ni kwa sbb ni mtindo unaohitaji watu wenye exposure na uelewa mpana wa past and prevailing current global issues na wanaojisumbua kutafuta maarifa na kujisomea kwa wingi kila wakati...
Nasikitika kusema hili kwa ndugu zangu wa CCM ya leo, kuwa mimi sioni mtu wa kariba hii huko...
Na sababu ni moja tu, wamechoka, wamebweteka, wanadhani wameshafika Kanaani, hawana cha kuwasumbua, akili zao zimelala usingizi wa pono na walishalewa madaraka...
Kilicho mbele yao kwa sasa ni kula na kunywa kujaza Marumbo yao hadi kusaza, baaaasi..
Hiki ndicho kinachomsumbua Rais wetu huyu Samia S. Hassan...
Kuna kila dalili kuwa, amekwenda Scotland kupiga "misele" tu na kutalii. Anadhani kila wakati ni Wa kufanya ROYOL TOUR tu...!!