Mama unakumbuka Serikali ya JK ilivyoyumba? Ilianza kuyumbishwa Bungeni. Genge ambalo halikuridhishwa na ushindi wa JK 2005 likaungana na genge la mtandao wa JK lililokasirika kwa kukosa vyeo vinono na kuanza kuiandama Serikali Bungeni. Walikuwa wajanja: Hawakuwa wanamtaja JK wala kumshambulia. Tena walikuwa wanamsifia kwa maneno ya kinafki lakini wakaanza na Waziri wake Mkuu Lowassa, wakaja wakapukutisha Mawaziri mmoja baada ya mwingine. Serikali ikapwaya.
Mama kuna watu ambao hadi leo hawajaamini wewe ni Rais. Mwanzoni walitaka kukuita wa mpito. Wengine wanasema huna Awamu yako. Wengine wakasema usirekebishe kitu chochote. Lakini umesimama na umejiimarisha. Sasa wanataka kukuingia kwa njia nyingine. Wanaenda kulekule walipomuendea JK.
Wabunge wengi wanakupenda na ukiwa unaangalia TV na kuona sura zao wanavyoosaidia Serikali yako unaona kabisa inatoka moyoni. Hata wanapokosoa unaona kabisa ni kwa nia ya kusaidia. Ila wapo wachache wanne au watano hivi tukiwa nao huku mitaani hawakusemi vizuri. Wengine rekodi zao zipo. Hata wakiipiga Serikali yako wanawasumbua media na hizi TV za mtandaoni wawaposti.
Bahati nzuri unawajua na jamii inawajua.
Wawili wanasema eti iundwe Kamati Teule ya Umeme kuihoji Serikali yako (bahati nzuri Bunge liliipuuza hoja hii ya kizandiki lakini Mama sisi tunapendekeza Kamati Teule kubali iundwe iangalie masuala yote ya umeme kwa miaka 10 iliyopita halafu tuone nani ataumbuka kwa hapa tulipo leo). Kwenye miaka mitano ya Marehemu hakuna aliyefungua mdomo kuhusu Kamati Teule ya Bunge (ya kuchunguza sakata la wavuvi ingefaa).
Kuna wanaokuona wewe ni dhafu: Mswahili, mwanamke. Hawa wanajua kabisa kwamba umerithi li-Gridi mkweche na mgao hujauleta wewe na wanajua kabisa hata CAG mwaka 2019 alitoa kwenye taarifa yake kwanini umeme unakatikakatika. Taarifa akaileta Bungeni na ikawa mali ya Bunge. Mama hawa watu wanajua wanachofanya kuhoji kilekile CAG wao alichokitoleq maelezo. Mama, wanaokupamba kabla ya kuishambulia Serikali yako au Mawaziri wako ni wale wale wanaokung’ong’a ukiwapa kisogo.
Mama shika fimbo. Kuna mambo umuige Marehemu. Yule alikuwa Chuma haswa hakukubali atenganishwe na Serikali yake na Wateule kisa tu kapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Kuna Waziri mmoja wa Marehemu hadi leo ana laana ya kuchoma mitumbwi na nyavu zetu sisi baadhi ambao tunavua na kutufilisi. Hadi CCM ikasema atolewe. Marehemu aligoma kwasababu alitaka kazi hiyo aifanye mwenyewe. Ndio heshima ya Rais na heshima ya Urais. Waziri huyo huyo akachukua rula na kupima samaki mmoja mmoja kwenye kantini ya Bunge. Wabunge wakaja juu hadi Spika akaja juu.
Marehemu akasimama kidete. Wewe ndio unateua Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na viongozi wengine. Siku ukikubali kelele zikuamulie nani anaweza kazi na nani hawezi kazi, utakuwa huna Serikali. Wewe ndio muamuzi wa mwisho wa nani anakufaa, nani hakufai; nani anakusaidia, nani hakusaidii. Vijana mle ndani ya Bunge wataanza kupigana vikumbo vya 2030 na itakuwa kila siku ni kutaka kukwamishana na mwishowe kukukwamisha. Tunasema Kazi Iendelee.
Mama kuna watu ambao hadi leo hawajaamini wewe ni Rais. Mwanzoni walitaka kukuita wa mpito. Wengine wanasema huna Awamu yako. Wengine wakasema usirekebishe kitu chochote. Lakini umesimama na umejiimarisha. Sasa wanataka kukuingia kwa njia nyingine. Wanaenda kulekule walipomuendea JK.
Wabunge wengi wanakupenda na ukiwa unaangalia TV na kuona sura zao wanavyoosaidia Serikali yako unaona kabisa inatoka moyoni. Hata wanapokosoa unaona kabisa ni kwa nia ya kusaidia. Ila wapo wachache wanne au watano hivi tukiwa nao huku mitaani hawakusemi vizuri. Wengine rekodi zao zipo. Hata wakiipiga Serikali yako wanawasumbua media na hizi TV za mtandaoni wawaposti.
Bahati nzuri unawajua na jamii inawajua.
Wawili wanasema eti iundwe Kamati Teule ya Umeme kuihoji Serikali yako (bahati nzuri Bunge liliipuuza hoja hii ya kizandiki lakini Mama sisi tunapendekeza Kamati Teule kubali iundwe iangalie masuala yote ya umeme kwa miaka 10 iliyopita halafu tuone nani ataumbuka kwa hapa tulipo leo). Kwenye miaka mitano ya Marehemu hakuna aliyefungua mdomo kuhusu Kamati Teule ya Bunge (ya kuchunguza sakata la wavuvi ingefaa).
Kuna wanaokuona wewe ni dhafu: Mswahili, mwanamke. Hawa wanajua kabisa kwamba umerithi li-Gridi mkweche na mgao hujauleta wewe na wanajua kabisa hata CAG mwaka 2019 alitoa kwenye taarifa yake kwanini umeme unakatikakatika. Taarifa akaileta Bungeni na ikawa mali ya Bunge. Mama hawa watu wanajua wanachofanya kuhoji kilekile CAG wao alichokitoleq maelezo. Mama, wanaokupamba kabla ya kuishambulia Serikali yako au Mawaziri wako ni wale wale wanaokung’ong’a ukiwapa kisogo.
Mama shika fimbo. Kuna mambo umuige Marehemu. Yule alikuwa Chuma haswa hakukubali atenganishwe na Serikali yake na Wateule kisa tu kapakwa mafuta kwa mgongo wa chupa. Kuna Waziri mmoja wa Marehemu hadi leo ana laana ya kuchoma mitumbwi na nyavu zetu sisi baadhi ambao tunavua na kutufilisi. Hadi CCM ikasema atolewe. Marehemu aligoma kwasababu alitaka kazi hiyo aifanye mwenyewe. Ndio heshima ya Rais na heshima ya Urais. Waziri huyo huyo akachukua rula na kupima samaki mmoja mmoja kwenye kantini ya Bunge. Wabunge wakaja juu hadi Spika akaja juu.
Marehemu akasimama kidete. Wewe ndio unateua Mawaziri, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Mikoa na viongozi wengine. Siku ukikubali kelele zikuamulie nani anaweza kazi na nani hawezi kazi, utakuwa huna Serikali. Wewe ndio muamuzi wa mwisho wa nani anakufaa, nani hakufai; nani anakusaidia, nani hakusaidii. Vijana mle ndani ya Bunge wataanza kupigana vikumbo vya 2030 na itakuwa kila siku ni kutaka kukwamishana na mwishowe kukukwamisha. Tunasema Kazi Iendelee.