Rais Samia: Sijawahi Kuua "Mtu" Bali Naua "Sisimizi" Walio Chimbuko la Nguvu Hasi ya Upinzani Dhidi ya Ccm na Serikali Yake

Rais Samia: Sijawahi Kuua "Mtu" Bali Naua "Sisimizi" Walio Chimbuko la Nguvu Hasi ya Upinzani Dhidi ya Ccm na Serikali Yake

Doctor Mama Amon

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2018
Posts
2,089
Reaction score
2,725


"Mkiambiwa kwamba Mwenyekiti wa CCM na Rais wenu Samia ni mwuaji waambie ni kweli bila hofu. Ninaua Sisimizi wenye nguvu hasi ya Upinzani dhidi ya serikali ya CCM, ninaua Sisimizi waletao umasikini, ninaua Sisimizi wenye mambo hasi ya kuturudisha nyuma kiuchumi, ninaua Sisimizi waletao giza lilinalotanda kwenye uso wa nchi yetu, kweli ninaua sisimizi lakini sijawahi kuua mtu. ” (paraphrased) - - Kauli ya Rais Samia, Songea, Ruvuma, 28 Sep 2024


Tarehe 28 Sep 2024, akiwa mjini Songea, mkoani Ruvuma, Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, alihutubia Mkutano Mkuu wa Umoja wa Wanawake (UWT) wa CCM na kusema maneno hayo hapo juu.

Tamko lake linakuja siku chache baada ya utekaji, utesaji na mauaji ya kikomandoo ya Mohamed Ally Kibao yaliyotekelezwa na wahusika waliobeba silaha za kijeshi kwa mujibu wa mashuhuda.

Ni tamko linalokuja wakati ambapo, kwa mujibu wa taarifa ya TLS, kuna orodha ya watu wapatao 80 ambao wametoweka na hawajulikani waliko, baadhi wakiwa wamechukuliwa na Wahusika waliojitambulisha kuwa ni mapolisi.

Ni katika mazingira haya Rais Samia ameamua kucheza na "unyumbulifu" wa maana ya neno "muuaji. "

Neno hili linaloweza kumaanisha muuaji wa mtu, muuaji wa Sisimizi, muuaji wa mende, muuaji wa umaskini na kadhalika.

Anatumia utata huu kuwahamisha wasikilizaji kutoka kwenye tuhuma kuu yaani tuhuma kwamba "Rais Samia ni muuaji wa watu wanwoikosoa Ccm na Serikali yake"

Hata hivyo hajafanikiwa. Mazingira tuliyomo leo yanaashiria wazi kuwa Rais Samia ametofautisha maneno "Sisimizi" na "watu" kama mkakati wake wa propaganda dhidi ya wakosaji wa serikali yake.

Ni kama ambavyo maneno "mende" na "watu" yalitofautishwa huko Rwanda miaka ya 1990 katika vurugu za kundi moja dhidi ya kundi jingine (mass violence) ili kufanikisha dhana ya "wao" dhidi "yetu"

Katika kanuni za propaganda mkakati huu unaitwa "dehumanisation".

Rafiki yangu mmoja anasema yafuatayo kuhusu kanuni hii:

"Perpetrators of mass violence often appear to deny the humanity of their victims. Theoretical treatments of this topic suggest such dehumanization facilitates violence by disengaging moral restraints against harming fellow humans"

Hivyo ni sahihi kuhitimisha kuwa Rais Samia alitumia neno Sisimizi kama silaha ya kipropaganda.

Na kwa kweli limebeba maana ambayo inamtia hatiani Rais Samia.

Na likiendelea kutumika katika mtazamo huo linaweza kuleta maafa makubwa sana hapa Tanzania.

Historia inaonyesha kuwa huko Rwanda Wahutu waliwaua Watusi kwa sababu walitumia mkakati wa dehumanisation kuwabatiza Watusi jina baya la MENDE.

Hivyo ikawa rahisi kwa wahutu kutekeleza mauaji ya halaiki ya Watusi kwa kuwa wauaji walijawa na ujasiri wa "HAPA TUKO TUNAUA MENDE TU"

Aidha Waarabu na Wazungu waliokuwa wachuuzi wa biashara ya watumwa weusi hapa Afrika waliwabatiza Wabantu majina mabaya kama vile "nyani", "sokwe," na "nguruwe" na kwa sababu hii ikawa rahisi kwao kuwapiga bei Waafrika hawa katika masoko ya watumwa kwa sababu ya ujasiri kwamba "HAWA NI NYANI TU."

Kwa sababu hizi namwalika Rais Samia na wasaidizi wake kujielekeza kwenye mada ya msingi kwa faida ya Taifa.

Na mada kuu ni hii hapa:

Je, nguvu ya hoja iliyo hasi dhidi ya madudu ya Ccm na Serikali yake inawafanya wakosoaji husika kupoteza hadhi ya utu wao hadi watekwe, wateswe, wasiginwe kama "Sisimizi" na hatimaye kuuliwa na milli yao kuharibiwa kwa kumwagiwa tindikali kama tukio la Mohamed Ally Kibao linavyothibitisha?

Je, kwa mujibu wa katiba ambayo SAMIA aliapa kulinda, ni halali kwa mtu yeyote kueneza itikadi, sera na mipango ya serikali kwa kutumia itikadi ya JAMBIA LA MTUME MOHAMED isemayo kuwa "kila mtu aliye kinyume chetu ni kafiri anayestahili adhabu ya kuchinjwa kwa upanga hadi kufa"?

Na je, kwa nini Samia na wasaidizi wake wanashindwa kuona kwamba sisi Waafrika tulipokubali kuwa na Rais Mwarabu tulikuwa tunajua ukweli kuwa mataifa yote ya kiarabu yanaikataa democracy na kukumbatia autocracy, lakini tukaamua kwamba tumpe, benefit of doubt, kwa kumkabidhi kamba ya urais ili ajinyonge mwenyewe, kama akitaka?

Kwa kukiri kwa mdomo wake kwamba yeye ni muuaji wa Sisimizi wanaomnyima usingizi tayari Rais Samia amekataa urais kwa maneno na matendo yake mwenyewe.

Ameamua kujinyonga mwenyewe kwa kamba hadi kufa!

RIP Samia Suluhu Hassan!

CCM mkimaliza matanga anzeni kuandaa mgombea irais mwingine!

Nakala kwa:

1. Mary Chatanda,
Mwenyekiti UWT Taifa,
Tanzania
(Aione kwenye faili)

2. Dk. Emanuel Nchimbi,
Katibu Mkuu CCM
(Aione kwenye faili)

1727668759154.png




View: https://youtu.be/qzZAu97hmUo
 
Tarehe 28 Sep 2024 Rais Samia amehutubia Mkutano Mkuu wa UWT na kusema maneno hayo hapo juu.

Tamko lake linakuja siku chache baada ya utekaji, utesaji na mauaji ya kikomandoo ya Mohamed Ally Kibao yaliyotekelezwa na wahusika waliobeba silaha za kijeshi kwa mujibu wa mashuhuda.

Ni tamko linalokuja wakati ambapo kuna orodha ya watu wapatao 80 ambao wametoweka na hawajulikani waliko, baadhi wakiwa wamechukuliwa na Wahusika waliojitambulisha kuwa ni mapolisi.

Rais Samia anacheza na "unyumbulifu" wa maana ya neno "muuaji" linaloweza kumaanisha muuaji wa mtu, muuaji wa Sisimizi, muuaji wa mende, muuaji wa umaskini na kadhalika ili kuwahamisha wasikilizaji kutoka kwenye tuhuma kuu yaani tuhuma kwamba "Rais Samia ni muuaji wa watu"

Lakini pia Rais Samia anasahau kuwa neno "Sisimizi" likitumika kama neno "mende" lilivyotumika huko Rwanda mwaka 1992 linaweza kuleta maafa makubwa sana hapa Tanzania.

Wahutu waliwaua Watusi kwa sababu waliwabatiza jina la MENDE.

Hivyo ikawa rahisi kwa wahutu kutekeleza mauaji ya halaiki ya Watusi kwa kuwa wauaji walijawa na ujasiri wa "HAPA TUKO TUNAUA MENDE TU"

Aidha wachuuzi wa biashara ya watumwa weusi waliwabatiza jina baya "nyani" na kwa sababu hii ikawa rahisi kuwauza Waafrika hawa katika soko la watumwa kwa sababu ya ujasiri kwamba "HAWA NI N6ANI TU."

Kwa sababu hizi namwalika Rais Samia kujielekeza kwenye mada ya msingi kwa faida ya Taifa.

Na mada kuu ni hii hapa:

Je, nguvu ya hoja iliyo hasi dhidi ya serikali ya CCM inawafanya wakosoaji husika kupoteza hadhi ya utu wao hadi watekwe, wateswe, kusiginwa kama "Sisimizi" na hatimaye kuuliwa na kumwagiwa tindikali kama tukio la Mohamed Ally Kibao linavyothibitisha?
Ney wa Mitego katika wimbo wake "Nitasema" amesema watavuna wanachopanda.
 
Kwa hiyo?
Watavuna wanachopanda.

Mwalimu Nyerere katika press conference yake ya Kilimanjaro Hotel ya mwaka 1995 aliongea sana kuhusu sifa za rais atakayetufaa.

Aliongea sana kuhusu, ukabila, udini, kujenga umoja wa kitaifa.

Inaonekana hawa viongozi wetu wa sasa hawajui au hawajali kujenga umoja wa kitaifa.

Rais ni mtu anayetakiwa kuliunganisha taifa, si kunyanyapaa wananchi kwamba hawa ni mende, na sisimizi tutawaua tu, askari wetu huwa hawakosi wakipiga risasi.

Samia hana uwezo wa uongozi, hana hulka ya kuunganisha watu.

Ana hulka ya kutoa hotuba za taarabu za mipasho, something unpresidential.

Yani kashindwa hata kuwa mfariji mkuu, watu wameuawa yeye anasema "kifo ni kifo tu". Tukisema tunamuua na yeye atasema ni sawa, kifo ni kifo tu?

Kashindwa hata kuwa na kauli nzuri, kitu ambacho hakihitaji pesa za kigeni wala za ndani.

Atavuna anachopanda.
 
Lakini pia Rais Samia anasahau kuwa neno "Sisimizi" likitumika kama neno "mende" lilivyotumika huko Rwanda mwaka 1992 linaweza kuleta maafa makubwa sana hapa Tanzania.
Hata Gadaffi alipoona wananchi wa Benghazi wanaamka na kuanza kuandamana kumpiga aliwaita Cockroaches (mende) na pia aliwaita rats (panya).

Samia ameitumia maneno hasi kubeza na kudogosha suala nyeti na zito la mauaji na utekaji.

2025, Samia must GO!
 
Kila analotamka mh rais haswa hivi karibuni kinakuwa negative !
Siwezi kujua ni sababu gani inampelekea kuzungumza lugha ngumu namna hii!
 
Tarehe 28 Sep 2024, akiwa mkoani Ruvuma, Rais Samia amehutubia Mkutano Mkuu wa UWT na kusema maneno hayo hapo juu.

Tamko lake linakuja siku chache baada ya utekaji, utesaji na mauaji ya kikomandoo ya Mohamed Ally Kibao yaliyotekelezwa na wahusika waliobeba silaha za kijeshi kwa mujibu wa mashuhuda.

Ni tamko linalokuja wakati ambapo, kwa mujibu wa taarifa ya TLS, kuna orodha ya watu wapatao 80 ambao wametoweka na hawajulikani waliko, baadhi wakiwa wamechukuliwa na Wahusika waliojitambulisha kuwa ni mapolisi.

Rais Samia anacheza na "unyumbulifu" wa maana ya neno "muuaji" linaloweza kumaanisha muuaji wa mtu, muuaji wa Sisimizi, muuaji wa mende, muuaji wa umaskini na kadhalika ili kuwahamisha wasikilizaji kutoka kwenye tuhuma kuu yaani tuhuma kwamba "Rais Samia ni muuaji wa watu"

Lakini pia Rais Samia anasahau kuwa neno "Sisimizi" likitumika kama neno "mende" lilivyotumika huko Rwanda mwaka 1992 linaweza kuleta maafa makubwa sana hapa Tanzania.

Wahutu waliwaua Watusi kwa sababu waliwabatiza jina la MENDE.

Hivyo ikawa rahisi kwa wahutu kutekeleza mauaji ya halaiki ya Watusi kwa kuwa wauaji walijawa na ujasiri wa "HAPA TUKO TUNAUA MENDE TU"

Aidha Waarabu na Wazungu waliokuwa wachuuzi wa biashara ya watumwa weusi waliwabatiza Wabantu majina mabaya kama vile "nyani", "sokwe," na "nguruwe" na kwa sababu hii ikawa rahisi kwao kuwapiga bei Waafrika hawa katika masoko ya watumwa kwa sababu ya ujasiri kwamba "HAWA NI NYANI TU."

Kwa sababu hizi namwalika Rais Samia na wasaidizi wake kujielekeza kwenye mada ya msingi kwa faida ya Taifa.

Na mada kuu ni hii hapa:

Je, nguvu ya hoja iliyo hasi dhidi ya serikali ya CCM inawafanya wakosoaji husika kupoteza hadhi ya utu wao hadi watekwe, wateswe, kusiginwa kama "Sisimizi" au "nyani" na hatimaye kuuliwa na kumwagiwa tindikali kama tukio la Mohamed Ally Kibao linavyothibitisha?

CC: Mary Chatanda, Mwenyekiti UWT Taifa.
Nadhani watu wataweka vizuri juu ya wanaouliwa ambao ni sisimizi.
 
Kila analotamka mh rais haswa hivi karibuni kinakuwa negative !
Siwezi kujua ni sababu gani inampelekea kuzungumza lugha ngumu namna hii!
Kile kisomo cha Tanga tayari kimejibu, na huu ni mwanzo tu.
 
Back
Top Bottom