Rais Samia, sio malaika ni binadamu anaweza kukosea. Tusimlaumu, kumshutumu na kumponda kwa makosa ya kukoseshwa. Tumvumilie tumpe muda

Hapa ishu ni katba tu
 
Ukimuuliza Bi Mkubwa hili, atakwambia anamuenzi JPM kama vile hapo awali yeye alivyowateua Jokate, Patrobas Katambi na Always Happi. Kwa kweli miaka hii mingapi sijui hadi tumpate Rais wa maana, tumepigwa sana!!!
 

Paskali bana, una ubendera fulani fuata upepo, hili neno kuwa hatukumpangia Magufuli huwa linasemwa humu mitandaoni, na ww ukalibeba kama lilivyo, kisha unalitumia katika kujenga hoja zako! Kwa taarifa kinachofanyika humu mitandaoni sio kumpangia rais, bali watu wanatoa mitazamo yao, hivyo ni juu ya rais kufuata ama kuacha. Huyo Magufuli mpaka anaingia kuzimu teuzi zake nyingi tulizipinga, ila alikuwa mtu wa kushupaza shingo. Labda uweke bandiko la hizo teuzi zake, tuone watu wakimsifia kwenye hicho unachoiita kutokupangiwa.
 
Mama kweli hapi kakosea kabisa, Mtu kama Nik wa Pili [emoji848][emoji848][emoji848]
 
Mibavicha ndio haina akili kabisa!

Mwanzo ilikuwa inamsifia sana! Alipofanya uteuzi wa kuwateua kina Nassari na Lijuakli ndio ikawa kama mbogo!

Nawaulizeni nyie mabavicha, hivi mlifikiri mama atafanya kwa matakwa yenu na si ccm?

Hamna cha ccm, kutokana na hii katiba mbovu, rais anafanya chochote atakacho kwa mapenzi yake, au ya genge la wale wanaomzunguka. Hiyo unayoita ccm inatumika tu kufanikisha agenda za walioshika mpini.
 
Acha utoto.....
jamaa akitoa maoni yake tu anatafuta teuzi!!!??
Wengine wanaposoma mtu anamwambia Paschal kuwa anatafuta teuzi na wao wanaiga kwa kufuata mkumbo tu. Wamejaa wa aina hiyo.

Kutafuta teuzi sio dhambi, ikiwa wanasiasa wakubwa wanatumia pesa nyingi kujenga mitandao ya marafiki ili siku moja waje kupata nafasi ya urais wa nchi kuna ubaya gani kwa mtu mmoja kuwa na ndoto za kuteuliwa kuwa mkuu wa mkoa au wilaya au kupewa cheo kingine kikubwa?. Bado humu JF kuna wenye kuendekeza utoto.
 
Kwakweli hawamtendei haki Mama, anajitahidi sana kazi anayoifanya sasa sio ya kubeza nafikiri sote tunaona jinsi kesi zinavyopanguliwa na mambo mengine kama hayo.

Tumpe muda na tumsaidie kwa kufanya kazi zetu kwa weledi.
Hakuna Rais anayechaguliwa kwa ajili ya kupangua makesi maswala ya kesi ni mfumo wa kisheria na kimahakama niambie tu toka ameingia ameshashugulikia mfumo wa kisheria na mahakama kuwe na haki hata siku akiwa amestaafu watu wasionewe?
 
DC anaripo asubuhi kesho anaondolewa, hovyo kabisa
 
Huku mtaani wanasema raisi anayeongoza nchi kwa sasa ni Mstaafu Kikwete eti Mama ni Bendera tu.
 
Paskali katika UBORA wako .....

Iko siku VETTING itakuona hata UDED....madini yamejaa kwako.....

#KaziInaendelea
 
Huku mtaani wanasema raisi anayeongoza nchi kwa sasa ni Mstaafu Kikwete eti Mama ni Bendera tu.
Labda mtaani/mitaani kwenu....

Huku mtaani kwetu wanasema nchi inaongozwa vyema na mh.Samia Suluhu Hassan!!!

#KaziIendelee
 
Nakuunga mkono ndugu yangu Paschal Mayalla watu waache kuongea ongea kusema wakubwa wa nchi hii haipendezi kabixa
 
Sawa kwa kuwa Magufuli hakuwa binadamu hakupaswa kukosea wala kusamehewa.

Upuuzi tu kila pahala ni mizengwe mwanzo mwisho.

Sent from my PIC-LX9 using JamiiForums mobile app
 
Anybody can get it!

Nilimsema sana Magufuli kuhusu Makonda.

Nitamsema Samia pia.

She shouldn’t be mollycoddled just because she’s a woman.

No way! No how!


 

Kuna madalali wa hizi teuzi , wakiambiwa watafute watu ni ulaji kwao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…