Rais Samia sio mzalendo kwao!

Rais Samia sio mzalendo kwao!

tpaul

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2008
Posts
24,225
Reaction score
22,632
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi pasipo kuwachosha. Rais Dr Samia atajaribu kumuiga Magufuli lakini kamwe hataweza asilani hadi anaondoka madarakani. Wakati Dr Magufuli akiwa Rais aliusaidia sana mkoa wake wa Chato kimaendeleo na kiuchumi. Hili halihitaji utafiti kwani liko wazi kwa kila Mtanzania mwenye akili zilizotimia.

Baada ya Dr Samia kushika madaraka anajaribu kufuata nyayo za Magufuli lakini ameshindwa kuzifuata sawasawa. Tukumbuke Magufuli alipeleka Chato mbuga ya wanyama, uwanja wa ndege wa kimataifa, hospitali ya kanda, mabenki, ujenzi wa vivuko vya majini, ujenzi wa barabara kila kona ya Chato na mambo mengine kadha wa kadha. Mtu kwao.

Sasa wewe fikiria Magufuli kapeleka kwao mambo yote haya halafu Dr Samia (chifu Hangaya) yeye anapeleka akademi ya mpira na matamasha ya “Usiku wa mama Samia”. Hivi huyu Rais kweli ana uzalendo wa kutosha kwa watu wa Kizimkazi kama Magufuli alivyokuwa serious na Chato? Mimi tpaul nasema huyu mama hana uzalendo na mahali alipotoka.

Hafai kwa kula wala kwa kulumangia. Hivi anawaonaje au anawachukuliaje watu wa Kizimkazi kwa kuwapelekea matamasha na viwanja vya mpira wakati wazanzibar mambo ya mpira sio kipaumbele chao?

1693459586518.jpeg


Mama aliwahi kusema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Iweje leo aende tofauti na Magufuli kama sio kukengeuka? Inasikitisha sana. Mtu kuwa pamoja na mtu sharti uwaji huo wa pamoja uhusishe matendo sio maneno matupu ambayo hayawezi kuvunja mfupa. Tafadhali sana Dr Rais Samia nakuomba uwaheshimishe wanaKizimkazi kama Magufuli alivyowaheshimisha wanaChato. Mdharau kwao ni mtumwa. Usiwe mtumwa Tanganyika ukasahau kwenu Zanzibar.

Nawasilisha.
 
MWALIMU NYEREREANAMALIZA KWA USHAIRI KWENYE KITABU CHAKE.

UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.

Ole wake Tanzania Tusipoisaidia
Niwezalo nimelifanya kushauri na kuonya nimeonya.

tahadhali nimetoa ushauri na kuonya nimeshatoka kitini zaidi nifanye nini.

Namlilia Jaalia atumulikie njia Tanzania ailinde WAOVU wasiishinde.


UONGOZI WETU NA HATMA YA TANZANIA.
MWALIMU JK NYERERE.
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi pasipo kuwachosha. Rais Dr Samia atajaribu kumuiga Magufuli lakini kamwe hataweza asilani hadi anaondoka madarakani. Wakati Dr Magufuli akiwa Rais aliusaidia sana mkoa wake wa Chato kimaendeleo na kiuchumi. Hili halihitaji utafiti kwani liko wazi kwa kila mtanzania mwenye akili zilizotimia.


Nawasilisha.
Duuh🙄
Kwa hiyo unataka akajenge international airport kijijini Kizimkazi?
Halafu gharama ziwe juu ya nani, Zanzibar au Tanganyika?
Huo siyo ufisadi wa fedha za walipakodi?
1693461103474.png
 
Duuh🙄
Kwa hiyo unataka akajenge international airport kijijini Kizimkazi?
Halafu gharama ziwe juu ya nani, Zanzibar au Tanganyika?
Huo siyo ufisadi wa fedha za walipakodi?
View attachment 2734248
Acha double standard mkuu. Magufuli alipojenga Chato alitumia hela za nani? Mama alitakiwa achague mradi uliochangamka sio mradi wa maviwanja ya michezo ambayo hayana tija yoyote kwa wanaKizimkazi. Wewe unaona kafanya sawa?
 
Naingia kwenye mada moja kwa moja na kwa ufupi pasipo kuwachosha. Rais Dr Samia atajaribu kumuiga Magufuli lakini kamwe hataweza asilani hadi anaondoka madarakani. Wakati Dr Magufuli akiwa Rais aliusaidia sana mkoa wake wa Chato kimaendeleo na kiuchumi. Hili halihitaji utafiti kwani liko wazi kwa kila Mtanzania mwenye akili zilizotimia.

Baada ya Dr Samia kushika madaraka anajaribu kufuata nyayo za Magufuli lakini ameshindwa kuzifuata sawasawa. Tukumbuke Magufuli alipeleka Chato mbuga ya wanyama, uwanja wa ndege wa kimataifa, hospitali ya kanda, mabenki, ujenzi wa vivuko vya majini, ujenzi wa barabara kila kona ya Chato na mambo mengine kadha wa kadha. Mtu kwao.

Sasa wewe fikiria Magufuli kapeleka kwao mambo yote haya halafu Dr Samia (chifu Hangaya) yeye anapeleka akademi ya mpira na matamasha ya “Usiku wa mama Samia”. Hivi huyu Rais kweli ana uzalendo wa kutosha kwa watu wa Kizimkazi kama Magufuli alivyokuwa serious na Chato? Mimi tpaul nasema huyu mama hana uzalendo na mahali alipotoka.

Hafai kwa kula wala kwa kulumangia. Hivi anawaonaje au anawachukuliaje watu wa Kizimkazi kwa kuwapelekea matamasha na viwanja vya mpira wakati wazanzibar mambo ya mpira sio kipaumbele chao?

View attachment 2734237

Mama aliwahi kusema yeye na Magufuli ni kitu kimoja. Iweje leo aende tofauti na Magufuli kama sio kukengeuka? Inasikitisha sana. Mtu kuwa pamoja na mtu sharti uwaji huo wa pamoja uhusishe matendo sio maneno matupu ambayo hayawezi kuvunja mfupa. Tafadhali sana Dr Rais Samia nakuomba uwaheshimishe wanaKizimkazi kama Magufuli alivyowaheshimisha wanaChato. Mdharau kwao ni mtumwa. Usiwe mtumwa Tanganyika ukasahau kwenu Zanzibar.

Nawasilisha.
Wewe umeona hayo tu?? Fanya utafiti Tena. Kazi hujaimaliza. Ana uzalendo kwao balaa
 
What’s the real point here? Kama taifa tunapata thamani gani kuwa na viongozi wanaohamishia kwao rasilimali za taifa bila kufuata mipango ya kitaifa iliyoidhinishwa na bunge?
 
What’s the real point here? Kama taifa tunapata thamani gani kuwa na viongozi wanaohamishia kwao rasilimali za taifa bila kufuata mipango ya kitaifa iliyoidhinishwa na bunge?
The point is: Mdharau kwao ni mtumwa. Na point nyingine ni kwamba usijenge kwa jirani huku kwako kunaporomoka. Anzia kwako kwanza.
 
Tafadhali sana Dr Rais Samia nakuomba uwaheshimishe wanaKizimkazi kama Magufuli alivyowaheshimisha wanaChato. Mdharau kwao ni mtumwa. Usiwe mtumwa Tanganyika ukasahau kwenu Zanzibar.

Nawasilisha.
Naunga mkono hoja,
P
 
Back
Top Bottom