Rais Samia Suluhu aitaka Wizara ya Habari kuvifungulia Vyombo vya Habari vilivyofungiwa. Avitaka kufuata Sheria na Kanuni

Duuu hii nimeipenda ntaamia ccm nisifu nakuabudu kama nikiliona gazeti langu tena Tz Daima aaaaaaaah mama kumi tena aaaaaah kudadadeki oyoooopp aaaaah Mataga Keisha habari yao.
Mkuu unakosea kuwatamka hao...

Wanaitwa mataga chato sukuma mafiaso gang !!
 
Biashara
mabenki
Magazeti
Viwanda
Sekta binafsi hoi
Mazao ya biashara
Korosho
Kahawa
Chai
Pamba
Wawekezaji
Chadema
Act wazalendo
Cuf(maalim?)
Ajira mpya
Vyeo/madaraja kazini
Mishahara kwa miaka 5,
Kusomesha imekua taabu
Afya,huna pesa hugomboi mwili!
Mtaani hapafai

Mungu akubariki mama hebu tuokoe kumbe ulikua unaona!
 
Mlisema upinzani umekufa na kuzikwa baada ya uchaguzi feki mwaka jana! Utazikwa mara ngapi tena?
 
Shikamoo mama!
Yale madudu ya mwendazake najua ulikuwa unapinga na yeye anakukaripia, sasa tekeleza mema , bado hujazungumzia mahakama na watu waliwekwa ndaninkwa kusingiziwa,wachiwe na kesi zifutwe.
 

Hili haliwezi kuwa zuri sana iwapo sheria zote kandamizi ile ya magazeti ya toka enzi za ukoloni na zile zilizopitishwa kwa wingi kati ya 2016 na 2020 zitabaki kama zilivyo....

Atakuwa shujaa atakayekumbukwa sana kama kauli yake hii itaenda sambamba na kuagiza marekebisho au kufutwa kwa baadhi...

Hata hivyo, tumpongeze ingalau kwa mwanzo huu, tuendelee kutoa maoni yetu, yanawezwa kufanyiwa kazi..
 
wadau hapa anamainisha nini.hata zile luninga ambazo zilikuwa hazionekani kwenye ving'amuzi vya ZUKU mfano ITV,STAR TV nk.au anazungumzia hivi vi online tv?
 
Ni siku ya 20 leo tangu aapishwe kuwa Raisi.

Hata awamu ya 5 ilianza na MANENO then baada ya hapo ikafuata sheria.

Tumpe muda. mtoto huanza kwa kukaa, kutambaa, kusimama then ndio hutembea.
 
Huyu mama tangu siku ya kwanza nilijua tu atakuja kuiharibu nchi.
Mimi nashangaa! Hivi Rais wetu mpendwa anamaanisha vyombo hivyo vya habari vilionewa! Ati vilifungiwa bila kufuata sheria kweli? Sasa anaposema vifunguliwe vifuate sheria, na hizo sheria zieleweke, kwani Mwanzo walipofungiwa hizo sheria zilikuwa hazieleweki? Kutofahamu sheria si utetezi wa kukuondolea kosa.

Kwa hivyo Rais wetu, anamaanisha kama hivi vyombo vilionewa tu kufungiwa bila kuvunja sheria basi vinauwezo kwenda mahakamani, kuishitaki serikali kudai fidia. Make vimepoteza fedha nyingi ambazo vingepata wakati vimefungiwa kwa kuonewa.
Ushauri wangu, mama awe makini asitake cheap popularity, uwezi sema unafungulia vyombo ili wasiseme kuwa mnafunguia uhuru wa habari.
Rais wetu anamuogopa nani? Huyu atakae sema! Kumbe tuna Rais muoga, anaogopa kusemwa.....! Mmmmh! Yangu macho......!

Rais wetu kumbuka uwezi kumpendezesha kila mtu. Usiogope kusemwa, wewe ni Amiri Jeshi Mkuu.
Hata hawa wanao kusifia, subiri watakusema tu. Rais Kikwete (Mstaafu) Aliwapa uhuru, lakini huyo huyo walimtukana, hadi kumwita ni Dhaifu.
Duniani uwezi ridhisha kila mtu.
Rais wetu chapa kazi, usifanye maamuzi kisha unataka fulani acheke, akuone weye mzuri. Kuwa makini na angalia sheria za nchi zinasemaje.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…