Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Mtego Mkubwa sana Mei Mosi hii ya mwaka 2021

Rais Samia Suluhu Hassan kwenye Mtego Mkubwa sana Mei Mosi hii ya mwaka 2021

NewPage

JF-Expert Member
Joined
Mar 22, 2021
Posts
1,321
Reaction score
2,106
Kwanza kabisa haijajulikana kama Sherehe hizi yeye ndiye atakuwa mgeni Rasmi au nayo itapita kimya kimya kama ilivyokuwa jana Sherehe za Muungano kwa sababu ya kuomboleza Msiba Mkubwa wa Jiwe.

Rais Samia ameamua kutojitenganisha na Hayati JPM - Mpango Kazi wa Mwaka 2020-2021 umejadiliwa lakini hakuna dalili kabisa kama kutakuwa na nyongeza ya mshahara. Rais Samia kaanza vizuri na hata kutamka kuwa kutakuwa na nyongeza ya mshahara. Wafanyakazi wanasubiri - hata hivyo mijadala ya bungeni na Serikali ilivyojionesha katika Mpango kazi ni hamna kabisa suala la kupanda mishahara. Hii ni ajabu ingine ambayo Rais Samia anataka kuionesha na kuonesha wazi wazi kuwa atakuwa anapelekeshwa na Spika Ndugai.

Spika Ndugai ni mjanja sana - anaenda kumtumbukiza Samia kwenye shimo - chuki kwa Samia itaanzia Mei Mosi. Ilipaswa kabisa baada ya Samia kuchukua URais asimamishe ule Mpango wa Serikali aupitie upya kwa kutumia wateuzi wake na kisha ndiyo upelekwe bungeni - yeye inavyoonekana ni kama amaeamua uende ulivyo. Huu Mpango Kazi na Mwelekeo wa Bajeti sio wa Samia ni wa Mtangulizi wake.

Kwa nini hakuufanyia hata review kidogo tu - Mwaka jana JPM alishusha kodi kwenye mishahara angalau kwa asilimia moja (1) lakini Mwaka huu baada ya kuwa ameshashinda Uchaguzi hicho hakikuwekwa kabisa. Yaani ni balaaa! Mama Samia hivi kwa nini umewaacha hawa watu kama akina Ndumbaro wa Utumishi na Msaidizi wake - huyu Waziri wa Utumishi naye kaingia lakini halioni hili kabisa.

Ninashangaa sana Bajeti za Wizara zinaendelea kujadiliwa zikiwa hazina kabisa projection ya nyongeza za mishahara - hivi kwa nini mnataka kumwangamiza huyu Mama kwa kuanza kuchukiwa mapema mapema hivi. JPM alikuwa anasema atakuja kufanya nyongeza kubwa - hamna kitu kama hicho duniani. Nyongeza kubwa ya mshahahara - say zaidi ya asilimia 50 huashiria kudorora kwa uchumi. Nyongeza hupaswa kwa wafanyakazi waliopo kwenye nchi wanazolipwa vizuri huwa haizidi asilimia sita (6%). JPM alichokuwa anasubiriwa kukifanya kama kweli ingekuwa ni kudororesha uchumi wa Tanzania zaidi au kuendeleza uwongo wa waziwazi na huku akitumia ubabe na ukandamizaji kutuongoza.

Rais Samia tafadhali achana na akina Ndugai - Ndugai atakuangusha - kundi lake la kutumia ubabe - yaani ile Sukuma Gang ipo na imeanza kushamiri zaidi. Mama pls pls jitenge na Ndugai. Huyu staili ya uongozi wake ni hiyo ya kibabe. Fikiria tu wewe kwa makini inakuwaje mpaka leo akina Halima Mdee na Kampani yake bado wapo bungeni?

Huo ndiyo mtihani wako wa kwanza - ulipaswa uanzie hapo - elekeza mbunge wako aanzishe hoja ya kutokuwa na Imani na Spika Ndugai kwa kulazimisha Halima and Gang kuwa wabunge. Ikibidi unda Tume ya kufanya uchunguzi kwa jambo hili. Una mamlaka hayo Rais wangu. JPM alijisahau sana na kakuzingatia misingi ya demokrasia hata kdg - ndiyo maana watu hawaogopi hata kumpa jina la Mwendazake - na ni kweli kabisa aende zake kule! Wewe jitofautishe na hawa watu - kama usipofanya hivyo kwa kweli hata hizi chokochoko za kutaka uongoze mara moja zitakuwepo sana.

Kwa kuanza hebu toa maelekezo ya nyongeza hata asilimia mbili tu kwa watumishi hawa waliosota miaka sita (just 2%) uone morari ya kazi na nchi itavyochangamka. Huwezi kuwatenganisha watumishi hawa na wananchi waliokuwa wakisemwa na JPM kuwa ni wanyonge au walalahoi. Kumbuka familia zetu WaTanzania ni extended so tupo nao humo humo. Usifuate kinachojadiliwa bungeni ni haramu kabisa. Hilo ni limpango la JPM na wewe sio JPM hata ukitaka kujing'ang'aniza hivyo wewe si yeye - kwa hili mwache ameshaenda zake pls!

NB. Kwa kushauri zaidi Hayati Magufuli alikuwa kabla ya Mei Mosi anakutana na viongozi wa wafanyakazi wanaweka mambo sawa - JPM alifanya hivyo miaka yake mitatu ya mwanzo akawaacha wafanye watakalo. Wewe pia unataka kufanya hivyo hivyo kutoitisha vikao na vyama kujadili maslahi yao. Viongozi wa vyama nao siku hizi wamejaa hofu tu utafikiri JPM bado yupo hawasemi hata tu kupongeza ahadi yako ya kuongeza mshahara. Wanapimia tu kwa sababu walishanunuliwa na JPM - sisi tunawaangalia tu - mwaka huu hasira zimetufika shingoni.

Hayati Magufuli alitudharau sana - sina shaka wewe angalau utaleta nafuu. Kuwa makini na Bunge! (tena sio bunge lote - ni wale Sukuma Gang tu). Mahakama umeshamaliza kazi - tayari kuna mabadiliko makubwa - hata Jaji Kiongozi Feleshi tayari kishatoa mwelekeo wa utendaji haki Mahakamani.
 
Na mwaka huu wasiponipandisha tena daraja, mapambano yatendelea mpaka kieleweke. Hakuna namna. Ni lazima wote tuonje keki ya Taifa.

Haiwezekani wachache tu wafaidi, huku wengi tukitaabika kwa mishahara kiduchu.
 
Kuhusu Maslahi ya Watumishi Mama ameshasema lazima ayafanyie kazi, kikubwa tumpe nafasi atimize ahadi zake kwa Wakati na muda ukiwadia basi tumuongeze Mi5 tena!.
Ni kweli lakini mbona bungeni hawajabadili zile bajeti za wizara kuonesha nyongeza za mishahaa kama ilivyo kawaida?
 
Ni kweli lakini mbona bungeni hawajabadili zile bajeti za wizara kuonesha nyongeza za mishahaa kama ilivyo kawaida?
Wala usiwe na shaka coz Mchakato wa Bajeti ulianza kitambo kidogo, Bungeni ulipelekwa kwa ajili ya kujadiliwa na kupata idhini tu!
By then kukiwa na uhitaji wa Jambo jipya upo utaratibu wa kufuata pia!!!
 
Wala usiwe na shaka coz Mchakato wa Bajeti ulianza kitambo kidogo, Bungeni ulipelekwa kwa ajili ya kujadiliwa na kupata idhini tu!
By then kukiwa na uhitaji wa Jambo jipya upo utaratibu wa kufuata pia!!!
Sawa sawa - lia basi ili kuonesha hilo ni sawa basi akina Ndugai na Timu yake angalau watamke kuwa Bunge linaangalia uwezekano wa kutekeleza mtazamo wa mama wa kuongeza salary!
 
JPM kafariki mwezi wa Tatu bajeti ilishaandaliwa bado kusomwa tu,kama kuna ongezeko jua lilishapata baraka ya JPM na kama hakuna jua bado watumishi waendelee kufunga mkanda labda mwakani kwa bajeti itakayomuhusu Mama kifupi hana ujanja wa kubadili chochote labda posho mbalimbali za watumishi upandaji wa madaraja anaweza kinyume na hapo sahau.
 
JPM kafariki mwezi wa Tatu bajeti ilishaandaliwa bado kusomwa tu,kama kuna ongezeko jua lilishapata baraka ya JPM na kama hakuna jua bado watumishi waendelee kufunga mkanda labda mwakani kwa bajeti itakayomuhusu Mama kifupi hana ujanja wa kubadili chochote labda posho mbalimbali za watumishi upandaji wa madaraja anaweza kinyume na hapo sahau.
Unachosema ni kweli na ndiyo kisichotakiwa kwa sababu ile ilikuwa awamu ya tano - ya mama ni awamu ya sita. Utofauti lazima uwepo!
 
Ndugu Wana JF,Kuna nyuzi zimo humuhumu zikimuonya Raisi mpya juu ya kipindi hiki Cha mpito.Nadhani hata wasaidizi wake wamezisoma na kushauri ipasavyo.no further comment.
 
Yani wafanye wafanyavyo iwe mwaka huu huku wakijua huku makazini sisi "watumwa" wao tumebakiza hatua chache sana kuwa "misukule". Wacha kazi iendelee...
 
Tumpe muda mama aweke sawa serikali yake.
Wengi wa Wakuu wa Idara waliwekwa na Rais wa awamu ya Tano kwa lengo moja tu la kuwagandamiza wale wa chini ?

Ndio maana yule wa awamu ya tano aliweka watu wake wa Karibu au wa Nyumbani au wa ukanda wake au aliosoma nao japo alijua wazi kuwa ameacha vichwa Vingi vyenye uwezo mkubwa pembeni.
Ulikua ni mkakati maalum wa kuminya maslahi ,Uhuru haki na demokrasia ya watu .

Watu walikua wanapewa ulaji mkubwa sana alimradi wahakikishe walioko Chini hawafurukuti kabisa kuanzia kwenye serikali mpaka mtaani.
Kama Profesa wa Chuo Kikuu Msomi aliyebobea kwenye sheria anashiba na kulewa baada ya kutunukiwa ubunge na uwaziri kisha anawaona wenzake waliobaki Kufundisha kuwa bado wapo Jalalani ,unategemea nini hapo kwenye tofauti ya kimaslahi ?

Tumwache Mama yetu apangue kabisa uozo uliokuwepo wa kula nchi kwa watu wa Chache.


Mama Samia kwa kweli anatakiwa kwanza kabisa awapige chini wateule wote walioteuliwa na Mtangulizi wake kisha ateue kwa masharti mapya yanayoendana na hali ya nchi yetu.
Punguza mishahara yote ya wateuzi kwa 40% kisha ongeza wafanyakazi 4%.
Majeshi yote ongeza posho zao kwa kupunguza mishahara ya wateule wote asiyetaka akae pembeni.


Tumshauri mama yetu namna bora ya kuanza na sio kumtwisha dhambi za mtangulizi wake alizofanya.
 
watumishi wameonyesha uvumilivu wa hali ya juu kwa kipindi kirefu, ni wakati wao sasa kufutwa machozi, kwa kufanya hivyo Taifa litapata neema na baraka tele.
 
Na mwaka huu wasiponipandisha tena daraja, mapambano yatendelea mpaka kieleweke. Hakuna namna. Ni lazima wote tuonje keki ya Taifa.

Haiwezekani wachache tu wafaidi, huku wengi tukitaabika kwa mishahara kiduchu.
Yule shangazi yako kule kijijini ambae hata mlo mmoja hapati,yeye unataka abaki hivyo hivyo milele?Angalau wewe tayari unapata mlo mmoja.Ngoja shangazi yako naye tumuwekee miundo mbinu ya kupata mlo mmoja,usijifikirie wewe tu.Huo ni ubinafsi.

Na hayo mapambano unayo ongelea ni mapambano gani kwanza.Hayo mbona yapo miaka mingi na tunajua yanafanywa na mapandikizi ya mabeberu.Hayo hayatakoma,hata mishahara ikiongezwa.Unachofanya wewe kipya ni kuzidisha mgongano huo na serikali na kuuhalalisha.Naweza kuiita hii AN INSTIGATION TO REVOLT AGAINST A LEGIMATELY ELECTED GOVERNMENT.
 
Back
Top Bottom