Rais Samia Suluhu Hassan sikiliza kilio cha wengi, Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu

Rais Samia Suluhu Hassan sikiliza kilio cha wengi, Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu

Sijakataa Samia kuwa na watendaji wake, tatizo ni pale anapoendelea kuwakumbatia hata wale waliofeli, kwa kufanya hivyo anajifelisha yeye binafsi kwa kuonekana dhaifu, na serikali anayoiongoza.

Kuhusu bei ya umeme kutoka 27,000/= mpaka 320,000/=, pia sina tatizo nalo, tatizo lililopo ni Samia binafsi wakati ule wa Magufuli kutuambia 27,000/= ingetosha kutuunganishia umeme, lakini ajabu baada ya Magufuli kuondoka, Samia akaikataa 27,000/= kwa kusema ilikuwa bei ya kisiasa.

Huyu alitudanganya.
Kwa ufupi Rais Samia ni bonge la Muongo na mnafiki, najua watu wanamvumilia sana
 
Sijakataa Samia kuwa na watendaji wake, tatizo ni pale anapoendelea kuwakumbatia hata wale waliofeli, kwa kufanya hivyo anajifelisha yeye binafsi kwa kuonekana dhaifu, na serikali anayoiongoza.

Kuhusu bei ya umeme kutoka 27,000/= mpaka 320,000/=, pia sina tatizo nalo, tatizo lililopo ni Samia binafsi wakati ule wa Magufuli kutuambia 27,000/= ingetosha kutuunganishia umeme, lakini ajabu baada ya Magufuli kuondoka, Samia akaikataa 27,000/= kwa kusema ilikuwa bei ya kisiasa.

Huyu alitudanganya.
Mkuu kwanza nikupongeze kwa ku argue kwa hoja vizuri kabisa. Usemayo ni kweli kabisa. Lakini nawewe si unafahamu kuwa makamu ni mshauri tu kulingana na katiba yetu? Kumbuka rais hashurutishwi kupokea ushauri kutoka kwa yeyote yule. Hata kama Samia hakukubaliana naye, angefanyaje?.
 
Samia alijitengenezea tatizo mwenyewe bila kujua, sasa hilo tatizo alilojitengenezea ndio linaanza kumtafuna, amesababisha aonekane anawakilisha kikundi cha mafisadi wachache wanaoitafuna nchi kwa dharau.

Alipoingia madarakani akaanza kuwaondoa waliokuwa watendaji wa Magufuli, huku akiwarudisha wale waliotemwa na Magufuli. Sidhani kama alipata muda wa kutosha kujua sababu zilizomfanya Magufuli awatose kwenye serikali yake.

Binafsi, naona aliamua kufanya vile akiamini atakuwa salama kwa kuzungukwa na kundi la marafiki zake, au watoto wao, akasahau baadhi ya hao wana kashfa zinazowazonga muda wote, huku utendaji wao ukiwa mbovu.

Sasa ameanza kuvuna alichopanda, ameanza kazi ya kuwaombea msamaha kwa viburi vyao, kwa kujua au kutokujua, ametengeneza picha kwa watanzania wanaona vile anavyokibeba kikundi cha wachache.

Nao wanakikundi kwa kutambua udhaifu wake, wanachofanya ni kumsifia 24 hours ili kujihakikishia usalama wa ofisi zao, wala sio kwa utendaji wao serikalini ambao kwa kiasi kikubwa hauridhishi.
Nyie ndio mna matatizo, pambaneni na matatizo yenu. Rais wetu hana tatizo lolote
 
Mkuu kwanza nikupongeze kwa ku argue kwa hoja vizuri kabisa. Usemayo ni kweli kabisa. Lakini nawewe si unafahamu kuwa makamu ni mshauri tu kulingana na katiba yetu? Kumbuka rais hashurutishwi kupokea ushauri kutoka kwa yeyote yule. Hata kama Samia hakukubaliana naye, angefanyaje?.
Angejiuzulu.
 
Katiba imekushinda, Tume huru imekushinda, mikutano ya wanasiasa wenzio imekushinda
Mkuu technically , unaonyesha una haraka sana na mcheche!, katiba ni mchakato Doctor Mama aliisha lisemea kupanga ni kuchagua, amesema tujenge kwanza uchumi. Tume huru na mikutano ya vyama hili liko ndani ya uwezo wake and it's just a matter of time atalimaliza. Vuta subra tumpe muda.
P
 
ssass
Raisi wa Jamhuri Ya Muungano wa TZ halazimiki kufuata ushauri wa mtu yeyote (Katiba JMT,1977) Kifungu sikumbuki
Watu wakiambiwa katiba mpya wanashupaza shingo
sasa hata kama wewe ni Rais ufuate ushauri wa kila mtu si itakuwa balaa
 
Mkuu technically , unaonyesha una haraka sana na mcheche!, katiba ni mchakato Doctor Mama aliisha lisemea kupanga ni kuchagua, amesema tujenge kwanza uchumi. Tume huru na mikutano ya vyama hili liko ndani ya uwezo wake and it's just a matter of time atalimaliza. Vuta subra tumpe muda.
P
Kweli mzee Pascal Mayalla wahenga walisema "subira yavuta heri". Lakini wahenga hao hao wakasema tena, "ngoja ngoja yaumiza matumbo".
 
Wengi wanaopiga kelele wanakupenda sana.

Wachache wanaokusifia kwa kila jambo wanakupoteza na wanakuingiza mkenge shutuka.

Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu watu wengi wanataka yafuatayo!!

Umeme kuunganishwa umepanda kutoka 27000 mpaka 320,000 ndugu yangu rais wangu nakupenda Sana hapa wanachi wengi hawajafurahia na wanasononeka Sana.

Wananchi wengi hawapendezwi na jinsi wahuni ndani ya ccm wanavyomtukana Rais aliyepita Magufuli Kama vile hakuna jambo jema alilofanya nawaomba hii ajenda muachane nayo.

Mambo yote mabaya yanayomhusu Magufuli achana nayo Kama ulivyomsimanga juzi kuhusu vifaranga ndugu yangu achana na mtu aliyelala Marehemu hasemwi.

Rais wangu achana na wahujumu uchumi kupita wizara ya nishati wanafanya biashara za solar na generator wakiongozwa na February Hawa watakuangusha mvua imenyesha ya kutosha umeme uwake...!

Rais wangu Wizara ya nishati inahujumiwa na serikali yenyewe na kuna tetesi za kupandishwa kwa unit ya umeme kutoka 300+ kwenda 500+ kwa unit moja huu ni uhujumu uchumi wa wazi wazi!!

Tatizo la maji lisijirudie tena naona baada ya mto ruvu kujaa mmesahau tena na kuanza kukenua meno mwakani tutarudi kulekule mwakani.

Rais wangu acha kufurahisha genge la watu wachache ambao ni wahujumu uchumi wa nchi hii utachekwa pekee yako.

Kama wanavyomsimanga Magufuli na Jk na wewe unawatazama tu ndio hivyo hivyo watakutukana ukirudi Zanzibar.

Mambo ni mengi muda ni mchache ila nakupa tu tahadhari ukiendelea kusikiliza sauti za wachache na kuacha sauti za wengi by 2025 unaenda nyumbani.

Katiba imekushinda, Tume huru imekushinda, mikutano ya wanasiasa wenzio imekushinda, Maji yamekushinda, Uchumi umekushinda, mfumuko wa bei umekushinda, Bandari imekushinda, umeme ndio unapuyanga, Reli ndio hiyo umebariki tuletewe mabehewa fake upuuzi mtupu na nauri za dar dodoma eti elf 55😀😀

Nchi ipo kukopa tu na kuongeza deni la taifa wakati kinachokopwa Wala hakijulikani kinaenda wapi?

Chukua tahadhari wanaokupaka mafuta ndio watakuangusha.

Acha kumsema Magufuli, pia piga marufuku watu wote kumsema vibaya mtu aliyekufa.

Acha kuzunguka na kuzurura kaa ofisini pitia mafaili ya watu na watumbue watu Linda pesa za nchi by 2025 utakuja kunishukuru nimekaa pale!!.
Mungu anaipenda sana Tanzania.

Imeandikwa, Nitampiga Mchungaji na kondoo watatawanyika,

Bt Alipopigwa Mchungaji na maharamia Bado kondoo walirudi salama zizini.

Mungu Amesikia vilio vya watu wake, na anashuka tena kutenda HAKI na HUKUMU.

Mungu amekukumbuka ee Tanzania.

God has remembered our land Tanzania.

Justice is coming. Ameeeen.
 
Wengi wanaopiga kelele wanakupenda sana.

Wachache wanaokusifia kwa kila jambo wanakupoteza na wanakuingiza mkenge shutuka.

Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu watu wengi wanataka yafuatayo!!

Umeme kuunganishwa umepanda kutoka 27000 mpaka 320,000 ndugu yangu rais wangu nakupenda Sana hapa wanachi wengi hawajafurahia na wanasononeka Sana.

Wananchi wengi hawapendezwi na jinsi wahuni ndani ya ccm wanavyomtukana Rais aliyepita Magufuli Kama vile hakuna jambo jema alilofanya nawaomba hii ajenda muachane nayo.

Mambo yote mabaya yanayomhusu Magufuli achana nayo Kama ulivyomsimanga juzi kuhusu vifaranga ndugu yangu achana na mtu aliyelala Marehemu hasemwi.

Rais wangu achana na wahujumu uchumi kupita wizara ya nishati wanafanya biashara za solar na generator wakiongozwa na February Hawa watakuangusha mvua imenyesha ya kutosha umeme uwake...!

Rais wangu Wizara ya nishati inahujumiwa na serikali yenyewe na kuna tetesi za kupandishwa kwa unit ya umeme kutoka 300+ kwenda 500+ kwa unit moja huu ni uhujumu uchumi wa wazi wazi!!

Tatizo la maji lisijirudie tena naona baada ya mto ruvu kujaa mmesahau tena na kuanza kukenua meno mwakani tutarudi kulekule mwakani.

Rais wangu acha kufurahisha genge la watu wachache ambao ni wahujumu uchumi wa nchi hii utachekwa pekee yako.

Kama wanavyomsimanga Magufuli na Jk na wewe unawatazama tu ndio hivyo hivyo watakutukana ukirudi Zanzibar.

Mambo ni mengi muda ni mchache ila nakupa tu tahadhari ukiendelea kusikiliza sauti za wachache na kuacha sauti za wengi by 2025 unaenda nyumbani.

Katiba imekushinda, Tume huru imekushinda, mikutano ya wanasiasa wenzio imekushinda, Maji yamekushinda, Uchumi umekushinda, mfumuko wa bei umekushinda, Bandari imekushinda, umeme ndio unapuyanga, Reli ndio hiyo umebariki tuletewe mabehewa fake upuuzi mtupu na nauri za dar dodoma eti elf 55[emoji3][emoji3]

Nchi ipo kukopa tu na kuongeza deni la taifa wakati kinachokopwa Wala hakijulikani kinaenda wapi?

Chukua tahadhari wanaokupaka mafuta ndio watakuangusha.

Acha kumsema Magufuli, pia piga marufuku watu wote kumsema vibaya mtu aliyekufa.

Acha kuzunguka na kuzurura kaa ofisini pitia mafaili ya watu na watumbue watu Linda pesa za nchi by 2025 utakuja kunishukuru nimekaa pale!!.
Kama tungekuwa na katiba ya wananchi,viongozi ndio wangekuwa wanatusikia na kutubembeleza lakini kwa hii yakwenu tunawabembela na kuwapaka mafuta
 
Wengi wanaopiga kelele wanakupenda sana.

Wachache wanaokusifia kwa kila jambo wanakupoteza na wanakuingiza mkenge shutuka.

Sauti ya wengi ni sauti ya Mungu watu wengi wanataka yafuatayo!!

Umeme kuunganishwa umepanda kutoka 27000 mpaka 320,000 ndugu yangu rais wangu nakupenda Sana hapa wanachi wengi hawajafurahia na wanasononeka Sana.

Wananchi wengi hawapendezwi na jinsi wahuni ndani ya ccm wanavyomtukana Rais aliyepita Magufuli Kama vile hakuna jambo jema alilofanya nawaomba hii ajenda muachane nayo.

Mambo yote mabaya yanayomhusu Magufuli achana nayo Kama ulivyomsimanga juzi kuhusu vifaranga ndugu yangu achana na mtu aliyelala Marehemu hasemwi.

Rais wangu achana na wahujumu uchumi kupita wizara ya nishati wanafanya biashara za solar na generator wakiongozwa na February Hawa watakuangusha mvua imenyesha ya kutosha umeme uwake...!

Rais wangu Wizara ya nishati inahujumiwa na serikali yenyewe na kuna tetesi za kupandishwa kwa unit ya umeme kutoka 300+ kwenda 500+ kwa unit moja huu ni uhujumu uchumi wa wazi wazi!!

Tatizo la maji lisijirudie tena naona baada ya mto ruvu kujaa mmesahau tena na kuanza kukenua meno mwakani tutarudi kulekule mwakani.

Rais wangu acha kufurahisha genge la watu wachache ambao ni wahujumu uchumi wa nchi hii utachekwa pekee yako.

Kama wanavyomsimanga Magufuli na Jk na wewe unawatazama tu ndio hivyo hivyo watakutukana ukirudi Zanzibar.

Mambo ni mengi muda ni mchache ila nakupa tu tahadhari ukiendelea kusikiliza sauti za wachache na kuacha sauti za wengi by 2025 unaenda nyumbani.

Katiba imekushinda, Tume huru imekushinda, mikutano ya wanasiasa wenzio imekushinda, Maji yamekushinda, Uchumi umekushinda, mfumuko wa bei umekushinda, Bandari imekushinda, umeme ndio unapuyanga, Reli ndio hiyo umebariki tuletewe mabehewa fake upuuzi mtupu na nauri za dar dodoma eti elf 55😀😀

Nchi ipo kukopa tu na kuongeza deni la taifa wakati kinachokopwa Wala hakijulikani kinaenda wapi?

Chukua tahadhari wanaokupaka mafuta ndio watakuangusha.

Acha kumsema Magufuli, pia piga marufuku watu wote kumsema vibaya mtu aliyekufa.

Acha kuzunguka na kuzurura kaa ofisini pitia mafaili ya watu na watumbue watu Linda pesa za nchi by 2025 utakuja kunishukuru nimekaa pale!!.
1670688960841.png
 
Unajisumbua tu mkuu.

Swala la umeme akimuuliza waziri lazima apigwe kiswahili.

Kama ana mwita JANU unafikiri kuna kitu serious kinaendelea hapo??
 
Back
Top Bottom