Rais Samia Suluhu umeanza kuwa Dikteta mapema kuliko hayati John Pombe Magufuli

Rais Samia Suluhu umeanza kuwa Dikteta mapema kuliko hayati John Pombe Magufuli

Mshana, nakuapia Sasa tutaanza kushuhudia utekaji, mauaji, kubambikiwa kesi, upotezwaji na mengine mengi maovu ya Jiwe. Hii ni kauli ya kifo, maafa na maangamizi. Huyu mwanamke atakuwa hatari kuliko Magufuli nakwambia.

Sasa ukitaka kuanzisha chama utakienezaje? Huyu ni hatari Sana. Simpendi katu maana tunakwenda kufa
Kama kawa, usiombe ukutane na mchawi mwanamke. Hawana huruma hakika. Ila mama amebow kwa wahafidhina walioko ndani ya CCM kwani hajiamini naona. Nina hakika yeye kama yeye angeyaka utawala wa sheria ila ndani ya CCM kuna watu wameonja nyama ya mtu hawawezi kuacha.
 
Vijana mnakosea hapo tu! Unaweza ukawa na hoja yenye nguvu lakini maneno yenu ya shombo ndio yanaharibu hata hiyo hoja yenyewe mkaonekana wahuni.
Mjifunze kuhsehimu watu na maoni yao. By the way mimi ukinitusi na kunikashifu sibomoki wala mshahara wangu haupungui
Si kweli kwamba nimekutusi. Nimekutukana tusi gani? Mimi si kijana na situkani mtu. Nakuheshimu wewe lakini nashutumu unachosimamia.
 
Hayati Magufuli alisema analeta Maendeleo. Leo hakuna anayemkumbuka Magufuli na habari zake za Maendeleo bali anakumbukwa kwa kuminya na kukandamiza haki za Raia.
Maoni na mtazamo wako binafsi usiufanye kuwa maoni na mtazamo wa watanzania wote. Watu wenye mitazamo finyu kama wewe ndo wanaweza kuwa na generalizesheni za kitoto hivi.
 
Maoni na mtazamo wako binafsi usiufanye kuwa maoni na mtazamo wa watanzania wote. Watu wenye mitazamo finyu kama wewe ndo wanaweza kuwa na generalizesheni za kitoto hivi.
Lipa kodi ya simu, Huoni mbele
Hujui lolote

Ulienda shule kuokoteza maneno ya kiingereza
 
Hiyo Katiba iangaliwe upya, Mikutano ya kisiasa ISIWEPO mpaka muda wa Uchaguzi utakapofika.

Nchi zenye Demokrasia tangu miaka 200 iliyopita wanafanya siasa za hadharani inapokaribia Uchaguzi husika.

Sisi Tanzania tunataka miaka mitano mfululizo kupanda Majukwaani kueneza Siasa za uongo, chuki na kutoridhika na matokeo.

Leo Baiden kashinda Urais USA hatujaona Trump na wenzake wapo barabarani wakiendeleza siasa na malumbano
Hivi kwa nini mnapenda kusema uongo? Au mnadhani watu wote ni malimbukeni kama nyinyi?

Hakuna nchi yenye demokrasia kamili, kuanzia Marekani mpaka India, inayopanhia raia zake kipindi au mahali pa kufanya siasa. Marekani ndio kabisa. Tangu Trump ashindwe kwenye uchaguzi amekuwa akifanya kampeni ya kutaka matokeo yabatilishwe. Hata miezi sita haijapita toka Rais mpya aapishwe tayari anafanya mikutano ya hadhara akidai kuwa Biden alimuibia ushindi na si Rais wa halali.

Acolytes wake wanazunguka nchi nzima kutaka kubadilisha taratibu za upigaji kura ili kuhakikisha democrats hawatakuja kushinda tena. Wanafanya mikutano ya hadhara, wanafanya ya ndani (town hall meetings) na wanatumia media kikamilifu kuendeleza ajenda zao bila kubughudhiwa.

Democrats nao wanajibu mapigo. Wanaandaa maandamano na mikutano kuwapinga wasio mtakia mema Biden. Na kote huko hamna kiongozi (Rais au Gavana) anae agiza vyombo vya usalama viwashughulikie.

Katika demokrasi inayojitambua, kampeni za uchaguzi ujao zinaanza pale matokeo ya uchaguzi wa sasa yanapotangazwa. Haya mambo ya kumpangia mpinzani wako namna ya yeye kufanya siasa, muda wa kufanya siasa, mahali pa kufanya siasa na hata maneno atakayosema si ya demokrasi bali ni ya pseudo demokrasi!

Tunaona charade ya upinzani kuzuiwa kufanya shughuli zao wakati chama tawala wana carte blanche ya kufanya watakalo.

Leo wapinzani ambao ni raia wa nchi hii wanazuiwa kujadili na kuichambua Katiba halafu bado mnataka tuamini kuwa ni sehemu ya demokrasia? Watu wanakamatwa hotelini ili kuwazuia kuhudhuria kikao halali chini ya sheria na bado mnadai ni sehemu ya demokrasia? Leo kiongozi wa upinzani anaambiwa kuwa anatakiwa kufahamisha polisi akiingia kwenye mji mwingine kufanya shughuli za chama chake na mnadai hiyo ni demokrasi? Msitufanye wajinga.

Amandla...
 
Mikutano ya kisiasa hadharani sasa hv ya kazi gani mkuu? kama sio kuleta fujo tu!

Mama yupo sahihi kbs. Amani ndo kipaumbele. Kama katiba inasema tofauti basi iangaliwe upya!

Mikutano ya kisiasa hadharani ifanywe miaka ya uchaguzi
2024- Serikali za mitaa
2025- uchaguzi mkuu
Tumia Akili au Umetolewa Ubongo Katiba Mbovu iliyopo inaruhusu Mikutano Yeye Anazuia kwa Katiba Gani Naona Wamekutoa Ubongo
Screenshot_20210716-160038_Twitter.jpg
 
Yaaani mnampiga mkwala rais kisha mmataka akae kimya kuwafurahisha daaah akili matope si mlisema mtatumia wembe ule ule tumieni sasa.
Bunduki na mabomu yao ni maandishi yao humu jukwaani.

Silaha zenye nguvu mwisho mlangoni kurudi ilipo simu au laptop.
 
Ukishaona Rais fulani wa Afrika marafiki zake pamoja na wahisani wake wakuu ni Burundi na Zimbabwe jua kuwa hamna Rais humo

AUUsW.jpg
 
Chama chochote kishike dola mambo ni hayo hayo wacha Samia akupigeni spana hamtaki kumuheshimu na mnamzonga,ndio Kwanza miezi minne mnampanda kichwani
 
Kauli ya Rais Samia kuminya uhuru wa Raia na vyama vyao vya siasa kwa kutozingatia katiba na sheria ameingia kwenye rekodi mpya kama Rais Mwanamke wa kwanza Africa kuwa Dikteta.

Siku ya 101 madarakani, Rais Samia Suluhu tayari ameanza kulewa sifa na mapambio. Ameamua kuendelea kuminya uhuru wa vyama vya siasa kufanya mihadhara kwa kutumia utashi wake na siyo katiba iliyomfanya Yeye awe Rais bila kupigwa kura za wananchi.

Hakuna uchumi bila haki na uhuru wa watu, Tangu tupate uhuru kwa miaka zaidi ya ishirini na nne ya chama kimoja hakuna Uchumi wowote uliosimama, Uchumi ulianza kusimama wakati wa vyama vingi vya kisiasa na huu ni wakati wa Hayati Ben Mkapa, Hayati Ben Mkapa alisimamia uhuru na kujenga mfumo wa kitaasisi.

Mama Samia ameanza kuonyesha sura yake halisi ya udikiteta mapema sana, Atambue na akumbuke hakuna aliyempigia kura kwenye sanduku kama Rais wa nchi bali amepata Urais kwa kufuata katiba ya nchi, Wananchi wa Tanzania ni waelewa ndio maana Mama alipoapishwa kwa kufuata katiba hakuna aliyelalamika kwenye mitandao ya kijamii, Kuanza kuvunja katiba siku ya 101 kisa umesifiwa sana Jiandae kisaikolojia kwa watu kukusema kimataifa kama mtangulizi wako na kitakachofuatwa ni wewe kuhojiwa maswali Magumu na vyombo vya kimataifa ukajikuta unadhalilika na kutafuta mchawi nani.

Chuki ambayo umejenga kwa kauli yako ya kusema hakuna vyama vya siasa kufanya mikutano ya hadhara umeitoa kwa kutumia sheria na katiba ipi? Wewe uliapishwa kwa kufuata katiba kwanini umeanza kuharibu na kupindisha katiba ya nchi?

Kauli yako ya kuminya uhuru wa siasa imekuharibia kila kitu na sasa mjadala umeanza kuwa mkali zaidi, Jiandae Kwa watu kukusema hovyo na kukudhalilisha zaidi ya mtangulizi wako.

Kila kauli ina madhara yake, Kauli yako ya kuwa unajenga Uchumi, Hayati Magufuli alisema analeta Maendeleo. Leo hakuna anayemkumbuka Magufuli na habari zake za Maendeleo bali anakumbukwa kwa kuminya na kukandamiza haki za Raia.

Serikali iwape watu uhuru wao, Kuna tetesi zilizagaa kuwa hata wewe watu walitaka usipewe Urais kwani waliona hutaweza lakini kuna kundi likasimamia katiba na ukaapishwa kuwa Rais, Kwanini wewe unavunja katiba?

---
UPDATE tarehe 02/07/2021
Mkutano wa wanawake wa Chadema (Bawacha) uliokuwa unafanyika kwenye ukumbi mikocheni umevamiwa na polisi kwa amri toka juu, Wamefukuzwa ndani ya dakika 30

Serikali ya Samia Suluhu ni ya kidikiteta kuliko ya Magufuli, Hawajaangalia gharama za ukumbi, Polisi kwa amri toka juu wameuvuruga mkutano


Updates 17/07/2021

Sasa ni marufuku kujadili mambo ya tozo za miamala ya simu iliyokuwa ya kinyonyaji, Mama amezuia mjadala wa katiba mpya, Ukitaka kujadili katiba mikusanyiko inavamiwa na polisi kwa amri toka kwa Rais Samia
Ebu tutajie nchi moja tu duniani baada ya uchaguzi na serikali kutangazwa vyama vya siasa vinaendelea kufanya mikutano ya hadhara? Ata hiyo mikutano mkiruhusiwa mnazungumza Nini zaidi ya kueneza chuki? Mmesharuhusiwa kufanya mikutano ya ndani fanyeni matangazo na watu watakuja..magu nilikuwa simpendi lakini kwa hili nilimuunga mkono maaana haiwezekani mtu anafanya kazi wengine wanaangaika kufanya mikutano ya kuharibu....
 
Ebu tutajie nchi moja tu duniani baada ya uchaguzi na serikali kutangazwa vyama vya siasa vinaendelea kufanya mikutano ya hadhara? Ata hiyo mikutano mkiruhusiwa mnazungumza Nini zaidi ya kueneza chuki? Mmesharuhusiwa kufanya mikutano ya ndani fanyeni matangazo na watu watakuja..magu nilikuwa simpendi lakini kwa hili nilimuunga mkono maaana haiwezekani mtu anafanya kazi wengine wanaangaika kufanya mikutano ya kuharibu....
Imeisha hiyo
 
Back
Top Bottom