andjul
JF-Expert Member
- Dec 14, 2013
- 18,773
- 119,820
Nakubaliana na wewe mkuu.Ipo miji ambayo ina hivyo vitu kwa udogo toka kitambo na ina utalii ndani yake na mazingira yake yana ruhusu tatizo haisemwi. Mfano Tanga ni mji ambao hautajwi kwenye vitu kama hivi lakini ni mji ambao ungesimamiwa vzr naimani ungekua karibu na ilivyo dar.
Lakini, Tanzania imebahatika kwenye vivutio,karibu mikoa yote ina vivutio.
Hizi shughuli za kimataifa zinatakiwa ziwahamasishe wawekezaji wa ndani na nje wakishikwa mkono na serikali,kwenda kuwekeza kwenye maeneo ambayo bado hayajaamka. Rejea stand za mabus zilizo jengwa nje ya maeneo yaliyo changamka, wafanyabiashara wamezifuata zilipo.
Kama ni kiwanja kikubwa cha mpira hata Mtwara au Kigoma kinaweza kujengwa na kikaenda sambamba na ujenzi wa miundombinu husika, lakini kung'ang'ania kila kitu kiwe miji fulani matokeo yake ni watu kujazana kwenye hiyo miji huku mingine ikibaki miji mfu