Rais Samia: Tulikaa kikao na Katibu Mkuu Kiongozi na Waziri wa Fedha kujadili mkopo. Iko wapi nafasi ya Baraza la Mawaziri?

Rais kasema alikaa na nani?wewe unaeleza taratibu, bibi yeye anaeleza kilichofanyika. Kwa akili ya kawaida kuonyesha alipata idhini asingetaja hako kakikao bali angetaja kikao cha baraza
Story ya uzi huu imeanzia katikati labda kwa malengo ya kisiasa. Mama alipigiwa simu na Mwigulu usiku akamwambia wataongea kesho asubuhi.

Ndio akamuita katibu mkuu kiongozi, waziri pamoja na yeye. Hicho ni kikao cha kwanza kabla ya kuitisha baraza la mawaziri.

JPM alikuwa anawapigia simu mawaziri wake mmoja mmoja hadi saa kumi za usiku, ni masuala ya kawaida ya kikazi. Wakishakubaliana ndio anaitisha kikao cha baraza la mawaziri.
 
Ushatoka chato kufagia kwenye kaburi la yule shetani?

Enzi zake alikuwa alfa na omega haitaji hata mkewe achilia mbali bunge na mawaziri amshauri.

Na maamuzi yake ndo kila kitu.

Muacheni mama afanye apendavyo wanafki wakubwa nyinyi.
Hahahahahaha utakonda sanaaa kumuwaza mtu ambae yuko Kaburini.
Tulia kama alikufukuza kazi kwa cheti feki usilete povu kali kiasi hicho mpaka mtu anajuaa huyu hamnazo

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
 
Hata mimi nilijiuliza sana, nnchi inaendeshwa kama kampuni binafsi
 
Faida ni ipi sasa mpaka sasa kama mafuta ya kula tu hayashikiki dukani
Faida ni ujenzi wa mashule ya sekondari nchi nzima. Ni ujenzi wa madaraja makubwa na madogo nchi nzima.

Mafuta kutoshikika pengine ni masuala ya inflation, na haya yapo dunia nzima. USA walikutana na joto ya jiwe baada ya petrol kupanda bei miaka michache iliyopita.
 
Mashule ambayo yanazalisha jobless tu hamna kingine cha maana kweli?
 
Kipindi cha awamu ya tano mlikuwa mkijiita wazalendo hamkujisumbua kuhoji chochote ila mlijikita kuwakatisha tamaa wale waliokuwa wanahoji. Je, uzalendo wenu umeishia wapi? Ama mlikuwa mnaongozwa kwa mihemko tu? Ama mlikuwa mnapata chochote ili kujiita wazalendo?
 
Mashule ambayo yanazalisha jobless tu hamna kingine cha maana kweli?
Ni bora ujenge kwa mategemeo kwamba pesa zikizidi kupatikana utaboresha viwango vya ufundishaji wa waalimu wao.

Ni bora ujenge mashule kwa matarajio kwamba kazi zitakuja kupatikana siku zijazo. Binadamu angekuwa anatanguliza mawazo ya kufeli nina uhakika wasingekuwa na umuhimu watu wanaohubiri matumaini (motivational speakers).
 
Uamuzi kama huu unafanywa na waziri ambae amesema mkopo ni poa tu kwa sababu hakuna atakaegongewa hodi kulipa deni la Taifa...

Tunahitaji sheria za uratibu wa mikopo...

Huyo mwigulu ni mpumbavu kuliko maelezo! Eti hakuna atakaye gongewa kulipa Deni la taifa! Khaaa ! Mbona hodi ni kila dakika!! Ukifanya muamala ni hodi hiyo ! Ukinunua umeme hodiii !! Ukinunua chochote kile ni hodiii ! Kenge kabisa Huyu jamaa
 
Wakati huo watoto hawazaliwi sio!? Madarasa yataendelea kuwa hafifu tu sio kipaumbele kwa sasa halafu ni aibu mtu kukopa hela badala ufanyie investment unakopa hela ya kulipia madeni ya nyuma na kutumia😅
 
Ushatoka chato kufagia kwenye kaburi la yule shetani?

Enzi zake alikuwa alfa na omega haitaji hata mkewe achilia mbali bunge na mawaziri amshauri.

Na maamuzi yake ndo kila kitu.

Muacheni mama afanye apendavyo wanafki wakubwa nyinyi.

Afanye apendavyo duuh[emoji3]
 
Wakati huo watoto hawazaliwi sio!? Madarasa yataendelea kuwa hafifu tu sio kipaumbele kwa sasa halafu ni aibu mtu kukopa hela badala ufanyie investment unakopa hela ya kulipia madeni ya nyuma na kutumia😅
Kwako wewe sio kipaumbele. Kwa serikali na mipango yake ni kipaumbele muhimu.
 
Unajua maana ya DENI KUIVA??? Hapo MAGUFULI ALICHUKUA MKOPO HIVYO MAREJESHO YAMESHAFIKA. KWAHIYO MAMA SAMIA KAONA BORA WAANZE KULIPA HAYO MADENI. Tatizo letu hatufuatilii mambo na kuona kama Mama Samia haya madeni ndio msababishaji au la.
Kukopa deni Ili kulipa deni hapa akili imeenda likizo
 
Kwanini Ndugai hakuanza kuhoji mikopo iliyokuwa inakopwa kwa siri bila bunge kuhusishwa na manunuzi ya ndege nakadhalika pasipo muhuri wa bunge ama kujadiliwa? Kwanini aanze kuhoji wakati huu tena mkopo wa wazi kabisa ambao umma umefahamishwa pamoja na matumizi yake kuwa ya wazi.

Hapo ndipo wenye akili wanapohoji uhalali wa Ndugai kuhoji mkopo wa sasa tena wa 1.3 tr nakuacha mikopo kibao ya awamu ya tano iliyokopwa gizani.

CAG katika ukaguzi wake alibaini kutoonekana kwa matumizi ya zaidi zaidi ya 1.5 trilion lakini Ndugai hakuhoji badala yake CAG aliondolewa kinyume cha sheria.
 
Hahahahahaha utakonda sanaaa kumuwaza mtu ambae yuko Kaburini.
Tulia kama alikufukuza kazi kwa cheti feki usilete povu kali kiasi hicho mpaka mtu anajuaa huyu hamnazo

Sent from my SM-A125F using JamiiForums mobile app
Cheti changu wewe na ukoo wenu wote muungane hamuwez kufikia hata robo ya daraja lake.

Na hata kama ningefukuzwa kwa cheti feki bado haiondoi ukweli yule muhutu alikuwa ni shetani.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…