Rais Samia: Tumeshalipia treni 19 za Umeme na mabehewa 89, Seti 10 za treni na mabehewa 80 kwaajili ya mizigo

Rais Samia: Tumeshalipia treni 19 za Umeme na mabehewa 89, Seti 10 za treni na mabehewa 80 kwaajili ya mizigo

Miradi yote iliyoachwa na Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli Rais Samia Suluhu Hassan anaitekeleza kwa 100%

Sihiyo tu tayari mingine mipya inaendelea na Ujenzi,

Tunawajibu wa kumwombea Mama huyu,
 
Wakati mwingine waaminini walioko Serikalini. They're too Tanzanians, educated and some are patriotic and highly exposured.
Hawahaminic ,wenda wanaoaminika wako nje ya mfumo, tumeona wasomi, maprof, wawapo ndani ya mfumo kuleta matokeo chanya KWa kutumia elim zao imekuachangamoto,
 
..Mkandarasi wa Kituruki inaelekea amekata pumzi.

..Alitakiwa awe ameshakabidhi kipande cha SGR toka Dar kwenda Moro.
Swala sio kukata pumzi bali inatakiwa hela ipelekwe kwa wakati sasa hela ikicheleweshwa unategemea kazi itamalizikaje kwa wakati?
 
Tusidanyanyane mkuu

Waziri wa Nishati akibakia huyu huyu itakua jambo la kawaida kabisa kwenda kuchomoana huko maporini.
Hahahahaahahah wahuni watazimikiwa na umeme porini kmmmk labda treni ibebe jenereta mgongoni kwake liwake umeme ukizima😅

Huu umeme wa Januari Marope ni jau kinyama hauwakagi masaa 24 bila kuzima!
 
Hapo kwenye treni ya mizigo Bora malori yapungue kariakoo
Lakini watakubali?wenye malori?
Nina wasiwasi hii treni inaweza isiishe
Hahahahah treni itafika na itaanza kazi ila haitamaliza miezi 6 lazma wataihujumu ili malori yao yaendelee kufanya kazi aidha kwa ku cancel trips na dana dana bila sababu za msingi ili kusudi watu wakate tamaa warudi kwenye malori😅!

Sema tu Magufuli aliwaza vizuri kuwa malori yaanzie usafirishaji kule mizani yatapakilia kwenye ICD kule mizani karibu na Chalinze. So msongamano utapungua mjini!
 
Miradi yote iliyoachwa na Hayati Dkt John John Joseph Pombe Magufuli Rais Samia Suluhu Hassan anaitekeleza kwa 100%

Sihiyo tu tayari mingine mipya inaendelea na Ujenzi,

Tunawajibu wa kumwombea Mama huyu,
Ni zaidi ya asilimia 100%. Tukiangalia urefu wa kilometa za reli na treni na mabehewa yote na mradi mzima kwa mwendo huu wa Rais, Mama Samia historia itampa zaidi nafasi kwa asilimia 65%

1.Jakaya Kikwete 21% za ubunifu,usanifu,tathmini na utekelezaji.

2.John Pombe Magufuli 30% utekelezaji hatua ya kwanza,ubunifu hasa kuongeza kipengele Cha umeme,usimamizi

3.Samaia S. Hassan 49% Iwapo Kuna uhai, Mama Samia akafanikiwa kutekeleza yaliyo kwenye mradi basi yeye ndiye atakayekuwa amebeba mzigo mkubwa wa utekelezaji na usimamizi wa mradi. Kwa hivi sasa ameshafanikiwa kujitengenezea karibu asilimia 25%
 
Asante mleta mada. Nina vimaswali vidogo.
1. Ni kampuni gani imepata tenda hii ya mabehewa?
2.Malipo yalifanyika lini?
2a. Ni nani wanahusika kuhakiki ubora wa mabehewa?
3. Mabehewa yatafika nchini lini?
4. Yataanza kutumika lini?
===
Natanguliza shukrani kwa majibu.
 
Asante mleta mada. Nina vimaswali vidogo.
1. Ni kampuni gani imepata tenda hii ya mabehewa?
2.Malipo yalifanyika lini?
2a. Ni nani wanahusika kuhakiki ubora wa mabehewa?
3. Mabehewa yatafika nchini lini?
4. Yataanza kutumika lini?
===
Natanguliza shukrani kwa majibu.
Rais kasema hayo mengine mtafute Kadogosa
 
Icho kipande si alipewa mchina au vipiii kapigwa chini mturuki kalamba bingo?

Mkuu hizi propaganda ni hatari hata huelewi kipi ni kipi. Hata hivyo anavyosema kanunua mama, ukifuatilia utakuta ukweli ni tofauti kabisa na kisemwacho.
 
WAKIONA HIVI UJUWE WANACHUKIA KWELI KWELI MAANA MAMBO YANAKWENDA TOFAUTI KABISA NA WALIVYOTEGEMEA
mradipic
Serikali imesema imeingia mkataba wa ununuzi wa mabehewa ya abiria 89, vichwa vya treni ya umeme 19, seti za treni za kisasa 10 zenye behewa 80 vikiwa na gharama Dola za Marekani milioni 381,428,465.

Hayo yamebainishwa leo Jumanne Desemba 28, 2021 na Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan katika hafla ya utiaji saini mkataba wa ujenzi wa reli ya kisasa (SGR) kipande cha tatu kutoka Makutupora hadi Tabora chenye urefu wa kilometa 368, kitakachogharimu Dola za Marekani bilioni 1.908 sawa Sh4.41 trilioni kati ya Shirika la Reli Tanzania (TRC) na Yapi Merkez kutoka Uturuki.

Amesema pamoja na hayo Serikali inaendelea kukamilisha ununuzi wa mabehewa ya mizigo 1430 yenye thamani dola za Marekani milioni 127,206,300.

“Nitumie fursa hii kuagiza wizara na TRC kuhakikisha kuwa inasimamia kwa karibu ili kasi ya ujenzi iendane na kasi ya kusimamia ununuzi wa vifaa hivyo. Hii itafanya vifaa viwe vimekamilika sambamba na kukamilika kwa ujenzi wa reli. Vinginevyo miundombinu ya reli itakamilika huku tukisubiri kuwasili kwa vifaa na kuhakikisha ubora unaendana na thamani ya fedha."

“Nasema hivi kwa sababu miezi michache nimekaa katika Serikali hii nimeona kuna mambo yanataka kuanza kufanyika na mimi sitakubali yafanyike. Kwamba mradi unasimamiwa na wizara kupitia sekta husika, anatafutwa mkandarasi anapopatikana anakuwa na wasemaji wengi ndani ya nchi, na hasemewi bure watu wanajua watavuna. Sasa nasema mimi sijali mkandarasi atasemewa na watu elfu ninachotaka kusema nataka reli iwe ya viwango tulivyokubaliana,” amesisitiza
 
Asante mleta mada. Nina vimaswali vidogo.
1. Ni kampuni gani imepata tenda hii ya mabehewa?
2.Malipo yalifanyika lini?
2a. Ni nani wanahusika kuhakiki ubora wa mabehewa?
3. Mabehewa yatafika nchini lini?
4. Yataanza kutumika lini?
===
Natanguliza shukrani kwa majibu.
Ngoja kwanza
Kuna vile vichwa vilikamatwa bandarini na magu
Viko wapi vile vingetufaa sana
 
Huu mradi unaonekana ni pasua kichwa.tungekuwa na plani ya kuishia kwanza dodoma then tunacheki situation inaendaje.
 
Kuna wakati huyu rais anaongea vitu ambavyo havina uhalisia.Anasema.kwa muda huu mfupi aliokaa serikalini
amegundua mengi, ina maana.tangu mwaka 2015
hakuwa serikalini?.Au ameingia serikalini baada ya kifo cha JPM ?
 
Kuna wakati huyu rais anaongea vitu ambavyo havina uhalisia.Anasema.kwa muda huu mfupi aliokaa serikalini
amegundua mengi, ina maana.tangu mwaka 2015
hakuwa serikalini?.Au ameingia serikalini baada ya kifo cha JPM ?
Kwani magu nae si alikuwemo serikalini tangu 1995?
Mbona vituko alivianza baada ya kupata urais?
 
Back
Top Bottom